mnyikungu
JF-Expert Member
- Jul 26, 2009
- 1,960
- 2,464
Ukija Iringa msimu huu utaona wakandarasi walivyo tigwa,wanajenga na kukarabati barabara mno,na hili ndilo lililonosukuma kuandika post hii, kuna miradi mingi inayotekerezwa msimu huu hapa iringa.
Kuna miradi ya ukarabati wa barabara,kuna mradi mkubwa wa maji na pia upo mradi wa kupereka umeme vijiji,miradi ya barabara na maji nimeishuhudia na nimeridhika nayo jinsi inavyotekerezwa ila huo wa umeme vijijini bado sijauona.Pia mwaka huu raisi alikuja kupumzika Iringa tena nimedokezwa atakuja tena kwa ajiri ya kuifungua mbuga kubwa kuliko zote tanzania ya Ruaha.
Barabara ya kwenda dabaga imejengwa kwa kiwango cha rami japo siyo yote na barabara za mjini zinakarabatiwa pamoja kile kipande cha ipogoro ambacho ni gharama mno lakini kinatanuliwa na milima inatinduliwa kukiongezea upana achilia mbali barabarakuu inayofanyiwa ukarabati wa hali ya juu pamoja na kutanuliwa. Mradi wa maji ndio unaowafurahisha wakazi wengi wa mjini hapa kwa maana miundombinu inajengwa upya yaani wamefanya kama vile Iringa haijawahi kuwa na maji.
Mwanzo nilifikiri ni shukrani ya kikwete kwa wakazi wa iringa kwa maana ndio mkoa ulioongoza kwa kumpa kura mheshimiwa rais,lakini nikaanza kujiuliza mbona hii shukrani imechelewa kiasi hiki na inatolewa karibu na uchaguzi? Kwa nini isitolewe 2006 au 2007? Au alikuwa anajikusanya? Lakini nikaja kugundua kuwa kipindi hiki viongozi wengi wako kwenye mbio zao kuelekea uchaguzi basi nikahisi labda na mheshimiwa yuko kwenye mbio hizo
Kuna miradi ya ukarabati wa barabara,kuna mradi mkubwa wa maji na pia upo mradi wa kupereka umeme vijiji,miradi ya barabara na maji nimeishuhudia na nimeridhika nayo jinsi inavyotekerezwa ila huo wa umeme vijijini bado sijauona.Pia mwaka huu raisi alikuja kupumzika Iringa tena nimedokezwa atakuja tena kwa ajiri ya kuifungua mbuga kubwa kuliko zote tanzania ya Ruaha.
Barabara ya kwenda dabaga imejengwa kwa kiwango cha rami japo siyo yote na barabara za mjini zinakarabatiwa pamoja kile kipande cha ipogoro ambacho ni gharama mno lakini kinatanuliwa na milima inatinduliwa kukiongezea upana achilia mbali barabarakuu inayofanyiwa ukarabati wa hali ya juu pamoja na kutanuliwa. Mradi wa maji ndio unaowafurahisha wakazi wengi wa mjini hapa kwa maana miundombinu inajengwa upya yaani wamefanya kama vile Iringa haijawahi kuwa na maji.
Mwanzo nilifikiri ni shukrani ya kikwete kwa wakazi wa iringa kwa maana ndio mkoa ulioongoza kwa kumpa kura mheshimiwa rais,lakini nikaanza kujiuliza mbona hii shukrani imechelewa kiasi hiki na inatolewa karibu na uchaguzi? Kwa nini isitolewe 2006 au 2007? Au alikuwa anajikusanya? Lakini nikaja kugundua kuwa kipindi hiki viongozi wengi wako kwenye mbio zao kuelekea uchaguzi basi nikahisi labda na mheshimiwa yuko kwenye mbio hizo