Jinsi wanawake walivyo wavumilivu

Jinsi wanawake walivyo wavumilivu

babayao255

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2019
Posts
12,901
Reaction score
34,897
1.ANAKUFUMANIA: Analia,
ananyamaza, anasononeka, unambembeleza
anakuelewa anakusamehe halafu anasahau!!!
2. UNAZAA NJE YA NDOA:
Anasononeka na kulia sana . Anakuchukia, lakini baadaye anakusamehe.Halafu analea mtoto uliyemzaa nje kwa upendo.
Kama ni kuchukiwa atachukiwa mtoto, si wewe uliyefanya umalaya!
3.UNARUDI USIKU WA MANANE UKIWA MTUNGI:
Anakukaribisha, anakuandalia chakula,
unagoma kula. Anahifadhi chakula alichokuandalia bila manung'uniko.
4.UNAAMKA ASUBUHI NA MAHANGOVER:
Anakuandalia staftahi (saa nyingine unagoma
kutumia staftahi yake unakimbilia baa kwenda kunywa Supu na kuzimua. Wala
halalamiki!
5.CHAKULA CHA USIKU:
Ushapiga mtungi wako, unataka huduma.
Unamrukia, hamna maandalizi unamuumiza.
Anavumilia ili akuridhishe.
Na kesho yake tena inaweza tokea hii; hana
kinyongo!
6.UNAJIANDAA KWENDA KIBARUANI: Unakuta kashakuandalia viwalo, suruwale imenyooshwa kama ya askari trafiki, shati
limepigwa pasi ya maana! Nguo ulizovua jana
zimeshalowekwa tayari kwa kufanyiwa usafi! Ulichomuudhi jana kashasahau na
kukusamehe!
7. UNAMPA UJAUZITO:
Anauthamini, anautunza anajifungua kwa uchungu, mtoto anakuachia wewe umpe jina, la kwake halimo kabisa kwenye majina atakayotumia mtoto! Na pamoja na uchungu wa kuzaa, bado yuko radhi kukuzalia mtoto mwingine na mwingine tena! Na mengine meeeeengi sana wanafanyiwa hawa watu lakini WANASAMEHE, WANAVUMILIA! Ni watu muhimu sana hawa watu maishani mwetu.
 
Siyo uvumilivu, wanawake ni wajasili pia. Imagine, mtu hamjui lakini anampiga sound hadi mwanamke anamkubalia kwenda naye nyumbani kwake bila wasiwasi kumpa mzigo. Hawaogopi kabisa, strangers.
 
Tunajua ndivyo walivyo,ndio maana tunawaoa kwa sababu wao ni wanawake,wameumbwa kuwa hivyo,au ulikuwa kuna lingine ulitaka kuongezea...?
 
Wanawake wa hivyo wameisha Mkuu, siku hizi ukitoka nae anatoka, jioni anakupigia simu "baby kula chips huko huko, huku leo nimepaka kucha rangi sikupika" Ahhhhhh…. hatari asee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom