Jinsi Gani Tv inagharimu kwenye maisha yetu

Alagwa

Member
May 30, 2012
95
85
Tuelewane kidogo... Ishu sio bei ya tv au ukubwa wa tv yako bali gharama ya tv yako kwenye Maisha yako nikubwa sana kiuchumi kama utapiga Mahesabu vizuri.

Tunanunua kwa gharama sana ili kujiburudisha lakini sio gharama hiyo tuu pia tunatumia muda mwingi kuangalia tv hiyo ambapo muda huo tungeutumia kufikiria au kufanya shughuli itakayokuingizia kipato zaidi kama unaona shughuli hakuna basi tenga hata muda kidogo wa kutafakari Maisha yako na mishe mishe zako alafu ndio peleka macho yako kwenye tv baada ya kutumia muda kujiwekezea mwenyewe binafsi kwa kujitafakari.

Sisemi tv ni mbaya ila isichukue muda mwingi kwenye maisha yako kiasi cha kukosa muda na familia hapa nimeitaja familia kwakuwa wengi tunafikiri muda tunaoangalia tv na familia ndio muda wa familia hapana muda wa kuangalia tv hata kama familia nzima ipo ila ni muda wa tv lakini sio muda mnao utumia kuongea na kujadili mambo ya familia.

Leo nimeandika kwa kifupi tuu. Je wewe unaonaje hili?

Screenshot_20230417_214834_Facebook.jpg
 
Tutafakari kwa masaa mangapi, na tuangalie TV kwa masaa mangapi ili kuwe na balance???
 
Na jirani yangu mmoja ni mama wa watoto wawili ikifika tuuu asubuhi kwenye Tv swala la kupika kwake ni kipengele kila kitu Dada wa Kazi ,

Tamthilia ya HUBA inamtafuna umwambii kitu
 
Too much is harmful, kitu chochote ukifanya sana kinaweza Kukuletea madhara, including huko kutafuta maisha, unaweza ukatafuta maisha mda wote Na ukawa unajiumiza kuliko huyo anae angalia TV.

Cha muhimu balance tu maisha yako.
 
Tuelewane kidogo... Ishu sio bei ya tv au ukubwa wa tv yako bali gharama ya tv yako kwenye Maisha yako nikubwa sana kiuchumi kama utapiga Maesabu vizuri.

.... macho yako kwenye tv baada ya kutumia muda kujiwekezea mwenyewe binafsi kwa kujitafakari... si semi tv ni mbaya ila isichukue muda mwingi ....
baada = badala
si semi = sisemi
masahihisho madogo ya lugha yetu adhimu.
 
Watanzania wengi tuna muda mwingi na hatujui tuutumie kufanya nini. Achana na motivational speakers wanasema uamke saa 10 alfajiri wakati huna mchongo wowote.

Tusiache kuishi wakuu, let us enjoy life. Hatma ya mwanadamu ni kifo.
 
Tuelewane kidogo... Ishu sio bei ya tv au ukubwa wa tv yako bali gharama ya tv yako kwenye Maisha yako nikubwa sana kiuchumi kama utapiga Mahesabu vizuri.

Tunanunua kwa gharama sana ili kujiburudisha lakini sio gharama hiyo tuu pia tunatumia muda mwingi kuangalia tv hiyo ambapo muda huo tungeutumia kufikiria au kufanya shughuli itakayokuingizia kipato zaidi kama unaona shughuli hakuna basi tenga hata muda kidogo wa kutafakari Maisha yako na mishe mishe zako alafu ndio peleka macho yako kwenye tv baada ya kutumia muda kujiwekezea mwenyewe binafsi kwa kujitafakari.

Sisemi tv ni mbaya ila isichukue muda mwingi kwenye maisha yako kiasi cha kukosa muda na familia hapa nimeitaja familia kwakuwa wengi tunafikiri muda tunaoangalia tv na familia ndio muda wa familia hapana muda wa kuangalia tv hata kama familia nzima ipo ila ni muda wa tv lakini sio muda mnao utumia kuongea na kujadili mambo ya familia.

Leo nimeandika kwa kifupi tuu. Je wewe unaonaje hili?

View attachment 2591457
Ndugu zangu wako kijinini hakuna ata umeme ila Ni maskini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom