Jifunze kupitia pythagoras

D Metakelfin

JF-Expert Member
Mar 23, 2017
3,160
3,259
KUNA CHA KUJIFUNZA KWA PYTHAGORAS
Huenda hukusoma sana, lakini ulimaliza darasa la saba. Basi hiyo inatosha. Inatosha sana kwa wewe kukutana na kitu kinaitwa

" Pythagoras theorem"!! Hukumbuki? Je hii a²+b²=c² ushawahi kukutana nayo??! Kama umewahi kukutana nayo, hiyo ndiyo inaitwa “Pythagoras Theorem”.

Mwaka 569 BC, Pythagoras alizaliwa huko Samos, Ugiriki.
Kitu ambacho hukijui ni kuwa Pythagoras hakuwa tu Mathematician, ila alikuwa *Philosopher* mwenye msimamo wa kipekee. Japo Philosophers wengi walijikita katika kutafuta ukweli juu ya "Chimbuko la dunia", Pythagoras hakuwa na muda huo. Yeye aliamini tu kuwa dunia hii inatawaliwa na amani, na "mahusiano ya kihesabu" ndiyo yanayoweza kuelezea vizuri zaidi hii amani.

*Pythagoreans* ndiyo lilikuwa kundi lililoamini imani hii, wakaweka misingi yao "migumu" sana katika kutekeleza imani yao.

Moja kati ya mambo makubwa ni kuwa imani yao ilitawaliwa na usiri wa hali ya juu sana.
PYTHAGORAS alikataa kabisa mafundisho yake yasirekodiwe katika maandishi.
Kuna kitu kimenivutia zaidi kuhusu *PYTHAGORAS*ni pale alipokuwa na miaka 18, alipoamua kufunga safari hadi kwa Mathematician na Philosopher wa zama hizo aliyeitwa THALES, japo kipindi hiki alikuwa mzee sana na hakuwa anaweza tena kufundisha, lakini Pythagoras aliamua kwenda "kupata chochote".

Akafika na kuchota hekima na busara za kutosha sana zilizomjenga na kumfanya kuwa Mathematician mkubwa sana. Kabla THALES hajamkabidhi kwa mwanafunzi wake danistan ambapo hapa Pythagoras alisoma sana.

Hakuna mwenye ushahidi wa [HASHTAG]#proof[/HASHTAG] ya Pythagoras theorem, japo vitabu vingi vilijaribu namna ambazo "huenda" Pythagoras aliprove theorem yake hivyo. Lakini hadi sasa hakuna mwenye "uhakika", ila kwenye [HASHTAG]#RightAngledTriangle[/HASHTAG],
Pythagoras theorem (a²+b²=c²) haijawahi kuongopa.

NILIVYOJIFUNZA

1⃣ Pythagoras aliiona fursa ya kuzaliwa kipindi ambacho *Thales* yupo hai, akaitumia japo Thales alikuwa mzee sana na hakuwa anaweza kufundisha, lakini Pythagoras alipata makubwa sana.

2⃣ Pythagoras aliamua kuwa Philosopher mwenye mawazo tofauti na wenzie wote, lakini bado alikuwa sahihi na akapata kundi kubwa la watu waliomuunga mkono.

3⃣ Pythagoras hakutaka habari zake ziandikwe popote, lakini ziliandikwa na Pythagoras theorem (japo walioandika walimkosea) lakini imeisaidia jamii kiasi kikubwa sana.

4⃣ Pythagoras alizaliwa katika zama ngumu zaidi kimawasiliano lakini aliweza kusimamia alichokiamini na akapata wafuasi wengi sana.

5⃣ Pythagoras hakuridhika tu kuwa Philosopher akaamua kutafuta na taaluma nyingine ya Mathematics na ndiyo huyo mpaka leo tunamtaja.

Sasa turudi kwako wewe..

1. Una fursa ngapi zilizokuzunguka?

2. Una ugumu wowote wa kuwasiliana na mtu yeyote umtakaye duniani?

3. Una watu wangapi wanaofanya vizuri maeneo tofauti tofauti? Umewahi kuwafuata?

4. Umeshashirikishwa kwenye fursa ngapi na ukatoa visingizio?

5. Pythagoras hakutaka kuandikwa, ila dunia ilimbishia ikamwandika, je wewe hujatamani kuandikwa? Umefanya juhudi gani?

6. Unataka kizazi kijacho kikumbuke kwa namna gani??
 
Nimejifunza kitu, lkn nabakinajiuliza ni kwann hasa hakutaka kuandikwa ( mafundisho yake kuandikwa kamasikosei)
 
pia cha kuongezea kuhusu huyo jamaa alikua ana amini katika nadharia ya trans migration of souls yaaani kwamba binadam ni muunganiko wa mwili na roho na pia roho inakua ni mtuwa wa matakwa ya mwili na pia roho hupata uhuru wake pale mwili unapokufa then roho hiyo hua migrated na kupandikizwa katika mwili mwingine kisha maisha yanendelea kuna siku moja alikua na wanafunzi wake akapita sehem moja kisha akaangusha kilio kikubwa baada ya kuulizwa analia nini akasema anakumbuka kua aliwahi kuuwawa katika eneo hilo wakati alivyokua katika mwili wa warrior fulani miaka ya nyuma......
pythagoras ukiachana na mahesabu pia alikua mtaalam wa spiritual trainings hasa mambo yanayohusiana na Ajmi Chakra.
 
Heshima Mkuu, K NI K (Jina lako gumu kdg).

Historia hatuioni lakini tunaisikia, tunaisoma nk.Nayo daima huwa tayari kuzungumza nasi.Wakati mwingine hunongona tu, lakini saa nyingine huzungumza nasi kwa sauti KUBWA.

Ahsante sana kwa kutukumbusha Historia adhimu ya Mwanafalsafa Pythagoras.Hii theorem si option katika maendeleo ya kila siku ya mwanadamu, Ni sharti ifanyiwe kazi ili iumbike ndani yetu.

Ahsante kwa kuniongezea jambo.
 
Nimejifunza kitu, lkn nabakinajiuliza ni kwann hasa hakutaka kuandikwa ( mafundisho yake kuandikwa kamasikosei)
Heshima Mkuu, mzado .

Great thinkers walikuwa watata sana.Kuanzia kina Thales, Socrate, Aristotle, Plato, Anaximander, Seneca, Epictetus, Epicurus nk.

Walikuwa wabishi.Si huu ubishi wa kina sie holoi poloi.Walibisha kwa Kutumia Mantiki, utashi na ubora wa Mazungumzo.Socrate alikuwa mbishi, Gallileo alikuwa mbishi.

Ubishi, Utata ya Maisha ya hawa Great Thinkers ndiyo uliowafanya kuwa wa kipekee hadi leo.Hivyo ulivyouliza ni kwanini Pythagoras hakutaka maandishi yake yaandikwe basi ni muendelezo tu wa Huu ubishi wao wa kutumia mantiki na si ushabiki.Ipo sababu ya msingi sana.

Kutakuwa na hoja za msingi (Kutoandikwa kwa Mafundisho yake) ila binafsi sifahamu ni kwanini.Ngoja tuwasubiri wajuzi watujuze zaidi.
 
Heshima Mkuu, mzado .

Great thinkers walikuwa watata sana.Kuanzia kina Thales, Socrate, Aristotle, Plato, Anaximander, Seneca, Epictetus, Epicurus nk.

Walikuwa wabishi.Si huu ubishi wa kina sie holoi poloi.Walibisha kwa Kutumia Mantiki, utashi na ubora wa Mazungumzo.Socrate alikuwa mbishi, Gallileo alikuwa mbishi.

Ubishi, Utata ya Maisha ya hawa Great Thinkers ndiyo uliowafanya kuwa wa kipekee hadi leo.Hivyo ulivyouliza ni kwanini Pythagoras hakutaka maandishi yake yaandikwe basi ni muendelezo tu wa Huu ubishi wao wa kutumia mantiki na si ushabiki.Ipo sababu ya msingi sana.

Kutakuwa na hoja za msingi (Kutoandikwa kwa Mafundisho yake) ila binafsi sifahamu ni kwanini.Ngoja tuwasubiri wajuzi watujuze zaidi.
Sawasawa mkuu Dahafrazeril nadhani nimekuelewa vema
 
Mi najihisi mchawi sasa vipaji vya shetani ni hatar ila nashukuru this gene of wizardism is recessive and not dorminant thus not expressed
 
Kwa nyakati tulizopo Watu wanaofikiri kwa Namna km hii ni Wachache SANA,.
Pengine tujifunze pia ni kipi haswa kilikua kinawasukuma wao Kuwa na ufikiri Mkubwa Kiasi HIKI?.
 
Jamaaa una akili vizuri na mada zako ziko poa ila tatizo ni jina unalotumia K NI K duh sisi wachungaji litakwaza kidogo
 
Mkuu umenikumbusha harakati na hekaheka za Mwana FALISAFA (Philosophy) mmoja katika nchi ya TANZANIA....

Huyu mtu alipambana VITA kipindi hicho na WAKOLONI wenye Silaha za MOTO...

Alikwenda/Aliingia Vitani akiwa na Askari wake WATIIFU aliowajaza HARI na IMANI wakiamini RISASI za MOTO zingekeuka Maji...

Katika VITA hiyo walikufa WAAMINI/WATIIFU wengi, na ilipo fikia kukamatwa kwake MWANA FALISAFA huyu....

Alichukua hatua ambayo baada ya yeye MAJESHI mengi ULIMWENGUNI yaliiga/yalifuata KITENDO chake kama sehemu ya MAFUNZO katika MEDANI YA VITA....

Huyu mtu ALIJICHUKULIA uhai wake.
Namaanisha ALIJILIPUA kwa RISASI kabla ya kukamatwa na ADUI...

Naomba nikumbushwe kati ya MIRAMBO...na KINJEKETILE...

Amani itawale katika VIFO vyao..
 
Back
Top Bottom