Jinsi ya kumuua Mama-Mkwe

Jinsi ya kumuua Mama-Mkwe

Jambazi

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
16,654
Reaction score
18,792
Miaka kadhaa huko Uchina, Binti aitwaye Li- Li aliolewa na akaenda kuishi kwao mumewe na mama wa mumewe.Ndani ya muda mfupi Li-Li alijikuta hana maelewano kabisa na mama Mkwe wake.

Tabia zao zilikuwa tofauti kabisa, walipishana kauli kila mara na Li-Li alichukizwa sana na tabia nyingi za mama mkwe wake. Mbaya zaidi, mama-mkwe alimlaumu na kumsema vibaya Li-Li mara zote.

Kadri ya siku na wiki zilivyopita, Li-Li na mamamkwe wake walizidi kubishana na kugombana. Kilichofanya hali kuwa ngumu sana ni mila kuwa Li-Li alitakiwa kumnyenyekea na kutimiza kila alichohitaji.Ugomvi na kukosekana amani ndani ya nyumba vilimsababishia mfadhaiko na kumyima amani mume wa Li-Li kwani aliwapenda wrote.

Baada ya kushindwa kumvumilia mama Mkwe wake ambaye alinung'unika kila mara na kutaka kuwa ndiye anayefanya maamuzi yote ndani ya nyumba, Li-Li aliamua kwenda kwa rafiki wa baba yake,Huang, ambaye alikuwa anauza Dawa za mitishamba.

Itaendelea.....
 
khaa sasa hii hadithi simulizi habar au mbwaii
 
mxa...kumbe stori...nilifikiri umefanya kweli
 
alafu we jamaa utakuwa una matatizo ya problem na magonjwa ya desease yanayoambukizwa kwa njia ya infection nenda garage ukapime afya mkuu
 
Back
Top Bottom