Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

Ahsante Mkuu kwa kutupa taarifa. Kumbe nilikuwa sahihi kutojiunga kwenye promosheni zao. Ila Mkuu umelea tatizo muda mrefu. Ungetutonya mapema. Miaka kumi mingi sana watanzania tumeumizwa.
Asingeweza kufanya hivyo wakati yupo kibaruani alikuwa kwenye system. Alikuwa anamtumikia kafiri ili apate mradi wake baada kuondoka hana cha kupoteza tena
 
Wakuu napenda kuwakumbusha kuwa kuna wizi mpya unaofanywa na kampuni ya vodacom kupitia matumizi ya facebook bila malipo. Hawa watu ni waongo wa kutupwa....hakuna kitu kama hicho...ukifungua facebook isiyokuwa na picha unaliwa fedha kama kawaida. Naomba TCRA muingilie kati wizi huu.
 
Sio simu tu, huduma zote tunanyonywa... Hospital za serikali unambiwa ulete vifaa vya kujifungulia, vya kazi gani sasa wakati huduma bure na tena hapo hapo nesi anaweza ajakwambia yeye anavyo ununue kwake... Anamnunia mgonjwa hadi apewe hela atamuhudumia vizuri hadi ushangae... Si ni tunanyonywa mwanzo mwisho
 
Mimi sina hamu na vodacom , nakumbuka juzi kati kipindi wananidai 1450 ya nipige tafu nikabofya *149*42# ili nijiunge na bando la mb 500 kwa sh 500 kwa wiki nikaweka pesa m pesa kila nikitaka kununua naambiwa mchakato umezuiliwa ile napiga huduma kwa wateja muhudumu wa voda ananiambia heti huwezi kununua bando hili kwa m pesa (kumbuka hapo wananidai ) nikaona isiwe tabu nikanunua jumla vocha ya 2000 ile naweka tu majamaa yakakata 1450 hapo hapo nikabakiwa na 550 haya nikajaribu tena kujiunga naambiwa huduma hii haipatikani kwa sasa jaribu tena baadae, nikapiga huduma kwa wateja kakapokea kamdada flan nikakauliza mbona kila nikijaribu kujinga na bando la net la wiki kwa 500 sifanikiwi naambiwa huduma hii haipatikani kwa sasa ,
Kakanijibu "SASA WEWE UMEAMBIWA HUDUMA HII HAIPATIKANI KWA SASA UNATAKA NIKWAMBIE NINI ZAIDI?"
Kumbuka hapo nimeshaingia mkenge nimelipa deni lao lote la nipige tafu , nikaona isiwe inshu nikakata simu,
BALAA likaja nilipoingia katika kuperuzi tovuti za bure kwenye www.internet.org mzee nikafungua facebook ya bila malipo kama dakika 1 nikatoka nikaenda goal dot com kuangalia matokeo kama sekunde 50 hivi ile nakuja kuangalia salio nakuta limebaki 508 majamaa yameshakula sh 42 wakati yananadi tovuti yoyote inayopatikana kwenye internet.org ni ya bure kumbe ukiwa na salio yanang'amua salio kimya kimya ,
Nikaona huu ni upuuzi huu nikanunua tu bando la siku la internet napo nashangaa napewa mb 70 kwa tsh 500 wakati halotel mb 120 ni 499 aisee kwa kifupi VODACOM TANZANIA ni mafisadi sugu .
 
nitarudi baadae kuchangia
 
Mkuu kumbe nawe umeishaibiwa mno na hawa makaburu? Mimi niliwashtukia kitambo sana. Ule ujinga wanaonadi eti facebook isiyokuwa na picha inapatikana bure ni WIZI mtupu. Ukitaka kuprove hili ingia ukiwa na salio la Tsh 0 uone.....huwezi kupata hiyo huduma hadi uongeze salio. Hii maana yake ni nini? Ina maana huduma hii sio ya bure kama wanavyodai...ni utapeli wa kimataifa. Nashangaa hata TCRA wameamua kutuacha tuibiwe kijinga hivi bila kuwachukulia hatua hawa matapeli. Wako busy kukamata watu wanaopost maoni yao dhidi ya mafisadi huku wakituacha wananchi tunaibiwa kila kukicha.
 
Watanzania karibu wote viongozi mbaka wananchi wanalalamika tu,tumegeuka walalamikaji katika nchi yetu
Nini kifanyike:
Kama ushahidi upo namna tunavyo ibiwa sisi kama watumiaji wa hii mitandao tuanze sasa kuchukua hatua
Wanafamilia wa JF kwa umoja wetu tukusanye sahini za wadau wetu wote,tuandikie majina yetu pamoja na namba zetu za simu tumtafute wakili nguli twendeni mahakamani tukafungue mashtaka ya kuibiwa mchana kweupe na haya makampuni ya simu,na endapo sisi kama watanzania hatuna huo ushahidi wa kuibiwa basi tuache kulishana Matango pori
Tuanze sasa kuchukua hatua tuache kulalamika bila sababu..
 
VP kuhusu hii jaza ujazwe, tia utiwe nazo pia ni fake offer?
 
tpaul hapa ni shida tupu ndugu yangu mi bora nibaki halotel tu.
 
Asante sana mleta mada. Pia kuna wizi mwingine - nazungumzia Vodacom. Ukijiunga mitandao yote kiasi cha dakika utakachopata hakifikii hata nusu ya dakika za Vodacom-Vodacom. Kwa shilingi 1,000 mitandao yote unapata dakika 22 tu wakati kwenye vodacom-vodacom unapata dakika 50 na dakika 5 mitandao yote (kifurushi cha siku).

Lakini sasa, ukinunua muda wa maongezi kwa mitandao yote ya shilingi 1,000 wakati tayari ulikuwa umeshajiunga kwenye vodacom -vodacom kwa shilingi 1,000 pia, wizi unaanzia hapo. Ukipiga simu kwenye mtandao mwingine ukatumia dakika 7, kwenye salio la mitandao yote unabakia na dakika 15, na kwenye voda-voda unabakia na zile dakika 50. Simu inayofuata ukipiga voda-voda kwa dakika 15, badala ya kupunguza hicho kiasi kwenye dakika 50 za voda-voda, wanakata dakika zote 15 kwenye lile salio la mitandao ingine ambalo ulinunua kwa bei ghali. Wanakutumia ujumbe saa hiyo hiyo kwamba muda wako wa maongezi kwenye mitandao yote umeisha ilhali ulikuwa umepiga voda-voda na sio mtandao mwingine. Huu ni wizi mkubwa. Nadhani hao wafanyakazi wa Vodacom (labda wanashirikiana na wa TCRA) bila shaka ndio wanahusika na wizi huo. Jamani tunawaomba wakurugenzi wa Vodacom na TCRA mliangalie hili !
 
"Hatimae wengi wao hukata tamaa na kukubali kuliwa" aisee hii nayo kali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…