Ni takribani miaka miwili sasa tangu kufanyika uchaguzi mkuu wa Rais ,mbunge na diwani inchini,lakini huwezi amini Mtanzania, mbunge wa jimbo la Magu mkoani Mwanza CCM hajawahi kuchangia,kutoa mada,kuhoji,wala,kukumbushia mambo mbalimbali yanayohusu wanainchi na wapiga kura wake.kuna ahadi kibao aliahidi faatilia hakuna hata moja walau aliianzisha,ahadi ya ujenzi wa bwawa kubwa la maji kijiji cha Jinjimili,majengo mawili ya madarasa Jinjimili,Mradi wa umeme kutoka JIneri la Pamba Kasori kupita Kabila hadi Mahaha pia bei ya Pamba ilihari yeye ndiye Mwenyekiti wa Board hiyo na pia ujenzi wa Minara ya Simu maeneo mbalimbali ya JIMBO na upelekaji wa Maji mjini Magu. Wapi, Wapi Mbunge hata kuongea tu,hoi kazi kupiga makofi bungeni na kuunga mkono hoja za wengine, Mjadala wa katiba ulikuwa hot sana pale MJENGONI lakini jamaa kamwe hakuongea hata, kana kwamba katiba inayoundwa haiwagusi wakaazi wa JIMBO hilo,Hii ni Hasara nyingine kwa Jimbo la Magu.Ni Muda wa kutafakari uwepo wa Mbunge kama huyo na pia kuitumia fursa hii vizuri wakati ukifika,Siyo Kupokea kanga,sabuni,na vijisenti wakati mhimu kama wa uchaguzi unapofika.Nawasilisha Kamanda Kutoka JINJIMILI.