Leo hii tujifunze jinsi ya kupika tambi za mapapayu,usishangae ni katika ubunifu wa mapishi MAHITAJI
Tambi za mapapayu (papayu lilokatwa maganda na kukatwa kwa urefu kama tambi) kiasi bakuli moja la kiasi
Tui zito kikombe 1
Tui jepesi kikombe 1&1/2
Sukari kikombe 1
Iliki kiasi
MATAYARISHO
Weka tambi kwenye sufuria na maji kiasi cha kufunika tambi, zifunike na uziache zichemke mpaka ziive(zibonyeze na ukiziona ziko laini basi zimeiva) Tambi nyingine ni cherema na huenda zikachukua muda mrefu zaidi kuiva
Kisha mwaga maji ya ziada
Weka sukari, tui jepesi na iliki kwenye zile tambi ulizozimwaga maji na urejeshe motoni kwa takriban dakika 10
Kisha weka tui zito na uziache motoni kwa takriban dakika 5
Baada ya hapo tambi zipo tayari ipua anda mezani na chai ya maziwa.
"Nina mpango wa kufungua Mkahawa kwaiyo najiwekea kumbukumbu hapa na kufanya practice nyumbani"
Weka tambi kwenye sufuria na maji kiasi cha kufunika tambi, zifunike na uziache zichemke mpaka ziive(zibonyeze na ukiziona ziko laini basi zimeiva) Tambi nyingine ni cherema na huenda zikachukua muda mrefu zaidi kuiva