Jinsi Rais Magufuli anavyowakandamiza wanyonge

Hata mghani mashairi ya namna gani, sisi watanzania tunamuunga mkono Mheshimiwa rais Magufuli na serikali yake. Unapofanya mabadiliko makubwa ya kimfumo katika nchi ni lazima ukubali kuumia kidogo. Kwa mtu mwenye akili timamu hawezi akafikiri kufanya mabadiliko bila kupata maumivu. Nitoe mfano kidogo, wewe una nyumba ya kuishi ambayo imechakaa na inahitaji ukarabati mkubwa. Bila shaka huwezi kuepuka usumbufu wakati unapofanya ukarabati kwa sababu muda mwingine utalazimika kupanga nyumba kwa muda ili kupisha ukarabati huo. Kwa maana hiyo, kinachoendelea kwa sasa katika nchi yetu ni marekebisho makubwa ya kimfumo katika nchi yanayofanywa na MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI. Adha ndogo ndogo tunazoziona kwa sasa ni za muda mfupi tu hivyo tusiwahadae wananchi kuwa Mheshimiwa rais Magufuli ni dictator. Tutumie muda mwingi kuwahamasisha wananchi kufanya Kazi kwa bidii ili kujiongezea kipato chao. Ndani ya kipindi kifupi maisha ya watanzania yatakuwa ni mazuri sana.
acha hadithi zako za alfu lela ulela.....kuvunja sheria kwa kuwazuia watumishi wa umma kupandishwa vyeo na kunyimwa maslahi yao hakuna manufaa yoyote kwa wafanyakazi wanyonge wanaolipwa mishahara uchwara. kumbuka kwamba kama ilikuwa mtumishi apande cheo mwezi wa tano mwaka huu na bado hajapanda hawezi kupanda tena hadi dr makufuri atakapotaka na elewa kuwa sasa hivi hakuna kupanda cheo kwa kuserereka....hata ikipita miaka 10 hujapandishwa cheo, utakuja kupanda cheo mara moja tu.....wewe huoni kwamba hii ni dhuluma dhidi ya wanyonge?
 
mkuu, tunapishana padogo sana. mimi sijakataa kodi isilipwe...hebu nisome upya. ninachokataa ni kodi isiyokuwa na uwiano.....wanyonge wanakamuliwa hadi damu wakati sekta zingine zinaachwa. kwa mfano, nchini tanzania serikali inachukua 3% kutoka kwenye madini na kuwaachia wazungu 97%......nchini Botswana serikali inachukua 60% na mwekezaji anachukua 40% kutoka kwenye madini yale yale yanayochimbwa tanzania. umeona tofauti? kumbe serikali ikichukua hata 5% kutoka kwenye madini, hakutakuwa na haja ya kuwakamua masikini. aidha serikali bado haijachukua kodi ya kutosha kutoka kwenye utalii....wawindaji wa kizungu hupewa vitalu kwa bei chee na badala ya kuwinda hukamata wanyama na kuwasafirisha kwenda nje (rejea usafirishaji wa twiga na wanyama hai wengine). mwisho wa siku tutakosa watalii baada ya wanyama wote kusombwa kutoka mbugani na kusafirishwa uzunguni. serikali ikitia mkazo kidogo kwenye makusanyo ya utalii, hakuna haja ya kuwaumiza wanyonge na makodi ya ajabuajabu. vilevile wafanyabiashara wakubwa na wenye viwanda bado hawajalipishwa kodi sawa sawa....kama hili suala likifanyiwa kazi vizuri, hakuna haja ya kuendelea kuwakamua wanyonge. hii ndio hoja yangu. umeelewa?
Hawawezi kukuelewa mzee !! Huko kazi ni kusifu na kuabudu
 
mkuu, tunapishana padogo sana. mimi sijakataa kodi isilipwe...hebu nisome upya. ninachokataa ni kodi isiyokuwa na uwiano.....wanyonge wanakamuliwa hadi damu wakati sekta zingine zinaachwa. kwa mfano, nchini tanzania serikali inachukua 3% kutoka kwenye madini na kuwaachia wazungu 97%......nchini Botswana serikali inachukua 60% na mwekezaji anachukua 40% kutoka kwenye madini yale yale yanayochimbwa tanzania. umeona tofauti? kumbe serikali ikichukua hata 5% kutoka kwenye madini, hakutakuwa na haja ya kuwakamua masikini. aidha serikali bado haijachukua kodi ya kutosha kutoka kwenye utalii....wawindaji wa kizungu hupewa vitalu kwa bei chee na badala ya kuwinda hukamata wanyama na kuwasafirisha kwenda nje (rejea usafirishaji wa twiga na wanyama hai wengine). mwisho wa siku tutakosa watalii baada ya wanyama wote kusombwa kutoka mbugani na kusafirishwa uzunguni. serikali ikitia mkazo kidogo kwenye makusanyo ya utalii, hakuna haja ya kuwaumiza wanyonge na makodi ya ajabuajabu. vilevile wafanyabiashara wakubwa na wenye viwanda bado hawajalipishwa kodi sawa sawa....kama hili suala likifanyiwa kazi vizuri, hakuna haja ya kuendelea kuwakamua wanyonge. hii ndio hoja yangu. umeelewa?
NASADIFU ULICHOSEMA,UKO SAWA MKUU,HAPO KUNA HAJA YA SERIKALI KUPATOLEA MACHO KULIKO KUMKAMUA MTU WA MWISHO AMBAYE NI MASIKINI
 
Kwani ile chorus maridadi ya mtaisoma namba inamaana gani zaidi ya hiyo!?!?
Lazima watu walimie meno ili kieleweke.
 
Nilisema kitambo hapa Magufuli ni dikteta, watu wakaona kama natia chumvi gumzo.

Sasa wengi wanaona hili.
Watanzania ni watu wa kujifunza in "the hard way", acha tuisome namba. Pia katika vipaji ambavyo watanzania walinyimwa na Mungu ni mambo ya forecasting,,, mara nyingi mtu akiforecast anaonekana kama Prof Maji Marefu hakuna anayemtilia umuhimu
 
Jamani huyu Magufuli ana miez saba tangu awe Raisi. Embu tumstahi hadi tarehe 05 / 11 /2017 ambapo atakuwa ametimiza miaka miwili ktk utawala wake. Baada ya hapo tunaweza kusema mazuri na mabaya yake!!! Saivi Magufuli anaonekana yupo kwenye RECONSRUCTION period. Yaani kipindi cha UJENZI baada kubaini sera za Mtangulizi wake yaani JK hazikuwa nzuri japo zilitufaa na kutuvusha salama kipindi hicho!! Ndyo maana malalamiko meeengi, ni kutokana na mabadiliko hayo. TUMVUMILIE had November mwakani.
 
mkuu inawezekana ama uelewa wako ni mdogo au umeamua kujitoa ufahamu kwa makusudi. hakuna mtu anayekataa juhudi za dr makufuri kuirudisha nchi kwenye mstari. tunachokikataa ni tabia yake ya kuwakamua masikini huku akiacha sekta zingine kama vile madini (kwenye madini, wazungu wanachukua 97% makufuri anaambulia makombo ya 3%), utalii, wafanyabishara wakubwa (makanjibai, etc), bandari, misitu, uwekezaji, etc. umeelewa sasa?

wakati huo huo kumbuka maumivu yanayotokana na maamuzi yake ya kuwakamua masikini tayari yameanza.....tembelea wakala yeyote wa mpesa, tigo pesa, airtel money au z-money uone viwango vipya vya kutuma na kutoa pesa....haya yote yanatokana na maamuzi HASI yanayolenga kuwakamua wanyonge...punde si punde mabenki na wababa wenye nyumba nao watapandisha gharama kwa wanyonge. huu ukamuaji ina maana haukuhusu wewe au ukoo wako? kama wewe labda upo ughaibuni ukichakarika na box, je huwaonei huruma ndugu zako uliowaacha nyumbani?
Tujifunze kulipa kodi. Watu walipe kodi.
Huna unachojua kuhusu hiyo asilimia 4 kwa sasa ya kwenye madini ni nini. Tamko limekwisha toka la kuangalia migodi inayotangaza hasara.
 
Kazi siyo lazima kushika jembe au kubeba zege. Kuna biashara kwa njia ya mtandao pia
 
Mnaodhani kuwa Dr Magufuli ni mtetezi wa wanyonge (kama anvyojinukuuu mara kwa mara) mnapaswa kutafakari upya. Tangu Dr Magufuli alipoingia madarakani amefanikiwa kukanyaga haki mbalimbali za raia pamoja na kufanya maisha ya mamilioni ya watanzania wa kawaida yawe magumu zaidi kuliko ilivyokuwa katika utawala wa Dr JK.

Kuna baadhi ya maamuzi ya kikandamizaji ninayoweza kuyakumbuka ambayo madhara yake yamewaumiza wananchi huku wanafiki na wachochezi wachache wakichekelea wakati wanajua haki za msingi za wananchi zimekanyagwa:

KUINGILIA MFUMO WA BIASHARA HURIA

Ni dhahiri mfumo wa uchumi wa sasa ni wa BIASHARA HURIA – kwamba upatikanaji wa bidhaa (supply) na na mahitaji (demand) ndio huamua bei (price). Kazi ya serikali sio kufanya biashara ila kazi yake ni kurahisisha mazingira ya biashara na kukusanya kodi.

Lakini tumeshuhudia Dr Magufuli akizuia uagizaji wa sukari (intentional supply disruption) na kusababisha upungufu mkubwa wa sukari ambayo sasa huuzwa kati ya Tsh 6000 kwa kilo badala ya bei ya Tsh 1200 ya awali. Kwa lugha nyepesi naweza kusema uamuzi huu umekuza ugumu wa maisha ya wanyonge kwa 400% . Tazama sasa jinsi maamuzi ya mtu mmoja yanavyoweza kuathiri maisha ya mamilioni ya watanzania.

KODI YA MITUMBA, NYUMBA ZA KUPANGA, ATM NA MIAMALA YA SIMU

Kodi hizi zimelenga kuwaumiza wanyonge moja kwa moja. Viwanda vya nguo vya hapa ndani havijatosheleza mahitaji ya nguo kwa watanzania wote. Aidha, viwanda hivi bado havijawa na uwezo wa kutengeneza aina mbalimbali za nguo na imara kama za mitumba. Wananchi sio wajinga hadi wang’ang’anie kuvaa chupi na sidiria za mitumba. Ni kwa sababu hakuna nguo mbadala zilizo maridadi na imara kama mitumba ndio maana wanaona ni afadhali waendelee kuvaa chupi na sidiria za mitumba. Viatu vya mitumba vimekuwa ni mkombozi wa wanyonge kwa muda mrefu. Sasa inabidi wananchi tujiandae kuvaa YEBOYEBO nyeupe na njano zinazotengenezwa na makanjibai wa hapa nchini.

Utozaji wa kodi kwa wenye nyumba za kupanga ni msumali mwingine wa moto kwenye kidonda cha wanyonge. Asilimia 99% ya watanzania wanaishi kwenye nyumba za kupanga. Kodi hii itawaumiza watanzania wanyonge na ambao hawana uwezo wa kujenga nyumba zao za kuishi kwa sababu ya ugumu wa maisha unaowakabili. Tutarajie baba wenye nyumba kupandisha kodi za pango maradufu. Hivyo, wapangaji wengi watashindwa kumudu kodi za pango na kuishi chini ya miti huku wengine wakikimbilia mapangoni kujihifadhi. Naona kasi ya watanzania kuanza kuishi mapangoni kama ilivyokuwa zama za kwanza za mawe imewadia. Tunatolewa kwenye maisha ya utu na kurudishwa kwenye maisha ya kinyama!

Kana kwamba hili halitoshi, bado mwananchi huyo huyo amebebeshwa zigo la kodi ya kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu na kupitia ATM. Makampuni ya simu yote nchini Tanzania yameongeza gharama za kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu na tayari marekebisho hayo yameishasambazwa kwa mawakala wote. Nimebahatika kuona nakala hiyo ila nilishindwa kuipiga picha na kuiattach humu kwa sababu simu yangu feki imefungiwa na TCRA.

Naomba mdau yeyote atakayeipata nakala hiyo aipige picha na kuitupia humu ili kila mtanzania aangalie maumvivu atakayopata. Na bado.....mabenki nayo yataongeza gharama za kuchukua fedha na kuangalia salio very soon....stay tuned.....tuko pamoja katika maumivu haya hadi mwisho wa dahari!

Tutarajie ukabaji na uporaji wa fedha majumbani kuongezeka kwa kuwa sasa wananchi wataamua kutunzia fedha zao kwenye michago na vibubu nyumbani badala ya kuzihifahi benki au kwenye simu.

KUVUNJA SHERIA YA KAZI

Kwa kisingizio cha kusaka wafanyakazi hewa, serikali ya Dr Magufuli imesema haitaongeza mishahara ya watumishi, imezuia upandaji wa vyeo na uhamisho wa watumishi kutoka kitengo kimoja hadi kingine (recategorization) au kutoka mwajili mmoja hadi mwajiri mwingine ambako atalipwa mshahara mkubwa kuliko ule wa sasa. Aidha, serikali imezuia ulipaji wa nauli kwa watumishi wanaoenda likizo au wanaostaafu. Kwa maana hiyo ni kwamba serikali imeaumua kuendesha nchi bila kuzingatia sheria za ajira. Hii ni hali ya hatari sana.

WAFANYAKAZI HEWA

Serikali imeanza kuwakamata baadhi ya watumishi wanaosadikiwa kuwa “wafanyakazi hewa” na kuwalazimisha kulipa fedha zilizongizwa (na mafisadi) kwenye akaunti zao. Inakuwaje mtumishi amestaafu lakini bado SERIKALI inaingiza fedha kwenye akaunti yake halafu leo serikali hiyo hiyo inakuja kumkamata na kumfungulia mashtaka? Na kibaya zaidi kuna baadhi ya watumishi ambao fedha zimeingizwa kwenye akaunti zao na kuchukuliwa na mafisadi walioziingiza pasipo mwenye akaunti kujua. Kwanini hao mafisadi waliongiza fedha kwenye akaunti hizo wasichuliwe hatua badala yake wananchi wanyonge wasiokuwa na hatia ndio wananyanyaswa? Na je, mbona hatujasikia wale mabingwa wa kuchomekea wafanyakazi hewa wakikamatwa mpaka leo hii wakati wameitia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi? Kwanini wahusika wanaachwa lakini wasiohusika wanaandamwa kila kukicha?


UKOSEFU WA FEDHA MTAANI

Kufuatia “ubanaji wa matumizi” unaofanywa na serikali ya Magufuli, mzunguko wa fedha umepungua sana hapa mtaani na kupelekea mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kwa wananchi. Ukosefu huu wa fedha umeongeza ughali wa maisha kwa wanyonge, hivyo kushindwa kumudu gharama za maisha. Wananchi wamekata tama kabisa ya maisha na wanajuta kuzaliwa katika nchi hii ya Tanganyika.


Tujiandae tuu na issue za vibaka na ujambazi mitaani kwa hii hali...HALI NI MBAYAAAA
 
msema ukweli ni mpenzi wa MUNGU! nchi ilikuwa shamba la bibi, na raisi wetu anatutoa huko kwa msaada wa MUNGU...tuendelee kumwombea maana sisi pia tuwajibike upande wetu, tuwe wabunifu, tuache kulalamika na ku think negative!
angalieni msije baki jangwani....msimuudhi malaika mwema! tujenge nchi yetu kwa pamoja... ubarikiwe sana ndugu yangu!


Tatizo wanaoumizwa ni watu wa hali ya chini, mafisadi papa mbona hawaguswi, Lungumi imeishilia wapi mbona kimya?, Hao waliochukua fedha za wafanyakazi hewa mbona wao hawawajibishwi wanaowajibishwa ni wafanyakazi ambao hawajui hata hela hizo kama walikuwa wanalipwa.

Tatizo sasa wanaobanwa ni watu wa chini, wanaohamisha fedha katika mitandao ya simu ni watu wa hali ya chini, Matajiri wao hawatumii hii mitandao, wanatumia CHEQUE, na njia za benki.
Mitumba wanaovaa ni watu wa chini,
Wenye nyumba ni Wenye nazo, hivyo kodi watampandishia mtu wa chini ambaye hana nyumba anategemea kupanga ndio mzigo woote wa kodi atabebeshwa yeye.
 
Mnaodhani kuwa Dr Magufuli ni mtetezi wa wanyonge (kama anvyojinukuuu mara kwa mara) mnapaswa kutafakari upya. Tangu Dr Magufuli alipoingia madarakani amefanikiwa kukanyaga haki mbalimbali za raia pamoja na kufanya maisha ya mamilioni ya watanzania wa kawaida yawe magumu zaidi kuliko ilivyokuwa katika utawala wa Dr JK.

Kuna baadhi ya maamuzi ya kikandamizaji ninayoweza kuyakumbuka ambayo madhara yake yamewaumiza wananchi huku wanafiki na wachochezi wachache wakichekelea wakati wanajua haki za msingi za wananchi zimekanyagwa:

KUINGILIA MFUMO WA BIASHARA HURIA

Ni dhahiri mfumo wa uchumi wa sasa ni wa BIASHARA HURIA – kwamba upatikanaji wa bidhaa (supply) na na mahitaji (demand) ndio huamua bei (price). Kazi ya serikali sio kufanya biashara ila kazi yake ni kurahisisha mazingira ya biashara na kukusanya kodi.

Lakini tumeshuhudia Dr Magufuli akizuia uagizaji wa sukari (intentional supply disruption) na kusababisha upungufu mkubwa wa sukari ambayo sasa huuzwa kati ya Tsh 6000 kwa kilo badala ya bei ya Tsh 1200 ya awali. Kwa lugha nyepesi naweza kusema uamuzi huu umekuza ugumu wa maisha ya wanyonge kwa 400% . Tazama sasa jinsi maamuzi ya mtu mmoja yanavyoweza kuathiri maisha ya mamilioni ya watanzania.

KODI YA MITUMBA, NYUMBA ZA KUPANGA, ATM NA MIAMALA YA SIMU

Kodi hizi zimelenga kuwaumiza wanyonge moja kwa moja. Viwanda vya nguo vya hapa ndani havijatosheleza mahitaji ya nguo kwa watanzania wote. Aidha, viwanda hivi bado havijawa na uwezo wa kutengeneza aina mbalimbali za nguo na imara kama za mitumba. Wananchi sio wajinga hadi wang’ang’anie kuvaa chupi na sidiria za mitumba. Ni kwa sababu hakuna nguo mbadala zilizo maridadi na imara kama mitumba ndio maana wanaona ni afadhali waendelee kuvaa chupi na sidiria za mitumba. Viatu vya mitumba vimekuwa ni mkombozi wa wanyonge kwa muda mrefu. Sasa inabidi wananchi tujiandae kuvaa YEBOYEBO nyeupe na njano zinazotengenezwa na makanjibai wa hapa nchini.

Utozaji wa kodi kwa wenye nyumba za kupanga ni msumali mwingine wa moto kwenye kidonda cha wanyonge. Asilimia 99% ya watanzania wanaishi kwenye nyumba za kupanga. Kodi hii itawaumiza watanzania wanyonge na ambao hawana uwezo wa kujenga nyumba zao za kuishi kwa sababu ya ugumu wa maisha unaowakabili. Tutarajie baba wenye nyumba kupandisha kodi za pango maradufu. Hivyo, wapangaji wengi watashindwa kumudu kodi za pango na kuishi chini ya miti huku wengine wakikimbilia mapangoni kujihifadhi. Naona kasi ya watanzania kuanza kuishi mapangoni kama ilivyokuwa zama za kwanza za mawe imewadia. Tunatolewa kwenye maisha ya utu na kurudishwa kwenye maisha ya kinyama!

Kana kwamba hili halitoshi, bado mwananchi huyo huyo amebebeshwa zigo la kodi ya kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu na kupitia ATM. Makampuni ya simu yote nchini Tanzania yameongeza gharama za kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu na tayari marekebisho hayo yameishasambazwa kwa mawakala wote. Nimebahatika kuona nakala hiyo ila nilishindwa kuipiga picha na kuiattach humu kwa sababu simu yangu feki imefungiwa na TCRA.

Naomba mdau yeyote atakayeipata nakala hiyo aipige picha na kuitupia humu ili kila mtanzania aangalie maumvivu atakayopata. Na bado.....mabenki nayo yataongeza gharama za kuchukua fedha na kuangalia salio very soon....stay tuned.....tuko pamoja katika maumivu haya hadi mwisho wa dahari!

Tutarajie ukabaji na uporaji wa fedha majumbani kuongezeka kwa kuwa sasa wananchi wataamua kutunzia fedha zao kwenye michago na vibubu nyumbani badala ya kuzihifahi benki au kwenye simu.

KUVUNJA SHERIA YA KAZI

Kwa kisingizio cha kusaka wafanyakazi hewa, serikali ya Dr Magufuli imesema haitaongeza mishahara ya watumishi, imezuia upandaji wa vyeo na uhamisho wa watumishi kutoka kitengo kimoja hadi kingine (recategorization) au kutoka mwajili mmoja hadi mwajiri mwingine ambako atalipwa mshahara mkubwa kuliko ule wa sasa. Aidha, serikali imezuia ulipaji wa nauli kwa watumishi wanaoenda likizo au wanaostaafu. Kwa maana hiyo ni kwamba serikali imeaumua kuendesha nchi bila kuzingatia sheria za ajira. Hii ni hali ya hatari sana.

WAFANYAKAZI HEWA

Serikali imeanza kuwakamata baadhi ya watumishi wanaosadikiwa kuwa “wafanyakazi hewa” na kuwalazimisha kulipa fedha zilizongizwa (na mafisadi) kwenye akaunti zao. Inakuwaje mtumishi amestaafu lakini bado SERIKALI inaingiza fedha kwenye akaunti yake halafu leo serikali hiyo hiyo inakuja kumkamata na kumfungulia mashtaka? Na kibaya zaidi kuna baadhi ya watumishi ambao fedha zimeingizwa kwenye akaunti zao na kuchukuliwa na mafisadi walioziingiza pasipo mwenye akaunti kujua. Kwanini hao mafisadi waliongiza fedha kwenye akaunti hizo wasichuliwe hatua badala yake wananchi wanyonge wasiokuwa na hatia ndio wananyanyaswa? Na je, mbona hatujasikia wale mabingwa wa kuchomekea wafanyakazi hewa wakikamatwa mpaka leo hii wakati wameitia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi? Kwanini wahusika wanaachwa lakini wasiohusika wanaandamwa kila kukicha?


UKOSEFU WA FEDHA MTAANI

Kufuatia “ubanaji wa matumizi” unaofanywa na serikali ya Magufuli, mzunguko wa fedha umepungua sana hapa mtaani na kupelekea mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kwa wananchi. Ukosefu huu wa fedha umeongeza ughali wa maisha kwa wanyonge, hivyo kushindwa kumudu gharama za maisha. Wananchi wamekata tama kabisa ya maisha na wanajuta kuzaliwa katika nchi hii ya Tanganyika.


JUZI nafsi iliniiuma kijana amekamatwa na askari kisa Kuuza viazi vya kuchoma, viazi vyake vimemwagwa ktk fuko wakavichukua. Hawaangalii kuwa huu ni mtaji wa mtu, hawaangalii kuwa hiki ni chakula wahifadhi vizuri, hawajali utu.
yaani sasa ni mabavu sana kila mmoja anajichukulia.....ahh tubadilike bwana..
 
Tatizo wanaoumizwa ni watu wa hali ya chini, mafisadi papa mbona hawaguswi, Lungumi imeishilia wapi mbona kimya?, Hao waliochukua fedha za wafanyakazi hewa mbona wao hawawajibishwi wanaowajibishwa ni wafanyakazi ambao hawajui hata hela hizo kama walikuwa wanalipwa.

Tatizo sasa wanaobanwa ni watu wa chini, wanaohamisha fedha katika mitandao ya simu ni watu wa hali ya chini, Matajiri wao hawatumii hii mitandao, wanatumia CHEQUE, na njia za benki.
Mitumba wanaovaa ni watu wa chini,
Wenye nyumba ni Wenye nazo, hivyo kodi watampandishia mtu wa chini ambaye hana nyumba anategemea kupanga ndio mzigo woote wa kodi atabebeshwa yeye.

Unajua hata mja mzito ikifika wakati wa kujifungua ndiyo uchungu una zidi. ..lakini mtoto akisha toka ni furaha ya ajabu. ...haya mateso yatapita tu...utakuja kaniambia. ...ubarikiwe sana Kwa hekima na busara
 
ra
Mnaodhani kuwa Dr Magufuli ni mtetezi wa wanyonge (kama anvyojinukuuu mara kwa mara) mnapaswa kutafakari upya. Tangu Dr Magufuli alipoingia madarakani amefanikiwa kukanyaga haki mbalimbali za raia pamoja na kufanya maisha ya mamilioni ya watanzania wa kawaida yawe magumu zaidi kuliko ilivyokuwa katika utawala wa Dr JK.

Kuna baadhi ya maamuzi ya kikandamizaji ninayoweza kuyakumbuka ambayo madhara yake yamewaumiza wananchi huku wanafiki na wachochezi wachache wakichekelea wakati wanajua haki za msingi za wananchi zimekanyagwa:

KUINGILIA MFUMO WA BIASHARA HURIA

Ni dhahiri mfumo wa uchumi wa sasa ni wa BIASHARA HURIA – kwamba upatikanaji wa bidhaa (supply) na na mahitaji (demand) ndio huamua bei (price). Kazi ya serikali sio kufanya biashara ila kazi yake ni kurahisisha mazingira ya biashara na kukusanya kodi.

Lakini tumeshuhudia Dr Magufuli akizuia uagizaji wa sukari (intentional supply disruption) na kusababisha upungufu mkubwa wa sukari ambayo sasa huuzwa kati ya Tsh 6000 kwa kilo badala ya bei ya Tsh 1200 ya awali. Kwa lugha nyepesi naweza kusema uamuzi huu umekuza ugumu wa maisha ya wanyonge kwa 400% . Tazama sasa jinsi maamuzi ya mtu mmoja yanavyoweza kuathiri maisha ya mamilioni ya watanzania.

KODI YA MITUMBA, NYUMBA ZA KUPANGA, ATM NA MIAMALA YA SIMU

Kodi hizi zimelenga kuwaumiza wanyonge moja kwa moja. Viwanda vya nguo vya hapa ndani havijatosheleza mahitaji ya nguo kwa watanzania wote. Aidha, viwanda hivi bado havijawa na uwezo wa kutengeneza aina mbalimbali za nguo na imara kama za mitumba. Wananchi sio wajinga hadi wang’ang’anie kuvaa chupi na sidiria za mitumba. Ni kwa sababu hakuna nguo mbadala zilizo maridadi na imara kama mitumba ndio maana wanaona ni afadhali waendelee kuvaa chupi na sidiria za mitumba. Viatu vya mitumba vimekuwa ni mkombozi wa wanyonge kwa muda mrefu. Sasa inabidi wananchi tujiandae kuvaa YEBOYEBO nyeupe na njano zinazotengenezwa na makanjibai wa hapa nchini.

Utozaji wa kodi kwa wenye nyumba za kupanga ni msumali mwingine wa moto kwenye kidonda cha wanyonge. Asilimia 99% ya watanzania wanaishi kwenye nyumba za kupanga. Kodi hii itawaumiza watanzania wanyonge na ambao hawana uwezo wa kujenga nyumba zao za kuishi kwa sababu ya ugumu wa maisha unaowakabili. Tutarajie baba wenye nyumba kupandisha kodi za pango maradufu. Hivyo, wapangaji wengi watashindwa kumudu kodi za pango na kuishi chini ya miti huku wengine wakikimbilia mapangoni kujihifadhi. Naona kasi ya watanzania kuanza kuishi mapangoni kama ilivyokuwa zama za kwanza za mawe imewadia. Tunatolewa kwenye maisha ya utu na kurudishwa kwenye maisha ya kinyama!

Kana kwamba hili halitoshi, bado mwananchi huyo huyo amebebeshwa zigo la kodi ya kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu na kupitia ATM. Makampuni ya simu yote nchini Tanzania yameongeza gharama za kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu na tayari marekebisho hayo yameishasambazwa kwa mawakala wote. Nimebahatika kuona nakala hiyo ila nilishindwa kuipiga picha na kuiattach humu kwa sababu simu yangu feki imefungiwa na TCRA.

Naomba mdau yeyote atakayeipata nakala hiyo aipige picha na kuitupia humu ili kila mtanzania aangalie maumvivu atakayopata. Na bado.....mabenki nayo yataongeza gharama za kuchukua fedha na kuangalia salio very soon....stay tuned.....tuko pamoja katika maumivu haya hadi mwisho wa dahari!

Tutarajie ukabaji na uporaji wa fedha majumbani kuongezeka kwa kuwa sasa wananchi wataamua kutunzia fedha zao kwenye michago na vibubu nyumbani badala ya kuzihifahi benki au kwenye simu.

KUVUNJA SHERIA YA KAZI

Kwa kisingizio cha kusaka wafanyakazi hewa, serikali ya Dr Magufuli imesema haitaongeza mishahara ya watumishi, imezuia upandaji wa vyeo na uhamisho wa watumishi kutoka kitengo kimoja hadi kingine (recategorization) au kutoka mwajili mmoja hadi mwajiri mwingine ambako atalipwa mshahara mkubwa kuliko ule wa sasa. Aidha, serikali imezuia ulipaji wa nauli kwa watumishi wanaoenda likizo au wanaostaafu. Kwa maana hiyo ni kwamba serikali imeaumua kuendesha nchi bila kuzingatia sheria za ajira. Hii ni hali ya hatari sana.

WAFANYAKAZI HEWA

Serikali imeanza kuwakamata baadhi ya watumishi wanaosadikiwa kuwa “wafanyakazi hewa” na kuwalazimisha kulipa fedha zilizongizwa (na mafisadi) kwenye akaunti zao. Inakuwaje mtumishi amestaafu lakini bado SERIKALI inaingiza fedha kwenye akaunti yake halafu leo serikali hiyo hiyo inakuja kumkamata na kumfungulia mashtaka? Na kibaya zaidi kuna baadhi ya watumishi ambao fedha zimeingizwa kwenye akaunti zao na kuchukuliwa na mafisadi walioziingiza pasipo mwenye akaunti kujua. Kwanini hao mafisadi waliongiza fedha kwenye akaunti hizo wasichuliwe hatua badala yake wananchi wanyonge wasiokuwa na hatia ndio wananyanyaswa? Na je, mbona hatujasikia wale mabingwa wa kuchomekea wafanyakazi hewa wakikamatwa mpaka leo hii wakati wameitia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi? Kwanini wahusika wanaachwa lakini wasiohusika wanaandamwa kila kukicha?


UKOSEFU WA FEDHA MTAANI

Kufuatia “ubanaji wa matumizi” unaofanywa na serikali ya Magufuli, mzunguko wa fedha umepungua sana hapa mtaani na kupelekea mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kwa wananchi. Ukosefu huu wa fedha umeongeza ughali wa maisha kwa wanyonge, hivyo kushindwa kumudu gharama za maisha. Wananchi wamekata tama kabisa ya maisha na wanajuta kuzaliwa katika nchi hii ya Tanganyika.
Kazi anayo ifanya Raisi tunaiona na tunamkubali nchi ilikuwa imefika pabaya sana,wale wote wanaomponda kama siyo mazezeta basi ni miongoni mwa wale walikuwa wananufaika na ule mfumo fisidi aka majipu.Mungu yuko pamoja na JPM.
 
Lazima nchi iende mbele kama ulizoea kula jasho la wengine ndiyo madhala unayokumbana nayo sasa utakalia kulalamika tu lakini raisi anaendelea kupiga kazi bila wasiwasi sisi kazi yetu ni kumuombea tu.
 
Lazima nchi iende mbele kama ulizoea kula jasho la wengine ndiyo madhala unayokumbana nayo sasa utakalia kulalamika tu lakini raisi anaendelea kupiga kazi bila wasiwasi sisi kazi yetu ni kumuombea tu.
mkuu, mimi nakula jasho langu mwenyewe ila ninacholalamikia ni SERIKALI YA MAKUFURI KULA JASHO LANGU huku ikiwaacha wazungu waedelee kuchimba madini bila kulipa kodi pamoja na kusafirisha twiga na wanyama wengine nje ya nchi bila kuchukuliwa hatua.
 
Tulihitaji sana mtu wa kusaidia kubadili mfumo wa uendeshaji nchi na utohaji haki kwa watanzani. Sasa mtu tumempata. Mfumo hauwezi kubadilishwa na mtu bila baadhi ya watu kujitolea muhanga. Kitendo cha baadhi yetu kuonekana haki zetu zimekanyangwa na msaidizi wa kubadilisha mfumo, ni mojawapo ya kujitoa muhanga kwetu kwa ajiri ya kubadilisha mfumo. Kwa hili tujipongeze kwani tumejitendea haki na wale wa vizazi vijavyo vya watanzania. Tumuunge mkono rais.
 
Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Joseph Magufuli, naomba usipoteze muda kuwasikiliza hawa waliofirisika kifikra. Wanapobwatabwata mitaani wewe piga kazi kwani sisi watanzania tunajua unachokifanya. NCHI HII ILIKARIBIA KUOZA, HIVYO NI LAZIMA KUFANYA MABADILIKO MAKUBWA ILI KURUDISHA NIDHAMU NA UWAJIBIKAJI. KATIKA KUTEKELEZA HAYO USISIKILIZE KELELE ZA WATU WALA USIGEUKE NYUMA, WEWE SONGA MBELE.
hvi umesoma uzi kweli au unakurupuka tu kujibu bila kuelewa jambo linaloongelewa hapa? hivi, kwa mfano Dr Makufuri anapozuia watumishi wasipandishwe vyeo wala kulipwa fedha za likizo unaona yuko sawa? labda twende na hoja moja moja ndipo utanielewa.
 
Back
Top Bottom