Khaa! Kuogelea anajua? Maana kile kidude kupinduka ni dakika sifuri tu (baharini) na baada ya kupinduka kinahitaji ujuzi kukiokoa na kukipanda tena ili urudi. sasa huyo mdau wako sijui kama ataweza kukigeuza coz kikipunduka kinakua upside down, then kunashuhuli ya kukimwaga maji humo humo baharini then ukipande uendelee na shughuli or urudi nacho kwenu.
Anyway hilo ni angalizo tu (la muhimu)
Namna ya kukiendesha:
Ajifunze kukontroo tanga, ikiwa kinatumia tanga, tanga ni kama sukani. linahitaji ujuzi wa hali ya juu kilishusha, kilipandisha na kuliendesha. Ajue kusoma upepo.
Ikiwa ni la mashine ajifunze hata ujuzi wa mashine coz mashine likimgomea ajue kulibust, na lile mashine kugoma ni takika sifuri tu.
Ikiwa ni la kafi ajue kutumia kafi. ile ni skani yake.
General concepts.
Dereva anakaa nyuma kabisa ya ngalawa.
Ngalawa inaendeshwa kinyume nyume: akitaka kupinda kulia asukume kafi/mashine upande wa kushoto, na akitaka kupinda kushoto asukumie kulia. akitaka kunyoosha apige kafi kulia na kushoto. ikiwa ni ya mashine ni kuinyoosha tu.
Ni lazima ajifunze unahodha, hasa kwa vitendo, ili ajue kusoma upepo, mwelekeo wa maji, wimbi na hali ya hewa, asome na namna ya kukabiliana na hivyo.
NB: Usimshauri kuingia kwenye maji na chombo kabla ya mafunzo. ni hatari sana.