Jinsi ya kuendesha Ngalawa

Jinsi ya kuendesha Ngalawa

kwangu na kwako ila kwao ni salama tu



kuogelea naogeleaga coco ila kinachowaua watu baharini sio kutojua kuogelea bali kuchoka na baridi

si unaogelea uku umevaa jaketi la baridi kabisa
 
tulikua watu zaidi ya hamsini yaani ukiwa ndani ya chombo maji unaweza ukayashika hivi halafu goma limeinuka kwa mbele utashangaa wimbi hilo linakuja mwongozaji anavyolikwepa sasa kama linazama hivi tukafika mahari watu wakapungua tukaambiwa turudi nyuma ili injini iguse maji sasa mbele kuko juu huku nyuma kupo chini katika masaa nane sikusinzia hata dakika moja ni hofu tu wenyewe wanapiga stori hawana hata wasiwasi nikajisemea bora ningezunguka kwa gari

Hahahahaaaaa! Yalinikuta hayonilipotembelea watu wangu kijiji fulani when I finished my exam (A level)

Nilipenda siku moja niwafate kuvua coz kuna madogo tu walikua wanakwenda, nakumbuka wazee walinisisistiza nisiende coz wimbi kali na kutapika ningerudi mgonjwa. Nilipenda kuona namna watu wanavyovua huku nikijisemea nitajifunza mengi.

Siku nikakomaa nakuwafata.
Mwanzoni safari ilikua tamuu, coz tulikua ktk mto (pwani) = tulikua tunapita pwani/mto ulioga vitongoji viwili. wataki tunaingia baharini ndio kasheshe! coz mbele yetu kulikua na kisiwa, mean mbele kutakua na sehemu mbili za kuingia bahari kuu (wanaita milango) Dah aliekufa Mungu amrehemu! Mawimbi ya bahari kuu yanapiga kwa kasi milangoni.

Kabla ya kuvuka hapo, nilijua ni kazi nyepesi sana kuvuka kwani nilipoona weupe kwa mbali nilijua ni vijiwimbi vidogo vidogo tu!!! Kuyakaribia nilistka sana na kujisemea pale tunazama, kudadadeki wimbi linakingoe nasi ndio tunatakiwa kuyafesi kwa mbele, coz ukiyapa ubavu chonbo kinapinduliwa! niliamua kutoangalia mbele thus nikagekia tulipotoka, ile tunaanza kuyakata, maji yameshaanza kuingia kwenye chombo! Nikapewa kazi ya kutoa maji, yule mmoja kasimama kwenye behewa kukibalance chombo kutokana na mawimbi na upepo na mwengine alikua ndie dereva anadeal na usukani wake (tanga). Tulikua watatu.

Wakati natoa maji nilijaribu kuangalia mbele, hapo ndipo nilipobugi! coz ilikua ni kati kati ya mlango kuingia main sea. ile nageuka tu wimbi kubwa inakuja na ilikua na kimo cha mtu mzima kabisa! wakati naishangaa ndio inatpita sasa!! kudadadeki kidoo kilitupwa kule, tuliloa hadi nywele! nilishikwa na mfadhaiko na kujua leo kifo tu. Kwa bahati vidoo vilikua viwili nilikaripiwa kutoshangaa na niendelee kutoa maji. kile kidoo kilichoondoka na maji nikaambiwa hakiwezi fatwa coz chombo hakitakiwi kugeuza mbavu pale.

Tuliingia bahari kuu ambapo hakuna mawimbi ya kutembea ila ni maji kujifinya kwa chini na kurudi juu mwanzo mwisho, yaani kama upo kwenye bembea vile!!! na hali hiyo ndio huwafanya wengi kutapika (wageni)

Nashukuru tulirudi salama. Ila sitakaa niisahau kamwe siku hiyo.
 
Nawaonaga pale ferry wana endesha na mwiko, dereva anaendesha utadhani anasonga ugali. Mwambie kama anajua kusonga ugali anaweza akaendesha hicho kiboti ngalawa.
 
Nawaonaga pale ferry wana endesha na mwiko, dereva anaendesha utadhani anasonga ugali. Mwambie kama anajua kusonga ugali anaweza akaendesha hicho kiboti ngalawa.

daaaaaa! nimecheka hatari so ukijua kusonga ugali basi unaendesha dah! kwa hiyo mamantilie wasonga ugali wanaweza sio
 
Khaa! Kuogelea anajua? Maana kile kidude kupinduka ni dakika sifuri tu (baharini) na baada ya kupinduka kinahitaji ujuzi kukiokoa na kukipanda tena ili urudi. sasa huyo mdau wako sijui kama ataweza kukigeuza coz kikipunduka kinakua upside down, then kunashuhuli ya kukimwaga maji humo humo baharini then ukipande uendelee na shughuli or urudi nacho kwenu.

Anyway hilo ni angalizo tu (la muhimu)

Namna ya kukiendesha:
Ajifunze kukontroo tanga, ikiwa kinatumia tanga, tanga ni kama sukani. linahitaji ujuzi wa hali ya juu kilishusha, kilipandisha na kuliendesha. Ajue kusoma upepo.

Ikiwa ni la mashine ajifunze hata ujuzi wa mashine coz mashine likimgomea ajue kulibust, na lile mashine kugoma ni takika sifuri tu.

Ikiwa ni la kafi ajue kutumia kafi. ile ni skani yake.

General concepts.

Dereva anakaa nyuma kabisa ya ngalawa.

Ngalawa inaendeshwa kinyume nyume: akitaka kupinda kulia asukume kafi/mashine upande wa kushoto, na akitaka kupinda kushoto asukumie kulia. akitaka kunyoosha apige kafi kulia na kushoto. ikiwa ni ya mashine ni kuinyoosha tu.

Ni lazima ajifunze unahodha, hasa kwa vitendo, ili ajue kusoma upepo, mwelekeo wa maji, wimbi na hali ya hewa, asome na namna ya kukabiliana na hivyo.

NB: Usimshauri kuingia kwenye maji na chombo kabla ya mafunzo. ni hatari sana.

Mashaxizoumetisha
 
Last edited by a moderator:
Hii kitu sitaki hata kuisikia! kwenda kutongoza samaki! yalinikuta miaka ya 80hapana hicho chombo mpaka ujifyatue akili kidogo ndo ukipande oh hapana! unaliona wimbi kubwa kama ppf tower kisha linawapiga mnaenda juu nikajua leo sijui but kwa kudra ya mwenyezimungu tulifika ila jasho lilinitoka.
 
Hahahahaaaaa! Yalinikuta hayonilipotembelea watu wangu kijiji fulani when I finished my exam (A level)

Nilipenda siku moja niwafate kuvua coz kuna madogo tu walikua wanakwenda, nakumbuka wazee walinisisistiza nisiende coz wimbi kali na kutapika ningerudi mgonjwa. Nilipenda kuona namna watu wanavyovua huku nikijisemea nitajifunza mengi.

Siku nikakomaa nakuwafata.
Mwanzoni safari ilikua tamuu, coz tulikua ktk mto (pwani) = tulikua tunapita pwani/mto ulioga vitongoji viwili. wataki tunaingia baharini ndio kasheshe! coz mbele yetu kulikua na kisiwa, mean mbele kutakua na sehemu mbili za kuingia bahari kuu (wanaita milango) Dah aliekufa Mungu amrehemu! Mawimbi ya bahari kuu yanapiga kwa kasi milangoni.

Kabla ya kuvuka hapo, nilijua ni kazi nyepesi sana kuvuka kwani nilipoona weupe kwa mbali nilijua ni vijiwimbi vidogo vidogo tu!!! Kuyakaribia nilistka sana na kujisemea pale tunazama, kudadadeki wimbi linakingoe nasi ndio tunatakiwa kuyafesi kwa mbele, coz ukiyapa ubavu chonbo kinapinduliwa! niliamua kutoangalia mbele thus nikagekia tulipotoka, ile tunaanza kuyakata, maji yameshaanza kuingia kwenye chombo! Nikapewa kazi ya kutoa maji, yule mmoja kasimama kwenye behewa kukibalance chombo kutokana na mawimbi na upepo na mwengine alikua ndie dereva anadeal na usukani wake (tanga). Tulikua watatu.

Wakati natoa maji nilijaribu kuangalia mbele, hapo ndipo nilipobugi! coz ilikua ni kati kati ya mlango kuingia main sea. ile nageuka tu wimbi kubwa inakuja na ilikua na kimo cha mtu mzima kabisa! wakati naishangaa ndio inatpita sasa!! kudadadeki kidoo kilitupwa kule, tuliloa hadi nywele! nilishikwa na mfadhaiko na kujua leo kifo tu. Kwa bahati vidoo vilikua viwili nilikaripiwa kutoshangaa na niendelee kutoa maji. kile kidoo kilichoondoka na maji nikaambiwa hakiwezi fatwa coz chombo hakitakiwi kugeuza mbavu pale.

Tuliingia bahari kuu ambapo hakuna mawimbi ya kutembea ila ni maji kujifinya kwa chini na kurudi juu mwanzo mwisho, yaani kama upo kwenye bembea vile!!! na hali hiyo ndio huwafanya wengi kutapika (wageni)

Nashukuru tulirudi salama. Ila sitakaa niisahau kamwe siku hiyo.

Kiongozi, simulizi nzuri sana, asante ku share nasi!!!
 
unaogopa sana, wenyewe wanaiamini ngalawa kuliko hata meli, na wana sababu zao
1 ngalawa haizami, ikizama waibirua na kufata maji
2 ngalawa una uwezo wa kufunga breki na ukasimama hapo hapo
3 kama utakuwepo upepo, basi ngalawa ina spidi kuliko boti
twayyib!! Akhii hivi ni wapi wanatoa kozi ya kuendesha boti Ndogo (out engines)? kwa dar es salaam au zinjibar?
 
Back
Top Bottom