Jini, mapepo na mizimu ni kitu kimoja. Mizimu ni majini/mapepo yenye nguvu katika familia, ukoo au jamii fulani. Mashetani ni malaika walioasi na wapo katika daraja la juu na wana nguvu zaidi ya mapepo/majini/mizimu.
Jinamizi kusababishwa na majini yapendayo kumwingia mtu akia usingizini na kuchukua hatamu ya sehemu muhimu katika ubongo wa mwanadamu ili kuweza kufanya watakavyo. Mchawi aliye katika roho anaweza pia akamwingia mtu kama jinamizi. Hawawezi kuchukua hatamu ya roho yako kwani roho yako ina nguvu ya ajabu ya kimungu, hivyo huchukua hatamu ya mwili wako tu.
Wanapenda pia kuchukua hatamu ya uwezo wa mtu wa kutamka ili mtu asiweze kupata msaada kwa wenzake au kwa Mungu (Yesu Kristo).
Cha kufanya unapopata jinamizi ni kujitahidi kuita Jina la Yesu. Kama huwezi basi fikiri au leta picha ya Yesu kichwani na mara moja jinamizi hutoweka.
Ili usipate jinamizi dawa yake ni kuwa mtu wa Yesu Kristo, yaani mtu aliyekombolewa kwa Damu ya Yesu Kristo na kuishi maisha safi. Pia usikubali hata siku moja kulala bila kusali na kujiweka chini ya ulinzi wa Yesu Kristo. Ukifanya hivyo majinamizi utasikia tu hadithi zake kwa wengine.