fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,073
Busega jimbo ambalo lilikwa wilaya ya Magu sasa ni wilaya kamili, DC Paul Mzindakaya, kijana wa CCM ambaye baba yake amekula nchi akashiba sasa ni zamu za watoto wa wakubwa kuanza kujengewa misingi ya kututawala milele. Jimbo la Busega kutoka kwa Chegeni hadi kwa binamu yake Kamani, sasa halitakuwa chini ya CCM tena. Sababu ni nyingi lakini moja ni kushindwa kufanya au kushawishi maendeleo kwa wanandugu hao wawili yaani Chegeni na Kamani. Nyingine ni ugomvi wote ambapo vile wanafahamiana sana na kujua sana wametiana madoa makubwa, tatu ni ukweli kwamba vijana wa nassa waliamka siku nyingi wakawapa wenyeviti wa kijiji wapinzani wengi sana Busega licha ya CDM kuwa juu hivi karibu, pia CUF and UDP wako katika hali ya kuwepo na sio goigoi. VIJANA wanaotaka mabadiliko wako wengi, Yuko Meya wa jiji la Mwanza Mabula, ambaye yeye ni wa CCM kitu ambacho kitampa wakati mgumu kuwashawishi wajanja wa nassa wampe jimbo, Yupo Meneja wa Telecentre ya Kwanza Tanzania Bwana LONGO, Yupo Moses Masunga Kijana machachali na mwandishi wa habari mkongwe sasa, wapo vijana wengi ambao kwa kweli nguvu wanazo na CHADEMA sasa iko juu kuliko wakati mwingine BUSEGA, Swali ni je Kamani na Paul Mzindakaya wataweza kuzuia nguvu za vijana wasomi ambao pia wanakubalika na wakazi wa Busega??? CCM BUSEGA BYE BYE.