Habari wadau
Nimekua nikisumbuliwa na maumivu ya jino kwa miezi kadhaa sasa, nimekwenda hospitali mara mbili kucheki kama jino lina tatizo mara ya pili nililazimika kupigwa X-Ray ya kinywa lakini majibu ya Dr yalikua Jino langu halina shida wala halijatoboka hvyo akanipa dawa ambayo kwa mujibu wa maelekezo ya Dr ingesaidia kulinda fizi.
Nimetumia dawa hizo had kumaliza bila mabadiliko yoyote, bado nasumbuliwa na maumivu ya jino hasa ninapokula/kunywa vitu vya moto au baridi. Naomba kama kuna dawa mbadala mnijuze.
Unakumbuka Nani Labda Ulimng'ata Mara Ya Mwisho?
Sikuwahi kung'ata mtu mkuu
Tumia Mikojo, hutibu Maumivu ya meno milele na milele., mm ilinsaidia sana
Tumia Mikojo, hutibu Maumivu ya meno milele na milele., mm ilinsaidia sana
Unakumbuka Nani Labda Ulimng'ata Mara Ya Mwisho?
Mkuu jitahidi kuswaki kila baada ya mlo.Na ukipiga baada ya kula usiku na kuswaki, usile kitu chochote usiku huo.Kwa sasa nenda famasi ukanunue syrup tunaita medi oral.Namna ya kutumia utasoma kwenye kasha.Utasahau matatizo ya meno.By Pastor Achachanda
Akhsante Sana Mkuu Na Ubarikiwe Kwa Msaada Wako Huu Mkubwa Kwangu Kwani Maumivu Ninayoyapata Yanazidi Hata Ya Wale Watia Nia CCM Watakaoondolewa Leo Dodoma Akiwemo Nanihiiiiiiiiiiiii.
Dawa ya Jino ni kung'oa!