Jitibu pumu kupitia tibambadala

BrotherAbdul

Member
Apr 21, 2017
9
26
) KUPITIA TIBAMBADALA
Pumu au asthma ni katika magonjwa hatari ambayo tiba sahihi kwa wengi imekuwa ni kitendawili, lakini lishe mbadala ni jibu lake, kutokana na tafiti za wataalamu na wadau mbalimbali, tafiti ambazo natija yake ni kupatikana kwa dawa muafaka za ugonjwa huu kupitia vyakula asilia Tumia vitu vifuatavyo kujitibu pumu kupitia tiba mbadala; 1.karafuu,unaweza kuchukua karafuu 5-6,chemsha karafuu ili kupata ujazo wa nusu glasi, kisha ongeza kijiko kikubwa cha asali mbichi, unaweza kunywa asubuhi na wakati wa Kuala. 2.juisi ya limau, tengeneza juisi ya limau, kwa kuchanganya na asali kijiko na mdalasini wa unga, tumia juisi hii murua asubuhi kabla ya mlo na kabla ya Kuala. 3.asali mbichi, na nivema ukachanganya na mdalasini wa unga, na mafuta ya mzaituni kidogo, tumia mchanganyo huu kijiko kimoja mpaka viwili, asubuhi na jioni. 4.kitunguu swaumu (garlic) chukua angalau tembe tano, maji robo lita pamoja na asali mbichi kijiko kikubwa na mdalasini wa unga kijiko. Chemsha pamoja 5.tangawizi,unaweza kuchemsha tangawizi ujazo wa robo lita, weka na kijiko kikubwa cha asali na mafuta ya. Mzaituni kijiko kidogo. 6.kitunguu maji, jitahidi kutumia kitunguu maji kwenye mboga au kachumbali. 7.maziwa,chemsha maziwa ukichanganya na asali kijiko kikubwa na mafuta ya mzaituni kijiko kwakikombe cha maziwa, kunywa yakiwa na moto. 8.binzari ,tumia kiungo hiki kwa wingi (turmeric) katika chakula chako 9.mafuta ya nazi, unaweza kunywa kijiko, au kupikia katika vyakula, kwa sababu kitaalamu mafuta ya nazi yana palmitic acid ambayo humsaidia sana mgonjwa pumu. Pia mgonjwa anashauriwa kula kwa wingi vyakula vifuatavyo : Karoti Mbegu za maboga ,korosho, karanga Vyakula vyenye vitamini C kwa wingi kama matunda Vitu vyenye magniziam kwa wingi kama vitunguu swaumu Maziwa mabichi Mbogamboga kwa wingi Unashauruwa kula nyama nyeupe kama samaki








Aprili 17, 2017

MAUMUIVU YA CHINI YA KITOVU KWA WANAWAKE
 
Shukrani mkuu kwa darsa murua.
Nilipokua mdogo nilisumbuliwa sana na asthma, ilisababisha hata utoto wangu nisiu-enjoy vizuri kwa michezo mbalimbali hasahasa mpira na michezo ya kukimbizana. Nilihangaika sana na dawa za hospitali na kuna kipindi niliwahi kutumia hadi zile "inhalers".

Nilipofika darasa la 5 mzee wangu alipata bahati akakutana na mama mmoja hivi mmasai akaamua kunisaidia baada ya mzee kumsimulia tabu anayoipata kwa kunitibia.

Nilitumia asali, nilichanganya na unga fulani hivi (sikuwahi kujua unaitwaje) ila ulikua ni mchungu sana, pia kulikuwa na dawa nyingine ya kuweka kwenye chai ila ilikuwa inaniwasha sana kwenye koo, na pia kuna moja nilikuwa naitumia kwenye maji yenye mvuke na kuipitishia puani.

Mungu si athumani, hata sikumbuki nilipona lini ila mpaka nilipofika darasa la 6 nikajikuta naanza kucheza mpira, naoga maji ya baridi (wakati huo nilikuwa nikiishi mbeya na baridi ya kule si mchezo), natumia perfumes & sprays hadi leo hii na kufanya vitu vyote ambavyo sikuvitumia hapo kabla.
 
Pamoja
Shukrani mkuu kwa darsa murua.
Nilipokua mdogo nilisumbuliwa sana na asthma, ilisababisha hata utoto wangu nisiu-enjoy vizuri kwa michezo mbalimbali hasahasa mpira na michezo ya kukimbizana. Nilihangaika sana na dawa za hospitali na kuna kipindi niliwahi kutumia hadi zile "inhalers".

Nilipofika darasa la 5 mzee wangu alipata bahati akakutana na mama mmoja hivi mmasai akaamua kunisaidia baada ya mzee kumsimulia tabu anayoipata kwa kunitibia.

Nilitumia asali, nilichanganya na unga fulani hivi (sikuwahi kujua unaitwaje) ila ulikua ni mchungu sana, pia kulikuwa na dawa nyingine ya kuweka kwenye chai ila ilikuwa inaniwasha sana kwenye koo, na pia kuna moja nilikuwa naitumia kwenye maji yenye mvuke na kuipitishia puani.

Mungu si athumani, hata sikumbuki nilipona lini ila mpaka nilipofika darasa la 6 nikajikuta naanza kucheza mpira, naoga maji ya baridi (wakati huo nilikuwa nikiishi mbeya na baridi ya kule si mchezo), natumia perfumes & sprays hadi leo hii na kufanya vitu vyote ambavyo sikuvitumia hapo kabla.[/Q
Shukrani mkuu kwa darsa murua.
Nilipokua mdogo nilisumbuliwa sana na asthma, ilisababisha hata utoto wangu nisiu-enjoy vizuri kwa michezo mbalimbali hasahasa mpira na michezo ya kukimbizana. Nilihangaika sana na dawa za hospitali na kuna kipindi niliwahi kutumia hadi zile "inhalers".

Nilipofika darasa la 5 mzee wangu alipata bahati akakutana na mama mmoja hivi mmasai akaamua kunisaidia baada ya mzee kumsimulia tabu anayoipata kwa kunitibia.

Nilitumia asali, nilichanganya na unga fulani hivi (sikuwahi kujua unaitwaje) ila ulikua ni mchungu sana, pia kulikuwa na dawa nyingine ya kuweka kwenye chai ila ilikuwa inaniwasha sana kwenye koo, na pia kuna moja nilikuwa naitumia kwenye maji yenye mvuke na kuipitishia puani.

Mungu si athumani, hata sikumbuki nilipona lini ila mpaka nilipofika darasa la 6 nikajikuta naanza kucheza mpira, naoga maji ya baridi (wakati huo nilikuwa nikiishi mbeya na baridi ya kule si mchezo), natumia perfumes & sprays hadi leo hii na kufanya vitu vyote ambavyo sikuvitumia hapo kabla.
Pamoja waƙuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom