Mundali
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 749
- 164
Ni takribani miaka mitano sasa tangu tumpate kiongozi mpya ndugu Jakaya Mrisho Kikwete. Katika mchakato waa uchaguzi mwaka 2005, alitoa ahadi kemkem kubwa ikiwa ni maisha bora kwa kila mtanzania. Nasikitika kwa sasa ahadi hiyo ni njozi iliyosahaulika. Watanzania napenda niwakumbushe mambo muhimu ambayo pengine wengi wetu tumesahau yaliyojiri katika utawala wake wa miaka mitano.
1. Akilihutubia bunge kwa mara ya kwanza, akiwa rais wa nchi alisema kwamba atapambana na rushwa bila kificho wala woga, na kwamba si lazima mtu akamatwe na rushwa bali tuhuma tu zingetosha kumuwajibisha.
2. Alitamka kwamba urais wake hauna ubia.
3. Aliwahi kutamka kwamba amepokea majina ya wauza madawa ya kulevya wakubwa, na dawa yao iko jikoni.
4. Pamoja na mambo mengi mazito aliyotamka hili sintolisahau. Akiwa katika mahojiano na radio Ufaransa aliulizwa swali, "kwamba Tanzania ni nchi iliyojaa rasilimali za aina nyingi na utajiri wa kupindukia, lakini kwa nini watanzania ni masikini?" Akajibu, "hata mimi sijui kwanini watanzania ni masikini".
Jibu lile limenifadhaisha mpaka leo hii. Hivi ni kweli rais wangu hajui ni kwanini mimi ni masikini?
Ni kwanini basi aliniomba kura aniongoze tuondoe umasikini? Je, mpaka leo hajui kwamba mimi ni masikini? Na kwanini anaomba kura za watu masikini ambao hajui sababu ya umasikini wao?
Hivi JK anaweza kweli kusimamia anachokiamini? Aweza kutenda anachosema?
Jamani watanzania wenzangu, na hususani wanaccm, jikomboeni katika utumwa wa kiakili, ukombozi wetu utaletwa na sisi wenyewe. Umasikini, ujinga na maradhi vitaondolewa na sisi wenyewe. Tuikomboe nchi yetu, kiokoeni chama chenu. Kiongozi wenu hajui tutokapo, tulipo na wala tuendapo. Kwa kiingereza hana Vision, Mission, Strategeis. Yupoyupo tu.
Kama aliletewa sheria ya gharama za uchaguzi akaisaini blindly, kisha kwenye kikao cha NEC akamuuliza Marmo, "hivi sheria hii ndiyo tuliyoipitisha?" Sitashangaa akiletewa mkataba wa kuuza sehemu ya nchi akausaini kwa sherehe kuubwa bila kujua kauza nchi.
Tusichague rais mbumbumbu!!!!!!!!!!!!!!!!!! Tutajutia uamuzi kwa kuchagua rais mbumbumbu.
1. Akilihutubia bunge kwa mara ya kwanza, akiwa rais wa nchi alisema kwamba atapambana na rushwa bila kificho wala woga, na kwamba si lazima mtu akamatwe na rushwa bali tuhuma tu zingetosha kumuwajibisha.
2. Alitamka kwamba urais wake hauna ubia.
3. Aliwahi kutamka kwamba amepokea majina ya wauza madawa ya kulevya wakubwa, na dawa yao iko jikoni.
4. Pamoja na mambo mengi mazito aliyotamka hili sintolisahau. Akiwa katika mahojiano na radio Ufaransa aliulizwa swali, "kwamba Tanzania ni nchi iliyojaa rasilimali za aina nyingi na utajiri wa kupindukia, lakini kwa nini watanzania ni masikini?" Akajibu, "hata mimi sijui kwanini watanzania ni masikini".
Jibu lile limenifadhaisha mpaka leo hii. Hivi ni kweli rais wangu hajui ni kwanini mimi ni masikini?
Ni kwanini basi aliniomba kura aniongoze tuondoe umasikini? Je, mpaka leo hajui kwamba mimi ni masikini? Na kwanini anaomba kura za watu masikini ambao hajui sababu ya umasikini wao?
Hivi JK anaweza kweli kusimamia anachokiamini? Aweza kutenda anachosema?
Jamani watanzania wenzangu, na hususani wanaccm, jikomboeni katika utumwa wa kiakili, ukombozi wetu utaletwa na sisi wenyewe. Umasikini, ujinga na maradhi vitaondolewa na sisi wenyewe. Tuikomboe nchi yetu, kiokoeni chama chenu. Kiongozi wenu hajui tutokapo, tulipo na wala tuendapo. Kwa kiingereza hana Vision, Mission, Strategeis. Yupoyupo tu.
Kama aliletewa sheria ya gharama za uchaguzi akaisaini blindly, kisha kwenye kikao cha NEC akamuuliza Marmo, "hivi sheria hii ndiyo tuliyoipitisha?" Sitashangaa akiletewa mkataba wa kuuza sehemu ya nchi akausaini kwa sherehe kuubwa bila kujua kauza nchi.
Tusichague rais mbumbumbu!!!!!!!!!!!!!!!!!! Tutajutia uamuzi kwa kuchagua rais mbumbumbu.