Mjomba Fujo
JF-Expert Member
- Oct 27, 2012
- 2,322
- 5,946
Malalamiko yangu kwaniaba ya wengi, Jiji la Dodoma na askari wenu wa jiji mnatia aibu na fedheha, naomba niweke kisa cha mimi kufungua nyuzi hii, eneo la Makole hospital ilipo jengo jipya kabisa la LAPF likifahamika kama LAPF house kuna barabara ya lami inapita hapo kuunganisha mitaa ya uhindini na DSM road.
Barabara ninayozungumzia ni hiyo yenye mshale wa blue, awali hii ilitumika kuingia na kutoka kwa magari, ila ghafla inaonekana wamebadilisha matumizi kwamba ni njia ya kutoka tu na si kuingia, sasa kichekesho ni kwamba wameweka kabango kadogo kana kwamba si rahisi kuona mabadiliko na kama hujui mabadiliko hayo yatakukuta haya: kuna askari wa jiji wamejazana hapo, watu wasiofahamu mabadiliko hayo wakiingiia kwenye hiyo njia wanavizia wamefika mbele na kuwataka walipe 50,000/=, hivi wanashindwa nini kusimama hapo njiani na kuwaelekeza watu kwamba njia hairuhusiwi kuingia na kungoja watu waingie na kuwakamata, sijui hizi tabia tumetoa wapi za kukomoa au kufanya kutofahamu kwa watu ni mtaji wa mapato, naomba uongozi wa jiji uweke Bango kubwa kabisa na hao askari wafanye kazi ya kuwaelekeza raia na sio kutumia mwanya huo kupata makusanyo ya dhulma.
Barabara ninayozungumzia ni hiyo yenye mshale wa blue, awali hii ilitumika kuingia na kutoka kwa magari, ila ghafla inaonekana wamebadilisha matumizi kwamba ni njia ya kutoka tu na si kuingia, sasa kichekesho ni kwamba wameweka kabango kadogo kana kwamba si rahisi kuona mabadiliko na kama hujui mabadiliko hayo yatakukuta haya: kuna askari wa jiji wamejazana hapo, watu wasiofahamu mabadiliko hayo wakiingiia kwenye hiyo njia wanavizia wamefika mbele na kuwataka walipe 50,000/=, hivi wanashindwa nini kusimama hapo njiani na kuwaelekeza watu kwamba njia hairuhusiwi kuingia na kungoja watu waingie na kuwakamata, sijui hizi tabia tumetoa wapi za kukomoa au kufanya kutofahamu kwa watu ni mtaji wa mapato, naomba uongozi wa jiji uweke Bango kubwa kabisa na hao askari wafanye kazi ya kuwaelekeza raia na sio kutumia mwanya huo kupata makusanyo ya dhulma.