Ukisikia jiji la mbeya utafikiri bonge la jiji kumbe upuuzi mtupu. Sasa hapa kati nilipata safari ya mbeya nikakwea Fastjet ile kutua kwa kweli uwanja wa Songwe ni mzuri kiasi (pengine kwa sababu ya upya) sasa tukapanda shuttle kwenda mjini 10,000/= (bei ya kulangua) nikafika hoteli ambayo ndio wanaisifia ni classic (Mbeya hotel) duh ni kama nyumba ya makumbush.
Nikamuambia dereva nipeleke nyingine tukaenda Paradise Hotel (nayo ya kipuuzi pia) nikaenda nyingine (GR City) dah ndio nikajua kumbe zile sifa za Wanyakyusa hapo Dar kwao hamna lolote sasa sehemu ya kula ndio ishu yaani labda uende CITY PUB hakuna sehemu nzuri ya kupata varieties.
Poor Mbeya inastahili kuitwa KIJIJI CHA MBEYA si JIJI LA MBEYA mmekalia UCHAWI tu.
Changamkieni fursa ya Mipaka ya KASUMULU & TUNDUMA kufunguka kibiashara.
Cape 2 Cairo Road inayopita Mbeya nayo ni fursa za kiutalii lakini mmekalia kuzugia dini Jumapili mchana, USIKU kama kawa.
=====
Maoni ya wadau
Nikamuambia dereva nipeleke nyingine tukaenda Paradise Hotel (nayo ya kipuuzi pia) nikaenda nyingine (GR City) dah ndio nikajua kumbe zile sifa za Wanyakyusa hapo Dar kwao hamna lolote sasa sehemu ya kula ndio ishu yaani labda uende CITY PUB hakuna sehemu nzuri ya kupata varieties.
Poor Mbeya inastahili kuitwa KIJIJI CHA MBEYA si JIJI LA MBEYA mmekalia UCHAWI tu.
Changamkieni fursa ya Mipaka ya KASUMULU & TUNDUMA kufunguka kibiashara.
Cape 2 Cairo Road inayopita Mbeya nayo ni fursa za kiutalii lakini mmekalia kuzugia dini Jumapili mchana, USIKU kama kawa.
=====
Maoni ya wadau
Unakosea unapojadili utofauti wa miji negatively - inabidi uwe positive. ni kweli wewe ni mgeni mbeya lazima uone tofauti iliyopo na miji kama mwanza kwa mfano. Mambo uliyoyazungumza sikubaliani nayo yote hasa hili la uchawi ambalo tuliache kwanza.
mwanza nayo haikuwa hivi miaka kama 25 iliyopita - hoteli kumbwa sana za kujivunia ilikuwa Mwanza hotel na kidogo lake hotel. Pamba ilikuwa almost ni guest house ya hali ya juu. hizi hotel ndo ziko comaparable na hizi ulizozitaja za mbeya. na wakati wote wawekezaji wakuu wa mwanza wakitoka Bukoba, Musoma, Shinyanga na Tabora - mzee Makinda RIP, baba yake spika Anne, amabaye alikuwa RC wa Tabora enzi hizo (1970s) aliwasihi waarabu na wahindi wa Tabora kwamba wasisahau kuinvest Tabora na kukimbilia Mwanza. hadi sasa kuna wafanya biashara toka Mbeya wame invest Mwanza.
Investment ya juu na haraka kwa Mwanza imekuja baada ya upandikizaji na uvunaji wa Sangara, uvunaji wa madini ya dhahabu Geita, Kahama, Tabora, Mara nk. Angalia Tanga - ulikuwa ndo mji wa pili kwa Dar shauri ya mkonge na wazungu matajiri wakiwa Lushoto etc - lakini baada ya hapo mji umedorora ingawa kwa mbali unarudi tena. Maana yangu hapa ni kuwa unlike Mbeya Mwanza ina utajiri wa maeneo jirani tajiri ambayo yanakwenda kuinvest kule. Ukija kwenye population Wasukuma tu pekee ni wengi kuliko kabila lolote Tanzania na ni matajiri na watumiaji wazuri, acha wana Kagera, Mara etc
Mbeya imejikaza kuwa katika hali hiyo mbele ya policies ambazo zimewatimua wafanya biashara kadhaa ambao wameelekea Dar, Mwanza na kwingineko. Policies za Mbeya kwa wawekezaji ni HARSH = kwa mfano kuna mtu alitaka kujenga 5-star hotel eneo la gymkana kati ya uwanja wa Sokoine na mbeya peak hotel alipigwa vita tena na viongozi wenyeji wa Mbeya - ubovu wa mji wa Mbeya unaletelezwa na aina ya uongozi walionao. watu wamekalia kula pesa - miaka ile world bank ilikuwa na master plan ya kui modernize the notorious Mwanjelwa - hakuna kilichofanyika imebaki ni the best squatter ya Tanzania!!
hii thread yako inafaa isomwe na viongozi wa Mbeya masikio na macho yazibuke.
Kuhusu uchawi sikubaliani nawe - ukitoka mbeya wanasema pwani wana majini. ukifika pwani ya dar wanasema unguja. ukifika unguja wanasema pemba. pemba wanasema tanga etc.