Kama wewe ni mtumiaji wa hudumu za kutuma na kupokea hela kupitia mitandao yetu ya simu naomba nikutahadharishe kuhusiana na Airtel Money.Nilifungiwa akaunti yangu,nikaambiwa itafunguliwa baada ya masaa 72,baada ya muda huo kupita nikapiga simu na kuambiwa niwe mvumilivu kwani kuna watu akaunti zao zimewahi kufungwa zaidi ya mwezi.Nikawa nimekata tamaa na kuisahau kabisa,jana ambapo ni zaidi ya mwezi nikapiga simu, jibu nililopewa ni kwamba bado inashughulikiwa.Sasa jaribu kufikiria kama ndo umeweka fedha kwenye akaunti yako ambazo unataka kumtumia jamaa yako mwenye hitaji la haraka na kwa sababu zozote zile wakawa wamefunga akaunti yako na ufumbuzi wake haujulikani ndani ya mwezi mzima,je wadhani wanastahili kutoa huduma hiyo?.Hii si kwa yaliyo nitokea mimi tu, hata jamaa zangu wa karibu nimejarbu kuwaeleza hili na kwa bahati mbaya wengine wamekumbana na adha hii.JIHADHARI NA AIRTEL MONEY,maana ukisubiri yakupate wewe waweza hata kutupa sim card yao kabisa.