Idugunde
JF-Expert Member
- May 21, 2020
- 6,273
- 6,637
Siasa sio uadui na siasa ni suala muhimu kwenye ustawi wa jamii.Lakini pale mwanasiasa au Chama cha siasa kinapoitumia vibaya siasa huwa na matokeo mabaya sana.
Sisi bahati nzuri Chama tawala kimekuwa makini sana katika kuwashughulikia wanasiasa na vyama ambavyo vimekuwa na mbaya juu ya Taifa letu.
Act wazalendo na kiongozi wao walidiriki kuandika WB barua eti nchi yetu isipewe mkopo wa kuboresha elimu hapa nchini kwetu. Kwa akili ya kawaida tu hawa ni wazalendo kama wanavyojiita? Wanadai kuna ubaguzi katika utoaji elimu. Kisa serikali haitaki kuruhusu wanafunzi wanaondekeza ngono na kupata mimba kuendelea na shule.
Hao hao Act wazalendo walizunguka kwa mabeberu na kusema kuna uminywaji mkubwa wa demokrasia hapa nchini. Kama kuna uminywaji hicho chama kingekuwepo?
Limekuja Janga la Covid-19. Wakaungana na Chadema na kushinikiza serikali iweke lockdown. Na kila kaya ipewe laki tatu. Hili jambo linawezekana? Mbaya zaidi waliungana na kuichafua nchi yetu na kusema inapika data eti watu kwa maelfu wamekufa na wanazikwa usiku.
Kama makosa kama hayo yalitokea walipaswa kuongea na vyombo kama ITV au TBC na sio kwenda Aljazeera na Bbc kuichafua nchi yetu.
Kwa hiyo Act wazalendo fake na Chadema wapiga madili. Wananchi wamechukia sana. Maana hamna umoja na taifa letu. Nia yenu ni kuleta mpasuko na mgawanyiko. Hivyo Oktoba mtapata mlichokipanda.
Nawaambia mtavuna mlichopanda.
Sisi bahati nzuri Chama tawala kimekuwa makini sana katika kuwashughulikia wanasiasa na vyama ambavyo vimekuwa na mbaya juu ya Taifa letu.
Act wazalendo na kiongozi wao walidiriki kuandika WB barua eti nchi yetu isipewe mkopo wa kuboresha elimu hapa nchini kwetu. Kwa akili ya kawaida tu hawa ni wazalendo kama wanavyojiita? Wanadai kuna ubaguzi katika utoaji elimu. Kisa serikali haitaki kuruhusu wanafunzi wanaondekeza ngono na kupata mimba kuendelea na shule.
Hao hao Act wazalendo walizunguka kwa mabeberu na kusema kuna uminywaji mkubwa wa demokrasia hapa nchini. Kama kuna uminywaji hicho chama kingekuwepo?
Limekuja Janga la Covid-19. Wakaungana na Chadema na kushinikiza serikali iweke lockdown. Na kila kaya ipewe laki tatu. Hili jambo linawezekana? Mbaya zaidi waliungana na kuichafua nchi yetu na kusema inapika data eti watu kwa maelfu wamekufa na wanazikwa usiku.
Kama makosa kama hayo yalitokea walipaswa kuongea na vyombo kama ITV au TBC na sio kwenda Aljazeera na Bbc kuichafua nchi yetu.
Kwa hiyo Act wazalendo fake na Chadema wapiga madili. Wananchi wamechukia sana. Maana hamna umoja na taifa letu. Nia yenu ni kuleta mpasuko na mgawanyiko. Hivyo Oktoba mtapata mlichokipanda.
Nawaambia mtavuna mlichopanda.