tulikua watu zaidi ya hamsini yaani ukiwa ndani ya chombo maji unaweza ukayashika hivi halafu goma limeinuka kwa mbele utashangaa wimbi hilo linakuja mwongozaji anavyolikwepa sasa kama linazama hivi tukafika mahari watu wakapungua tukaambiwa turudi nyuma ili injini iguse maji sasa mbele kuko juu huku nyuma kupo chini katika masaa nane sikusinzia hata dakika moja ni hofu tu wenyewe wanapiga stori hawana hata wasiwasi nikajisemea bora ningezunguka kwa gari
Hahahahaaaaa! Yalinikuta hayonilipotembelea watu wangu kijiji fulani when I finished my exam (A level)
Nilipenda siku moja niwafate kuvua coz kuna madogo tu walikua wanakwenda, nakumbuka wazee walinisisistiza nisiende coz wimbi kali na kutapika ningerudi mgonjwa. Nilipenda kuona namna watu wanavyovua huku nikijisemea nitajifunza mengi.
Siku nikakomaa nakuwafata.
Mwanzoni safari ilikua tamuu, coz tulikua ktk mto (pwani) = tulikua tunapita pwani/mto ulioga vitongoji viwili. wataki tunaingia baharini ndio kasheshe! coz mbele yetu kulikua na kisiwa, mean mbele kutakua na sehemu mbili za kuingia bahari kuu (wanaita milango) Dah aliekufa Mungu amrehemu! Mawimbi ya bahari kuu yanapiga kwa kasi milangoni.
Kabla ya kuvuka hapo, nilijua ni kazi nyepesi sana kuvuka kwani nilipoona weupe kwa mbali nilijua ni vijiwimbi vidogo vidogo tu!!! Kuyakaribia nilistka sana na kujisemea pale tunazama, kudadadeki wimbi linakingoe nasi ndio tunatakiwa kuyafesi kwa mbele, coz ukiyapa ubavu chonbo kinapinduliwa! niliamua kutoangalia mbele thus nikagekia tulipotoka, ile tunaanza kuyakata, maji yameshaanza kuingia kwenye chombo! Nikapewa kazi ya kutoa maji, yule mmoja kasimama kwenye behewa kukibalance chombo kutokana na mawimbi na upepo na mwengine alikua ndie dereva anadeal na usukani wake (tanga). Tulikua watatu.
Wakati natoa maji nilijaribu kuangalia mbele, hapo ndipo nilipobugi! coz ilikua ni kati kati ya mlango kuingia main sea. ile nageuka tu wimbi kubwa inakuja na ilikua na kimo cha mtu mzima kabisa! wakati naishangaa ndio inatpita sasa!! kudadadeki kidoo kilitupwa kule, tuliloa hadi nywele! nilishikwa na mfadhaiko na kujua leo kifo tu. Kwa bahati vidoo vilikua viwili nilikaripiwa kutoshangaa na niendelee kutoa maji. kile kidoo kilichoondoka na maji nikaambiwa hakiwezi fatwa coz chombo hakitakiwi kugeuza mbavu pale.
Tuliingia bahari kuu ambapo hakuna mawimbi ya kutembea ila ni maji kujifinya kwa chini na kurudi juu mwanzo mwisho, yaani kama upo kwenye bembea vile!!! na hali hiyo ndio huwafanya wengi kutapika (wageni)
Nashukuru tulirudi salama. Ila sitakaa niisahau kamwe siku hiyo.