Ni asubuhi Tulivu ya siku ya Jumatatu huku jiji la Dar likiwa katika pilikapilika za kawaida kwa watu wake.Kwa wazungu wanaita Blue Monday.
Kwa upande wa kisiasa ni Jumatatu ya kitofauti kabisa ambapo Maelfu ya vijana wa Chadema wanatarajiwa kulitikisa jiji watakapoelekea ofisi ya Chadema Kinondoni kwa lengo la kumchukulia fomu za kugombea Uenyekiti Freeman Aikael Mbowe ambaye anatizamwa na watanzania kama mwanasiasa jabali wa upinzani asiyenunulika.
Wakizungumza na vyombo mbalimbali vya Habari kwa nyakati tofauti waratibu wa zoezi la kuchangisha fedha za kumchukulia fomu Mwenyekiti huyo anayemaliza muda wake wamekiri taratibu zote zimekamilika.
Mmoja wa waratibu hao Twaha Mwaipaya amesema tayari michango imetimia shilingi milioni moja ambayo ni gharama ya fomu.
Hata hivyo Mwapaiya amesema zoezi la kukusanya michango halitakoma kwani kiasi kitakachozidi atakabidhiwa Mhe Mbowe ili akitumie kwa ajili ya kuwafikia wajumbe kuomba kura.
Mratibu huyo amesema tayari magari yameandaliwa katika majimbo yote ya Dar es Salaam ambapo wanachama wote watakaribishwa kwenda kushuhudia zoezi la kuchukua fomu na kwenda kumkabidhi Mhe Mbowe.
Safari ya kwenda kumchukulia fomu itaanza saa 3 kamili asubuhi hii kutoka majimbo yote kumi ya mkoa wa DSM
Naye Daniel Naftali Ngogo ambaye pia ni mmoja wa waratibu wa vijana katika zoezi hili alisema vijana wanaona kwa sasa Freeman Mbowe ndiye mtu pekee anayeweza kuendelea kuongoza chama hiki.
*Molemo Media* inatarajiwa kutoa Live coverage wakati wa zoezi la kuchukua na kukabidhi fomu kuanzia saa 3 asubuhi.
Kwa upande wa kisiasa ni Jumatatu ya kitofauti kabisa ambapo Maelfu ya vijana wa Chadema wanatarajiwa kulitikisa jiji watakapoelekea ofisi ya Chadema Kinondoni kwa lengo la kumchukulia fomu za kugombea Uenyekiti Freeman Aikael Mbowe ambaye anatizamwa na watanzania kama mwanasiasa jabali wa upinzani asiyenunulika.
Wakizungumza na vyombo mbalimbali vya Habari kwa nyakati tofauti waratibu wa zoezi la kuchangisha fedha za kumchukulia fomu Mwenyekiti huyo anayemaliza muda wake wamekiri taratibu zote zimekamilika.
Mmoja wa waratibu hao Twaha Mwaipaya amesema tayari michango imetimia shilingi milioni moja ambayo ni gharama ya fomu.
Hata hivyo Mwapaiya amesema zoezi la kukusanya michango halitakoma kwani kiasi kitakachozidi atakabidhiwa Mhe Mbowe ili akitumie kwa ajili ya kuwafikia wajumbe kuomba kura.
Mratibu huyo amesema tayari magari yameandaliwa katika majimbo yote ya Dar es Salaam ambapo wanachama wote watakaribishwa kwenda kushuhudia zoezi la kuchukua fomu na kwenda kumkabidhi Mhe Mbowe.
Safari ya kwenda kumchukulia fomu itaanza saa 3 kamili asubuhi hii kutoka majimbo yote kumi ya mkoa wa DSM
Naye Daniel Naftali Ngogo ambaye pia ni mmoja wa waratibu wa vijana katika zoezi hili alisema vijana wanaona kwa sasa Freeman Mbowe ndiye mtu pekee anayeweza kuendelea kuongoza chama hiki.
*Molemo Media* inatarajiwa kutoa Live coverage wakati wa zoezi la kuchukua na kukabidhi fomu kuanzia saa 3 asubuhi.