Jitibu U.T.I kwa mmea huu kwa matokeo yenye ufanisi zaidi

digba sowey

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
7,894
14,353
Wakuu habari za leo ! Poleni na mihangaiko ya hapa na pale katika kutafuta riziki.

Nimekaa na kufikiri ni jinsi gani wazee wetu walikuwa wataalamu Wa tiba asilia lakini walikuwa wagumu sana kufundisha watu wakaribu yao, matokeo yake walikufa na maarifa yao, kwa Leo Mimi sitaki kufanana na hao wahenga.

Tangu nitambue kuwa huu mmea unatibu U.T.I, sasa Nina miaka miwili sijawahi tumia dawa za hospital, ninachokifanya Mimi ni kwenda kupima ili nijue nasumbuliwa na ugonjwa gani, baada ya hapo huwa narudi nyumbani na kuchuma majani haya , nayachemsha na kunywa. Hakika hii ni tiba nzuri sana wapendwa, kamwe hutakaa utake kutumia vidonge vya hospital kwa kutibu U.T.I., ufanisi wake ni zaidi ya % 80.

Matumizi yake ni kama ifuatavyo:

Chuma majani kati ya kumi hadi kumi na tano,baada ya hapo yasafishe kwa maji na kuyaweka katika chombo(sufuria) tia vikombe vya chai vitatu,na injika jikoni hadi yachemke(yatokote), hakikisha maji hayo baada ya kuchemka yanabaki vikombe vitatu, yakishachemka yaepue na toa majani yakae pembeni ili kubaki na kimiminika halisi,kunywa kikombe kimoja kutwa Mara tatu, hakikisha mchemsho unaoutengeneza ni Wa siku moja pekee, tumia dawa hii kwa muda Wa siku tatu hadi tano kwa matokeo yenye ufanisi.

NB. Jina la Mmea huu halijulikani,maana kwa utafiti wangu nimeuliza watu wengi lakini wanaishia kuniambia maua,lakini watu wengi hupenda kuutumia kama fensi/uzio.

IMG_20200502_074748_2.jpg
IMG_20200502_074748_2-1.jpg
 
Hii ni dawa safi sana,kwetu tunauita mkingili(ikingili) ukiacha magonjwa madogomadogo mengi ambayo mmea huu huweza kutibu kwa mafanikio makubwa nilipata jingine kwa rafiki yangu muhindi,yeye kwake ameyapanda kila sehemu kuzunguka ua wake.

Nikamuuliza kwa nini ameyaweka mengi kuliko maua mengine mazuri? Yeye akanijibu kuwa kwanza ni tiba ya magonjwa mbalimbali,lakini zaidi huwa anayatumia kiimani zaidi, anasema ukiwa na mimea hiyo nyumbani kwako basi watu wenye macho mabaya(ya husda) ambayo huleta madhara kwa watu na vitu hudhibitiwa barabara.

Anasema hata kama mchawi akija kwako kwa lengo baya basi mmea huu humfanya ashindwe kutimiza lengo lake,wachina pia wanauheshimu sana mmea huu kwa sababu kama hizo hizo, wao pia hudai kuwa mmea huu ukiupanda nyumbani huleta bahati njema, wahindi wa jamii ya ki hindu huchuma majani yake na kuyafunga pamoja na majani ya mwembe na kuyatundika mlangoni kama kinga dhidi ya wote wanaoingia ndani ya nyumba zao, hasa siku za sherehe au shughuli zinazokutanisha watu wengi,asante
 
Back
Top Bottom