JK ilikua atimukie CHADEMA: Absalom Kibanda

tusubiri mapinduzi ya kweli? hata CDM sina imani nao.....magamba wana Network ktk vyama vyote hapa nchini......hata sasa EL ametishia kwenda CDM wakiendelea na ajenda ya MAGAMBA..

Kwa hiyo CHADEMA ni mwavuli wao?

Natamani CCJ ingesajiliwa tujue ukweli zaidi wa siri ya CCM......Tendwa anajua undani wake ,najinsi kilivyozuiliwa kwa nguvu zote.

Hata JUKWAA LA KATIBA ni ujanja ujanja wa mafisadi ili nchi isitawalike......hawana msaada wowote.Wananchi acheeni ushabiki wa kisiasa kama mnataka amani .

Tunaanzisha chama Kipya ambacho kitafanya mapinduzi ya kweli......Tunaomba support yenu muda ukifika.


:smash:
CHADEMA wako makini, hawawezi kujichafua kwa kumkaribisha EL ndani ya chama chao.
 
Watu hawawezi kulazimishwa kujadili hoja kwa uwepo wa watu wengi hiyo ni silka yao ya kujadili watu badala ya hoja.
 
CHADEMA wako makini, hawawezi kujichafua kwa kumkaribisha EL ndani ya chama chao.

Mkuu, sıasa nı mchezo mchafu na lolote lınawezekana!
CDM/ENL wapo/yupo tayalı kujısafısha na kujıamınısha kwa umma yakwamba yeye hana makosa na Wadanganyıka wakaamını hılo pamoja na povu jıngı kwenye majukwaa wanalobubujıka WanaCDM kuhusu ufısadı wa huyu Mamvı.
Nınauhakıka huo!
 
Hili nalifahamu, kwamba ndilo lililofanya JK apitishwe kuwa mgombea uraisi, baada ya kumwambia Mkapa kwa uwazi kabisa kwamba kama wasingempitisha angehamia upinzani na alikuwa na uhakika wa kushinda. Mkapa akaogopa, akamwambia basi nitakupitisha ila na wewe unilinde utakapokuwa raisi. Wakapeana mkono wa ahadi (kumbuka kauli za JK za mwacheni mzee apumzike mambo yalipomgeukia Mkapa). Zaidi ya hilo ninaloelewa ni kwamba Sitta ndie aliyekuwa "the brain" nyuma ya mkakati huu wa uliomweka Mkapa kwenye hali ngumu kimaamuzi, japo JK, Rostam na Lowasaa walikuja kumtupa Sitta kama ganda la ndizi! Hasira ya Sitta ya sasa imetoka mbali!

Umenena Mkuu engineer wa mambo hayo wakati ule ni SITTA,na huyu RA alidandia UPEPO baada ya kuona treni ya UPANDE aliopo HAITASHINDANA NA NGUVU YA KIKWETE UKIZINGATIA YEYE AMEKAA ZAIDI KIMASLAHI YAKE.
 
Kibanda ni mtu aliyekata tamaa,ana chuki na kikwete baada ya kukosa utaji ikulu kama alivotarajia baada ya uchaguzi mkuu 2005 kikwete alipoingia madarakani.asitudanganye tunamjua vizuri.
 
Kwa hiyo huyu jamaa anataka kutudanganya kuwa Chadema wasingetoka nje wabunge wa ccm wangeujadili muswada?! Kumbe basi akili zao zimeshikwa na Chadema!! Na atasemaje kuhusu ule mkutano mwingine wa bunge ambao walibaki wanamjadili na kumtukana Lissu hadi wengine wakaanza kufundisha tafsiri ya majina yake? Mbona Chadema hawakuwa wametoka nje?? Mawazo haya kuwa ccm walishindwa kujadili muswada kwa sababu ya Chadema kutoka nje ni upotoshaji uliopindukia.

Hili nilitaka na mimi nilisemee. Bwana Absalom naona uchambuzio wako kwenye hili haujakaa vizuri. CHADEMA walijua kwamba hata kama wangebaki ndani na kujadili bado CCM na CUF kwa uwingi na ujinga wao wangepitisha tu muswada ule. Na isitoshe, hotuba ya Tundu Lissu ilijitosheleza kabisa, hakukuwa na haja ya CHADEMA kuanza kupigizana kelele na CCM na CUF. Kutoka nje kuonyesha msimamo wao kwamba hawakubaliani na kinachoendelea haikuwa upotevu wa nafasi yoyote muhimu kwenye mjadala huo.
 
Kibanda ni mtu aliyekata tamaa,ana chuki na kikwete baada ya kukosa utaji ikulu kama alivotarajia baada ya uchaguzi mkuu 2005 kikwete alipoingia madarakani.asitudanganye tunamjua vizuri.
 
:A S-confused1:kama ingetokea angekuwa ameishafukuzwa maana thinking capacity is very LOW:A S 112::A S 112:
 
....Kikwete analikumbuka hilo, ndio maana anamkumbatia Nape na kuona hoja ya ccj sio issue, ila asiwabeze cdm maana Mkapa na chama chake wasingeshtuka angekuwa raisi wa nchi hii kupitia cdm, kwa vile basi shida yake ilikuwa ni urais alikuwa tayari kuingia chama chochote ilimradi afanikiwe hilo; asiwabeze cdm,

Brother, shida hapa si CCJ au CHADEMA, ni ushamba tu wa kisiasa na uelewa mdogo wa akina Mgeja unaowafanya watu washangae mtu anapotaka kutumia haki yake ya kikatiba kuhamia chama kingine!
 
Si kweli kama CDM wangebaki bungeni kujadili muswada wa katiba ingebadilisha uelekeo! Nawapa 5 CDM kwa kutoshiriki mjadala huo kwani watu wasingewatofautisha. Kususia ni namna nyingine ya kutokubaliana na kilichokuwa kikiendelea hasa ikizingatia kuwa hata wangetoa maoni mazuri kiasi gani ya kuboresha muswada huo kisingebadilika kitu. kwangu mie walivyofanya CDM ni sawa tu!
 
Greenstar wewe ni pandikizi la Magamba,usiongopee watu utawaanzishia chama cha kweli,si mlianzisha CCJ mbona mmeiua?tuna vyama vingi sana TZ,tutafakari ni chama gani si cha kifisadi na kinawatetea kweli wanyonge na kisha tukiunge mkono,kikubwa ni kufanya tafakari ya kina kwa kujiwekea vigezo kila mtu kwa nafasi yake ili kubaini ni chama gani kinahitaji kupewa support na sio kutuambia tuanzishe chama kingine,greenstar nina mashaka na ushauri wako.
 
Wana CCM Zanzibar walikua na fursa ya kuendeleza utaratibu wa Ki-CCM kuachiana wakati Mkapa anaondoka,lakini kwasababu zao za chuki na ubaguzi walimtosa Salim A Salim kwasababu tu ni Mpemba na siyo mwana ASP asilia. Hiyo dhambi itawaandama siku zote kama watabakia ktk Muungano maana CCM haitafanya kosa la kumteua Mzanzibari kuwa mgombea u-Rais wakati inafahamu ni ticket ya kushindwa!
 
nashangaa wanaomtupia lawama Nape na CCJ yake

ilihali kabla walikua na mpango wakwenda Chadema

uasi ni uasi tu, uwe wa siku nyingi ama usio dhahiri
 
iz it so..! cjui ni nin kilimfanya kikwete akawa maarufu sana 2005, ukiangalia kikubwa sana alichokua amefanya kwenye jamii huoni!!!! I'm so confused with this tz politics
 
Back
Top Bottom