Jifunze basic za python

Jifunze basic za python

Terence Tao

Member
Joined
Jul 22, 2025
Posts
6
Reaction score
4
Katika Advancement ya AI zikiwepo Grok, Gemini, Chat Gpt, Deepseek, muhimu sana kujifunza programming maana unaweza kuletewa program ambazo hujui maana yake ukaenda kutengeneza kitu ambacho kikileta shida unashindwa kuelewa namna ya kutatua . Muhimu tujifunze programming ili ziturahisishie kwenye kazi zetu.


Leo tutajifunza kuhusu

Comment
Data type
Operators in python
If statement
Loops
Lists
Dictionaries
Function



Python ni programming language ambayo inatumika kufanya vitu vifuatavyo
-kutengeneza website, inatumika katika Data Science and Data Analysis (Numpy , Pandas), Machine Learning and Artificial Intelligence , Desktop GUI Application ( Tkinter, PyQt ) , Game Development ( PyGame ), Computer vision and Image processing , Internet of Things n.k

Unaposave file lako andika jina unalotaka mwisho unaweka .py, unatakiwa uinstall python kwenye pc yako pia unaweza kutumia VS code kurun python au kama hutaki waweza kutumia online software mfano Replit , Google Colab ukaandika program zako huko na kuzirun n.k

[COLOR=rgb(184, 49, 47)]Comment katika python[/COLOR]

Haya ni maneno ambayo ukiandika hayafinyiwi kazi katika program yako , Yawepo au yasiwepo hamna chochote kinachotokea . Ili umuhimu wake inamsaidia anayeandika program kuelezea Zaidi kuhusu code anazokuwa anaandika. Na pia atakayekuja kuzisoma hizo code ataelewa maana ya code zako.

Comment katika tunakuwa tunatumia alama ya # mwazoni mwa code yako . Baada ya # hata kama mbele ukiandika kikabila haina shida yoyote. kila ukianza mstari mwingine usisahau kutumia #


Data type .


-Data katika python zipo katika makundi mbali mbali ambazo ni

namba nzima tunaziita integers mfano 10, 30 ,56, 178 ,976 , -87 n.k
herufi tunaziita Characters mfano ‘a’ , ‘b’ , ‘c’ ,’d’ n.k
Kuna String ambazo hii ni muunganika wa Characters mfano “mkoa”, “chama”, “wanyama” n.k
desimali tunaziita decimal numbers au float au double mfano ni 4.5, 34.98, 837.86 n.k.
Boolean Type inakuwa ina dhamani mbili ya “True” au “False”
Zingine ni lists , dictionaries ambazo tutaiona Leo . n.k



UZURI MMOJA WAPO WA PYTHON HAUNA HAJA YA KUSEMA DATA TYPE NI IPI .


VARIABLE IN PYTHON

Data type ambazo tumezisema zinakuwa zinatunzwa ndani ya Variable. Mfano tulivyokuwa primary tulikuwa tuna let dhamani ya x=7, hapa x inakuwa ni variable inabeba dhamani ya 7. Tukiwa tunatumia string au charater Tunaweka Single Quote ( hii alama ' ') au Double quotes( hii alama " " ) ni wewe mwenyewe utakavyo amaua .

Code examples

x=10
miaka=40
mkoa=”dar”
distance=90.98
score=’A’

hapa x, miaka , mkoa , distance , score ni variable

NOTE:
Kwenye hizo code hapo juu hatuja sema aina za data ambazo tunakuwa tunadili nazo .

Ukitaka uonyeshe maneno kwenye Screen katika python

Ukitaka uone data zako au maneno yaonekane katika screen kwa python unakuwa unatumia neno print ikifatiwa na mabano .Hili ni neno ambalo tutalitumia sana katika python.
print()

Getting value from the user

Swali: Nawezakaje kuchukua data kutoka katika mtumiaje wa program yangu?

Majibu.
Ili tuchukue data kutoka kwa mtumiaji wa program tunakuwa tunatumia neno input() , ndani ya mabano tunaweza kuweka ujumbe ambao mtu atakuwa anauona pindi atakapo kuwa anatumia program .



Code
>>input(“ weka umri wako”)

Maelezo:

Mtumiaji akiweka umri wake tunaweza kuutunza huo umri kwenye variable mfano miaka . Na code ikabadilika na kuwa .

Code
>>miaka=input(“weka umri wako ”)



Swali :
Nataka variable yangu ambayo ni miaka iwe ni string au integers kwasababu kuna muda nataka niitumie kama namba na kuna muda nataka niitumie pamoja na maneno mengine

Maelezo
Ukitaka utumia variable miaka kama namba au integer ili uweze kufanya operation zingine inakuhitaji uweke neno int mwanzo wa neno input, au kama unataka miaka iwe ni string utaweka neno str kabla ya neno input.


Code
>>miaka= int(input(“ weka umri wako”))

Or
Code
>>miaka =str(input(“ weka umri wako”))

Operators in python.
Tukitaka kufanya mahesabu kama vile kujumlisha, kutoa , kugawanya , kuzidisha , . Tunakuwa tunatumia Arithmetic Operators.
Arithmetic operators +, -, *, /, %


Tukitaka kuangalia kama data ni kubwa kwa “ greater than” dhamani flani, au ndogo “ less than” , au “greater or equal to” au “less or equal to” ,au data flani ni sawa sawa na data nyingine .Tunakuwa tunatumia Relational Operator

Relational Operator<, >, <=, >=,= =, ! =


Kuna Logical operator
Hii tunaitumia sana kuangalia logic za data .
Logical operatorAND, OR, NOT


Kuna Assignment operator

Assignment operator=, +=, -=, *=, %=

Kama tunataka variable mshahara iwe ni mshahara wako tunaandika
Code:
>mshahara=300000
Maelezo:
Tukiprint mshahara tutapata 300000, tukitaka kuongeza mshahara kwa kiasi cha 20,000
Tunaandika.
code
>>mshahara=mshahara+20000
au
>> mshahara+=20000

>>print(mshahara)
Output
320000


Maelezo

Tukitaka kupunguza mshahara kwa kiasi cha 20000 basi tutaandika

Code
>>mshahara-=20000 au
>>mshahara= mshahara-20000

If Statement in python



If statement ni moja kati ya program ya muhimu sana , Maisha yetu asilimia kubwa tunaishi na if statement , Mfano Kama ikifika mwakani ntanunua kiwanja, kama nikifikisha miaka kadhaa ntaacha kufanya kazi Fulani, Kama nikiwa na elfu moja ntapata MB kadhaa , kama nikiwa na hela kadhaa ntafanya jambo fulani , N.k. vyote hivo vipo ndani ya if statement . Unaweza kuwa na machaguzi Zaidi ya moja .

Chini ya if statement na elif tukuwa tunafanaya indentation , tuacha nafasi kwenye lines zinazofuata chini. Au unabonyeza tab kwenye pc yako

Namna tunavyoandika if statement au syntax yake:

if ------:
#your Code

elif ------:
#yourCode

elif------:
#yourCode

else:

#yourCode



Mfano 1:


Unachukua umri wa mtu na kudisplay either anaruhusiwa kuendelea mbele na au haruhisiwi kutokana na umri wake

Simple Code:

print(“ karibu katika mfumo wetu”)
miaka=int(input(“ weka miaka yako”))

if miaka>=18:
print(“unaruhisiwa kuendelea mbele”)
else:
Print(“ umri wako bado”)
1753265606327.png




Mfano 2:

Kuchagua kifurushi cha siku au wiki au mwezi
1753265758758.png



Loop in python
Loop inatumika kurun code mara kadhaa. Tukitaka kuonyesha vitu mara kadhaa tunakuwa tunatumia loop. Mfano unapoenda kutoa pesa bank , ATM inavyohesabu hela mara kadhaa ile ni Loop, Saa inapokuwa inaccount seconds , minutes n.k hiyo ni Loop. Mwalimu anapokuwa anahesabu idadi ya wanafunzi wake hiyo ni Loop. Unapokuwa unaangalia video kadhaa kwenye mitandao ya kijamii hiyo ni loop N.k.

Kuna while loop , for Loop katika python

While loop

Syntax yake

While conditions:
#code




Note,


Baadaya ya neno while loop na condictions kunakuwa na vidoti viwili.
Chini ya while loop tunafanya indentation kwa maana tunaacha nafasi au unaweza kubonyeza tap. Lakini mara nyingi inakuwa automatic tu.

Mfano 1:
Tunataka kuonyesha namba kuanzia namba 1 mpaka 10 , Cha kwanza lazima tuwe na variable au “neno” ambalo litatunza namba moja ( Code: namba=1) , baada ya hapo tutakuwa na condition kuangalia kama namba yetu haijazidi kumi (Code : while namba<=10: ) , then tutakuwa tunaongeza dhamani ya namba kwa moja ( moja+=1)

Mfano wa Code:
1753266055209.png

Kwenye mfano wa hapo juu tuweza kuamua kuruka namba zionekane 1, 4 ,7, 10 . kinachobadilika ni kwenye namba+=1 tunaweka namba+=3

Simple Code:
1753266160765.png



  • Tunaweza kutumia if statement ndani ya while Loop . Kwa mfano tunataka kudisplay even numbers . Even numbers ni namba zinazokawanyika kwa mbili pasina ya baki. ( code yake inakuwa: namba%2= =0) . Modulus (%) inakuwa inaangalia baki . sawa sawa mbili inakuwa na maana ya je baada ya kugawanya baki inakuwa sawa sawa na 0 . Ikiwa ni kweli basi code za chini yake zinafanyiwa kazi .
    1753266332881.png

Break statement

B
reak statement inatumika endapo tunataka loop yetu iishie sehemu flani .

Mfano 3
Kudisplay number 1 mpaka 10 lakini ikifika namba saba program isiendelee.

Njia
Tunaweka inavalue ya mwanzo kuwa moja ( number=1), Tunaweka value ya mwisho ndani ya while loop ( while<=10) , baada ya hapo tunasema ikifika number 7 program isiendelee ( if number==7 break) , tunakuwa tunaruka number yetu kwa dhamani ya moja (number+=1)


Simple code
1753266486990.png


Mfano 4:
Kumuomba user aweke neno la sili asipo weka “password123” isimruhusu kuendelea mbele.

Simple code .
1753266549347.png


FOR LOOP


For statement.
Tunaweza kuwa na list ya vitu , Mfano List ya magari, majina ya watu, List ya matunda , List ya mikoa . Tunaweza kutumia for Loop kuonyesha list zote .



Mfano 1:
List ya mikoa kwa mfano Dar , Mbeya, Arusha , Dodoma, Tanga, Mwanza . ( Code: mikoa = [ ‘Dar’, ‘Mbeya’, ‘Arusha’,’Dodoma’,’Mwanza’] ) hapa tunakuwa tumetengeneza list teyali, Sasa tunatumia for loop kuonyesha mikoa yote ( Code: for x in mikoa: ) , x inakuwa inachukua mkoa moja baada ya mwingine ,x=’Dar’ next x=’Mbeya’ next x=’Arusha’ n.k. mpaka list zote ziishe alafu tunaweza kuzionyesha (Code : print(x) )



Simple code
1753266670137.png



Mfano 2:
Tunaweza kutumia for loop ndani yake pia tukaweka for loop ,Tunakuwa tunaita nested loop.

-unaweza kuwa na aina za simu Samsung,Iphone, Pixel ( Code: simu= [‘Samsung’, ‘Iphone’, ‘pixel’] tukawa na mikoa tuliyoiona juu ,mikoa kwa mfano Dar , Mbeya, Arusha , Dodoma, Tanga, Mwanza . ( Code: mikoa = [ ‘Dar’, ‘Mbeya’, ‘Arusha’,’Dodoma’,’Mwanza’] ). Sasa tunaweza kudisplay kila mkoa ukaonyesha aina za simu zinazopatikana. (Code: for x in mikoa: ) ikafuatia for loop nyingine ( Code: for y in simu: ) baada ya hapo tukadisplay mikoa ikafuata aina za simu

Simple code

1753266774595.png


Mfano 3

Kuunganisha pamoja for loop na if statement .

Kutengeneza list ya namba (Code: namba=[1,2,3,4,5,6,7,8] ) , katika hizi number tutazidisplay kwa kutumia for loop ( Code : for x in namba) baada ya hapo tutaangalia kama number inagawanyika kwa 2 ( Code : if x%2 == 0 ) , tutaonyesha kuwa hiyo number ni even number

Simple Code
1753266883428.png


Mfano 4:

Kudisplay numbers 1 to 9 kwa kutumia range()
1753266946436.png



Lists
Inakuwa na mchanganyiko wa namba, maneno , vitu mbali mbali kama object. Tunaweza kuongeza vitu ndani ya List , tunaweza kufuta vitu ndani ya list , tunaweza kucount idadi ya vitu ndani ya List.
Mfano .

List ya nchi , ( Code: nchi=[“Tanzania”,”Kenya”,”Uganda”]) , tukitaka kuziona tunaandika( code: print(nchi))
Simple code
1753267142391.png


Tukitakana kuziona kwa kutumia for loop , ( code: for x in nchi) baada ya hapo tunazidisplay
1753267183877.png



Tukitaka kuongeza mfano nchi nyingine tunakuwa tunatumia neno append ( code: nchi.append(“Uganda”). Hii tunakuwe tunaweka neno moja tu ndani yake
1753267228685.png





nchi=[“Tanzania”,”Kenya”,”Uganda”]
OperationMaelezoMajibu
nchi.append(“Rwanda”)Inaongeza nchi ya Rwanda kwenye listprint(nchi)

['Tanzania', 'Kenya', 'Uganda', 'Rwanda']
nchi.clear()Inafuta kila kitu kilichopo kwenye list za nchiprint(nchi)
[]
nchi.sort()Inapanga list kutokana na alphabetical orderprint(nchi)
['Kenya', 'Tanzania', 'Uganda']
nchi.reverse()Cha mwisho kwenye list kinakuwa cha kwanza na cha kwanza kinakuwa cha mwishoprint(nchi)
['Uganda', 'Kenya', 'Tanzania']
nchi.pop()Inaondona dhamani ya mwisho kwenye listprint(nchi)
['Tanzania', 'Kenya']


Itaendelea...
 

Attachments

  • 1753266833501.png
    1753266833501.png
    22.6 KB · Views: 22
Katika Advancement ya AI zikiwepo Grok, Gemini, Chat Gpt, Deepseek, muhimu sana kujifunza programming maana unaweza kuletewa program ambazo hujui maana yake ukaenda kutengeneza kitu ambacho kikileta shida unashindwa kuelewa namna ya kutatua . Muhimu tujifunze programming ili ziturahisishie kwenye kazi zetu.


Leo tutajifunza kuhusu

Comment
Data type
Operators in python
If statement
Loops
Lists
Dictionaries
Function



Python ni programming language ambayo inatumika kufanya vitu vifuatavyo
-kutengeneza website, inatumika katika Data Science and Data Analysis (Numpy , Pandas), Machine Learning and Artificial Intelligence , Desktop GUI Application ( Tkinter, PyQt ) , Game Development ( PyGame ), Computer vision and Image processing , Internet of Things n.k

Unaposave file lako andika jina unalotaka mwisho unaweka .py, unatakiwa uinstall python kwenye pc yako pia unaweza kutumia VS code kurun python au kama hutaki waweza kutumia online software mfano Replit , Google Colab ukaandika program zako huko na kuzirun n.k

[COLOR=rgb(184, 49, 47)]Comment katika python[/COLOR]

Haya ni maneno ambayo ukiandika hayafinyiwi kazi katika program yako , Yawepo au yasiwepo hamna chochote kinachotokea . Ili umuhimu wake inamsaidia anayeandika program kuelezea Zaidi kuhusu code anazokuwa anaandika. Na pia atakayekuja kuzisoma hizo code ataelewa maana ya code zako.

Comment katika tunakuwa tunatumia alama ya # mwazoni mwa code yako . Baada ya # hata kama mbele ukiandika kikabila haina shida yoyote. kila ukianza mstari mwingine usisahau kutumia #


Data type .


-Data katika python zipo katika makundi mbali mbali ambazo ni

namba nzima tunaziita integers mfano 10, 30 ,56, 178 ,976 , -87 n.k
herufi tunaziita Characters mfano ‘a’ , ‘b’ , ‘c’ ,’d’ n.k
Kuna String ambazo hii ni muunganika wa Characters mfano “mkoa”, “chama”, “wanyama” n.k
desimali tunaziita decimal numbers au float au double mfano ni 4.5, 34.98, 837.86 n.k.
Boolean Type inakuwa ina dhamani mbili ya “True” au “False”
Zingine ni lists , dictionaries ambazo tutaiona Leo . n.k



UZURI MMOJA WAPO WA PYTHON HAUNA HAJA YA KUSEMA DATA TYPE NI IPI .


VARIABLE IN PYTHON

Data type ambazo tumezisema zinakuwa zinatunzwa ndani ya Variable. Mfano tulivyokuwa primary tulikuwa tuna let dhamani ya x=7, hapa x inakuwa ni variable inabeba dhamani ya 7. Tukiwa tunatumia string au charater Tunaweka Single Quote ( hii alama ' ') au Double quotes( hii alama " " ) ni wewe mwenyewe utakavyo amaua .

Code examples

x=10
miaka=40
mkoa=”dar”
distance=90.98
score=’A’

hapa x, miaka , mkoa , distance , score ni variable

NOTE:
Kwenye hizo code hapo juu hatuja sema aina za data ambazo tunakuwa tunadili nazo .

Ukitaka uonyeshe maneno kwenye Screen katika python

Ukitaka uone data zako au maneno yaonekane katika screen kwa python unakuwa unatumia neno print ikifatiwa na mabano .Hili ni neno ambalo tutalitumia sana katika python.
print()

Getting value from the user

Swali: Nawezakaje kuchukua data kutoka katika mtumiaje wa program yangu?

Majibu.
Ili tuchukue data kutoka kwa mtumiaji wa program tunakuwa tunatumia neno input() , ndani ya mabano tunaweza kuweka ujumbe ambao mtu atakuwa anauona pindi atakapo kuwa anatumia program .



Code



Maelezo:
Mtumiaji akiweka umri wake tunaweza kuutunza huo umri kwenye variable mfano miaka . Na code ikabadilika na kuwa .

Code




Swali :
Nataka variable yangu ambayo ni miaka iwe ni string au integers kwasababu kuna muda nataka niitumie kama namba na kuna muda nataka niitumie pamoja na maneno mengine

Maelezo
Ukitaka utumia variable miaka kama namba au integer ili uweze kufanya operation zingine inakuhitaji uweke neno int mwanzo wa neno input, au kama unataka miaka iwe ni string utaweka neno str kabla ya neno input.


Code


Or
Code


Operators in python.
Tukitaka kufanya mahesabu kama vile kujumlisha, kutoa , kugawanya , kuzidisha , . Tunakuwa tunatumia Arithmetic Operators.
Arithmetic operators +, -, *, /, %


Tukitaka kuangalia kama data ni kubwa kwa “ greater than” dhamani flani, au ndogo “ less than” , au “greater or equal to” au “less or equal to” ,au data flani ni sawa sawa na data nyingine .Tunakuwa tunatumia Relational Operator

Relational Operator<, >, <=, >=,= =, ! =


Kuna Logical operator
Hii tunaitumia sana kuangalia logic za data .
Logical operatorAND, OR, NOT


Kuna Assignment operator

Assignment operator=, +=, -=, *=, %=

Kama tunataka variable mshahara iwe ni mshahara wako tunaandika
Code:

Maelezo:

Tukiprint mshahara tutapata 300000, tukitaka kuongeza mshahara kwa kiasi cha 20,000
Tunaandika.
code

au



Output
320000


Maelezo

Tukitaka kupunguza mshahara kwa kiasi cha 20000 basi tutaandika

Code


If Statement in python



If statement ni moja kati ya program ya muhimu sana , Maisha yetu asilimia kubwa tunaishi na if statement , Mfano Kama ikifika mwakani ntanunua kiwanja, kama nikifikisha miaka kadhaa ntaacha kufanya kazi Fulani, Kama nikiwa na elfu moja ntapata MB kadhaa , kama nikiwa na hela kadhaa ntafanya jambo fulani , N.k. vyote hivo vipo ndani ya if statement . Unaweza kuwa na machaguzi Zaidi ya moja .

Chini ya if statement na elif tukuwa tunafanaya indentation , tuacha nafasi kwenye lines zinazofuata chini. Au unabonyeza tab kwenye pc yako

Namna tunavyoandika if statement au syntax yake:

if ------:
#your Code

elif ------:
#yourCode

elif------:
#yourCode

else:

#yourCode



Mfano 1:


Unachukua umri wa mtu na kudisplay either anaruhusiwa kuendelea mbele na au haruhisiwi kutokana na umri wake

Simple Code:

print(“ karibu katika mfumo wetu”)
miaka=int(input(“ weka miaka yako”))

if miaka>=18:
print(“unaruhisiwa kuendelea mbele”)
else:
Print(“ umri wako bado”)
View attachment 3415656



Mfano 2:

Kuchagua kifurushi cha siku au wiki au mwezi
View attachment 3415659


Loop in python
Loop inatumika kurun code mara kadhaa. Tukitaka kuonyesha vitu mara kadhaa tunakuwa tunatumia loop. Mfano unapoenda kutoa pesa bank , ATM inavyohesabu hela mara kadhaa ile ni Loop, Saa inapokuwa inaccount seconds , minutes n.k hiyo ni Loop. Mwalimu anapokuwa anahesabu idadi ya wanafunzi wake hiyo ni Loop. Unapokuwa unaangalia video kadhaa kwenye mitandao ya kijamii hiyo ni loop N.k.

Kuna while loop , for Loop katika python

While loop

Syntax yake

While conditions:
#code




Note,

Baadaya ya neno while loop na condictions kunakuwa na vidoti viwili.
Chini ya while loop tunafanya indentation kwa maana tunaacha nafasi au unaweza kubonyeza tap. Lakini mara nyingi inakuwa automatic tu.

Mfano 1:
Tunataka kuonyesha namba kuanzia namba 1 mpaka 10 , Cha kwanza lazima tuwe na variable au “neno” ambalo litatunza namba moja ( Code: namba=1) , baada ya hapo tutakuwa na condition kuangalia kama namba yetu haijazidi kumi (Code : while namba<=10: ) , then tutakuwa tunaongeza dhamani ya namba kwa moja ( moja+=1)

Mfano wa Code:
View attachment 3415663

Kwenye mfano wa hapo juu tuweza kuamua kuruka namba zionekane 1, 4 ,7, 10 . kinachobadilika ni kwenye namba+=1 tunaweka namba+=3

Simple Code:
View attachment 3415664


  • Tunaweza kutumia if statement ndani ya while Loop . Kwa mfano tunataka kudisplay even numbers . Even numbers ni namba zinazokawanyika kwa mbili pasina ya baki. ( code yake inakuwa: namba%2= =0) . Modulus (%) inakuwa inaangalia baki . sawa sawa mbili inakuwa na maana ya je baada ya kugawanya baki inakuwa sawa sawa na 0 . Ikiwa ni kweli basi code za chini yake zinafanyiwa kazi .View attachment 3415667

Break statement

B
reak statement inatumika endapo tunataka loop yetu iishie sehemu flani .

Mfano 3
Kudisplay number 1 mpaka 10 lakini ikifika namba saba program isiendelee.

Njia
Tunaweka inavalue ya mwanzo kuwa moja ( number=1), Tunaweka value ya mwisho ndani ya while loop ( while<=10) , baada ya hapo tunasema ikifika number 7 program isiendelee ( if number==7 break) , tunakuwa tunaruka number yetu kwa dhamani ya moja (number+=1)


Simple code
View attachment 3415668

Mfano 4:
Kumuomba user aweke neno la sili asipo weka “password123” isimruhusu kuendelea mbele.

Simple code .
View attachment 3415671

FOR LOOP


For statement.
Tunaweza kuwa na list ya vitu , Mfano List ya magari, majina ya watu, List ya matunda , List ya mikoa . Tunaweza kutumia for Loop kuonyesha list zote .



Mfano 1:
List ya mikoa kwa mfano Dar , Mbeya, Arusha , Dodoma, Tanga, Mwanza . ( Code: mikoa = [ ‘Dar’, ‘Mbeya’, ‘Arusha’,’Dodoma’,’Mwanza’] ) hapa tunakuwa tumetengeneza list teyali, Sasa tunatumia for loop kuonyesha mikoa yote ( Code: for x in mikoa: ) , x inakuwa inachukua mkoa moja baada ya mwingine ,x=’Dar’ next x=’Mbeya’ next x=’Arusha’ n.k. mpaka list zote ziishe alafu tunaweza kuzionyesha (Code : print(x) )



Simple code
View attachment 3415677


Mfano 2:
Tunaweza kutumia for loop ndani yake pia tukaweka for loop ,Tunakuwa tunaita nested loop.

-unaweza kuwa na aina za simu Samsung,Iphone, Pixel ( Code: simu= [‘Samsung’, ‘Iphone’, ‘pixel’] tukawa na mikoa tuliyoiona juu ,mikoa kwa mfano Dar , Mbeya, Arusha , Dodoma, Tanga, Mwanza . ( Code: mikoa = [ ‘Dar’, ‘Mbeya’, ‘Arusha’,’Dodoma’,’Mwanza’] ). Sasa tunaweza kudisplay kila mkoa ukaonyesha aina za simu zinazopatikana. (Code: for x in mikoa: ) ikafuatia for loop nyingine ( Code: for y in simu: ) baada ya hapo tukadisplay mikoa ikafuata aina za simu

Simple code

View attachment 3415678

Mfano 3

Kuunganisha pamoja for loop na if statement .

Kutengeneza list ya namba (Code: namba=[1,2,3,4,5,6,7,8] ) , katika hizi number tutazidisplay kwa kutumia for loop ( Code : for x in namba) baada ya hapo tutaangalia kama number inagawanyika kwa 2 ( Code : if x%2 == 0 ) , tutaonyesha kuwa hiyo number ni even number

Simple Code
View attachment 3415680

Mfano 4:

Kudisplay numbers 1 to 9 kwa kutumia range()
View attachment 3415682


Lists
Inakuwa na mchanganyiko wa namba, maneno , vitu mbali mbali kama object. Tunaweza kuongeza vitu ndani ya List , tunaweza kufuta vitu ndani ya list , tunaweza kucount idadi ya vitu ndani ya List.
Mfano .

List ya nchi , ( Code: nchi=[“Tanzania”,”Kenya”,”Uganda”]) , tukitaka kuziona tunaandika( code: print(nchi))
Simple code
View attachment 3415684

Tukitakana kuziona kwa kutumia for loop , ( code: for x in nchi) baada ya hapo tunazidisplay
View attachment 3415685


Tukitaka kuongeza mfano nchi nyingine tunakuwa tunatumia neno append ( code: nchi.append(“Uganda”). Hii tunakuwe tunaweka neno moja tu ndani yake
View attachment 3415686




nchi=[“Tanzania”,”Kenya”,”Uganda”]
OperationMaelezoMajibu
nchi.append(“Rwanda”)Inaongeza nchi ya Rwanda kwenye listprint(nchi)

['Tanzania', 'Kenya', 'Uganda', 'Rwanda']
nchi.clear()Inafuta kila kitu kilichopo kwenye list za nchiprint(nchi)
[]
nchi.sort()Inapanga list kutokana na alphabetical orderprint(nchi)
['Kenya', 'Tanzania', 'Uganda']
nchi.reverse()Cha mwisho kwenye list kinakuwa cha kwanza na cha kwanza kinakuwa cha mwishoprint(nchi)
['Uganda', 'Kenya', 'Tanzania']
nchi.pop()Inaondona dhamani ya mwisho kwenye listprint(nchi)
['Tanzania', 'Kenya']


Itaendelea...
Terrence Tao teh teh teh
 
Function in Python

Function ni kundi la codes ambazo zinafanya task flani.

-unaweza kuwa code ambazo zinakuwa zinafanya kazi ya kujumlisha, unaweza kuwa na code zinazoandika ujumbe kwa watu wengi kwa wakati mmoja mfano kuandika barua moja yenye taarifa tofauti za majina ya watu , namba za simu , kazi mtu anayofanya tunatumia function, ili kuto kuandika code mara nyingi tunatumia function .

Function ni moja kati ya sehemu kubwa sana katika programming.

Tuchukulie umeandika code zinazofanana mara 50 lakini baadae ukaja kujua kuna sehemu umekosea kwenye code zako .Unatakiwa ukabadilishe hizo sehemu zote ulizokosea ,hapo unakuwa teyali umeshapoteza muda ili kuepusha hilo jambo tunakuwa tunatumia functions.



Mfano tunaweza kuwa na mtu X anafanya kazi ya kujumlisha namba mbili, Kwahiyo tukimpa namba mbili au Zaidi anazijumlisha anatupa jibu, Na atajulisha tu endapo tutamuita ,asipo itwa hafanyi chochote , Kwahiyo tukisema mtu X namba 2 na 4 anajibu 6. Tukisema mtu X 6 na 8 anajibu 14. Tunaweza kumuita mara nyingi kadiri tuwezavyo .Hivyo ndivyo namna function inavyokuwa. Tunaweka task flani ndani ya function na baadae tunaiita .
Function Syntax.

Namna function inavyokuwa tunaanza na neno def ikifuatiwa na jina la function baada yapo tunafunga mabano . Ndani ya mabano unaweza kuandika( kinachoandikwa ndani ya mabano tunakiita argument) au unaweza usiandike chochote.

Syntax.

def jinalaFunction():
#code

Au

def jinaLaFunction(argument):
#code



Mfano 1:
Kutengeneza function itakuwa na jina la jamiiForum ambayo tukiita neno Where we Dare to talk openly tunali display.

Simple Code

1753339545069.png


Mfano 2:

Kuchukua jina la mtumiaji wa mfumo
Maelezo

Kwanza tutatengeneza function inayoitwa salamu , ndani yake tutachukua taarifa ya jina ( Code : salamu(jina): ) , then tutaonyesha kwa kutumia print taarifa za jina lake ( Code: print( f “ jina lako ni , {jina} ” ) , hapa “jina lako ni” ni maneno tu ambayo unaweza kuweka na pia unaweza kuweka chochote . {jina} ni variable au dhamani tunaichukua kwa mtumia kupitia input function ( Code : jina=input(“ Karibu katika huduma yetu, Jina lako ni nani “ ) then tunaiita function salamu kwa kuiipa Argument jina ( Code: salamu(jina) )
1753339832778.png


Mfano 4:

Tunaweza kutengeneza function ya kuzidisha namba mbili. Function itakuwa inapokea namba mbili na kuzizidisha pamoja ( Code: zidisha(namba1,namba2) ). Baada ya hapo function itarudisha majibu ya namba mbili ( Code: return namba1*namba2 )

Simple Code.
1753339919456.png

Tunaweza kutengeneza multiplication table
1753339971231.png


Simple questions of Functions na majibu yake

1:Tengeneza function ya kutafuta namba kubwa kati ya namba mbili .
2.Andika function ambayo itachukua jina la kwanza, mkoa mtu alipozaliwa , umri na kuzionyesha hizo taarifa.
3.Andika program ya kubadilisha maneno kwenda yatakayo andikwa kwa herufu ndogo na mtumiaje kwenda herufi kubwa

Jibu
1
1753340087798.png


2
1753340125459.png



3.
1753340147176.png
 
Dictionary
Dictionary katika python tunaitumia ili kutunza taarifa.
Ili kuweza kusoma taarifa ya tulichokuwa tumekitunza katika dictionary tunakuwa tunatumia key ukilinganisha na List ambapo tunatumia nafasi ya data .Mfano mzuri

( Code : membersWaJamiiForum={ ‘x1’:’ni member wa kwanza wa Jamii Forum’, ‘x2’:’ni member wa pili wa jamii Forum’,’x3’: ‘ni member wa tatu wa jamii Forum’} )

Kwenye hii code x1 , x2, na x3 tunakuwa tunaziita keys ndo zinakuwa zimebeba taarifa husika za data zetu . Ili kupata taarifa za x1 tunakuwa tunandika (Code: membersWaJamiiForum[‘x1’] ) na pia inakuwa sawa kwa x2
au
( Code : membersWaJamiiForum={ ‘age’:45, ‘sex’:’male’,’kazi’: ‘mkulima’} ) , hapa age , sex na kazi tunakuwa tunaziita ni keys.
Inakuwa inataka kufanana na dictionary ambapo unakuwa na neno na tafsiri yake, kwahiyo lile neno tunakuwa tulichukulia kama key.
Example

Code

membersWaJamiiForum
={ 'x1':'ni member wa kwanza wa Jamii Forum',
'x2':'ni member wa pili wa jamii Forum',
'x3': 'ni member wa tatu wa jamii Forum'}
A.


Tukitaka kusoma taarifa za x1 tunatumia( Code: membersWaJamiiForum[‘x1’] )
Tukitaka kusoma taarifa za x2 tunatumia (code: membersWaJamiiForum[‘x2’] )

1753425557237.png



B. Ili kupata keys zote zilizopo kwenye dictionary
( Code: list(membersWaJamiiForum.keys() )
1753426408562.png

C. Kupata taarifa zilizokuwa ndani ya keys

(Code: membersWaJamiiForum.values() )
1753426529423.png

Tunaweza kutumia for loop ili tuweze kuona value moja moja.
1753426789203.png

D.
Ili kujua idadi ya taarifa ulizonazo kwenye dictionary

(Code: len(membersWaJamiiForum) )
1753426920594.png




E.
Tukitaka kuchange taarifa kwenye dictionary , tunatumia key moja ila maelezo tunayaweka mengine

(code : membersWaJamiiForum={ 'x1': 'huyu members hayupo' } )
1753427487212.png


F. Tukitaka kupata taarifa za dictionary kwa kutumia key

( Code: membersWaJamiiForum.get('x1') )
1753427532503.png

G
. Kama ukitumia get kutafuta key ambayo haipo jibu litakuja None

(code : membersWaJamiiForum.get('x5') )
1753427570469.png

H.
Kuongeza members mwingine kwenye dictionary
(code : membersWaJamiiForum['x4']= 'new member' )
1753427643892.png


I. k
ufuta vitu vitavyokuwa vinapatikana kwenye dictionary tutamia neno pop
(Code: membersWaJamiiForum.pop('x2') )
1753427711629.png


J.
Kufuta kila kitu kwenye list tunatumia neno clear

( Code: membersWaJamiiForum.clear() )
 
Vitu ambavyo mpaka sasa hivi tumeviangalia ni
1.Comment
2.Data type
3.Operators in python
4.If statement
5.Loops
6.Lists
7.Dictionaries
8.Function

Leo tuangalia namna ya kuanza kutengeneza basic Applications kwa kutumia tkinter (Graphical user interface,gui) ili tuweze kulink na tulivyosoma
 
tkinter
Hii ni GUI ( Graphical user Interface )

Hapa tunaweza kutengeneza mifumo mbalimbali katika computer yako , ambao mtumiaji atakuwa anaweka taarifa zake. Mfano mifumo ya hospitali, viwandani , kwenye mashule, mifumo ya kwenye masoko , mifumo ya standi , mifumo ya maduka n.k
Ili tuweza kuweza kuitumia tkinter cha kwanza tunakuwa tunaiita mwanzo wa kodi yetu ( Code: from tkinter import * ) , alama * inamaanisha vitu vyote ambavo vipo kwenye tkinter tunaweza kupata access zake. Then tunatengeza screen ambapo tutakuwa tunaandika taarifa mbali mbali ( Code: window=Tk() ) ,kwenye neno la window unaweza kuweka neno lolote unalotaka , Tutaspecify window iwe na size gani kwa kutumia geometry pamoja na title ya window . (Code: window.geometry(“ sizeUnayotaka” ) , window.title(“jinaLaMfumoWako”) )mwisho tunamalizia na (code: window.mainloop() ),mainloop() inawezesha application yetu kuonekana baada ya kuiandika
1753519460502.png


Label
Ili kuandika maneno ndani ya window tuliyotengeneza Tunamia neno Label ikifuatiwa na maneno unayotaka kuweka . (Code: jina=Label(window, text="jamii forum” ) ukirun program hii text tuliyoandika haiwezi kuonekana inabidi tumalizia na code za kuiweka kwenye window ,tunamia neno pack au place au grid . (Code : jina.pack() ) , au ukitumia place unaspecify x value pamoja na y value . ( Code: jina.place(x=0,y=0) )
1753519552120.png

Au tunaweza kutengeneza mfumo wa hospital
1753519588668.png

Entry
Entry inatumika kuchukua taarifa kwa mtu , Mfano jina lake, email yake, jinsia yake n.k . code zinakuwa kama Label tulizoziona hapo juu. ( Code: Entry(window) ) , ndani ya mabano ya entry au Label n.k. unaweza kuongezea taarifa za size ya maneno “font”, rangi wa maneno yaweje “fg” , background ya font yako “bgn.k.
1753519819086.png

Hizo rangi zinaonyesha mahusiano ya code na output
1753519879338.png

Note:

Hizo rangi zinaonyesha mahusiano ya code na output

Text
Tunakuwa tunatumia Text kama unataka kuandika mistari Zaidi ya moja .Inafanana na Entry isipokuwa Entry yenyewe tunatumia mstari mmoja .Mfano hapa tunapokuwa tunaandika ujumbe wetu kwenye jamii forum hii ni Text.Inakurusu andike zaidi ya mstari mmoja
(Code: Text() )

Button
Button inatumika endapo mtu anataka taarifa zake zikusanywe “ Button ya kusubmit “ au kuna taarifa anataka kuzifuta n.k. Ili kuweza kuandia button tunakuwa tunatumia Button .(Code : Button() ) ,ndani ya mapano tunaweka vitu mbali mbali ikiwemo, text ya button,colo,position ya button , command hii inatumika kuiita function endapo mtu ataclick button n.k
1753520249719.png




1753520281466.png



Checkbutton

Ni button ambayo mtu anaichagua ikiwa amekubaliana na taarifa flani , Tukitaka kuiweka tunatumia ( Code: Checkbutton(#humu ndani ya mabano vitu mbali mbali vinawekwa mfano maneno ya kuoneka ,ukubwa wa maneno, n.k ) ) , endapo checkbutton itakuwa clicked onvalue =1 vinginevyo offvalue=0 ) ,Hapa checkbutton mtu akiclick haifanyi chochote kwasababu bado hatujaandika code za kusema kitu gani kifanyike endapo mtu ataselect.

1753520393253.png

RadioButton

Inatumika katika kuchagua machaguzi mbali mbali zaidi ya moja unayotaka .

Mfano umeenda sehemu ya kula chakula umepewa Menu alafu unachagua unavyohitaji hii tunaweza kuirepresent k RadioButton. Au umeenda dukani unachagua vitu kadhaa unavyohitaji tukiandika program yake tunakuwa tunatumia RadioButton



Mfano ;Menu ya chakula
Kwanza tutaanza kusema list ya msosi iliyopo, ( Code: msosi=[‘wali nyama’,’pilau nyama’,’ugali Dagaa’,’ugali samaki’,’Ndizi’ ) then tunatumia for loop kuonyesha items moja baada ya nyingine, (Code: for chakula in range(len(msosi)) : ) then tunatumia Radiobutton kudisplay taarifa .

1753520658149.png
 
Tkinter using grid system


1753852707358.png


Code zilitumika juu badala ya pack kutumika tunaweza kutumia grid kuweka vitu kwenye window
1753852859873.png




1753852897453.png


Tunaweza kuzichukua taarifa kutoka kwa mtumiaji na kuzidisplay kwenye Application tuliyotengeneza au kuzipeleka kwenda kwenye database au tukazipeleka kwenda kwenye file.Tunatumia neno command ikifuatiwa na jina la function, pindi button inapo bonyezwa taarifa ambazo zitakuwa zimejazwa zinachukulia na kupeleka kwenye database, file au zinakuwa displayed

Simple code
Button ambayo mtu akibonyeza hello word inakuwa display
Code:
(Code: button1=Button(window,text="Bonyeza hapa",bg="black",fg="white", command=salamu )

1753853206517.png


Ilikuchua taarifa ambazo mtumiaji atakuwa ameziweka kwenye Entry tunatumia get() ndani ya function tutakayo iita ndani ya command.


1753853600087.png



Menubar
1753853634363.png


Hii code :fileMenu=Menu(menubar) inatumika kutengeneze menubar

Hii code : window.config(menu=menubar) inatumika kulink menubar zetu pamoja na Window yetu.

Ili kuweza kuadd menubar mbalimbali tunakuwa tunatumia add_cascade mfano menubar.add_cascade(label="JamiiHospital",menu=fileMenu)


Simple code

Python:
from tkinter import *

window=Tk()

window.geometry("420x420")

window.title("jamii Hospital ")


menubar=Menu(window)

window.config(menu=menubar)

fileMenu=Menu(menubar)

menubar.add_cascade(label="JamiiHospital",menu=fileMenu)

menubar.add_cascade(label="LOGIN",menu=fileMenu)

menubar.add_cascade(label="REGISTER",menu=fileMenu)

menubar.add_cascade(label="HELP",menu=fileMenu)
window.mainloop()


1753854918799.png


Combobox

Hii ni tunamia endapo kutakuwa na option mbali mbali tunataka mtumiaji achague moja. Mfano Jinsia yake Male or Female, Mwezi aliozaliwa, au mahali anapoishi

Code inayotumika ni Combobox()

from tkinter import *

Python:
from tkinter import ttk
window=Tk()
window.geometry("420x420")

window.title("jamii Hospital ")


label1=Label(window,text="Chagua jinsia yako" )
label1.pack()

opt=ttk.Combobox(window,values=["Male","Female"])
opt.pack()
window.mainloop()

OUTPUT

1753855016008.png


Scale.

Scale inawezesha mtu kuchagua namba yoyote itayokuwa inapatikna ndani ya range flani .Mfano tuna scale ya vertical itayoonesha tarehe kuanzia 1 mpaka 31 . Code: Scale(window,from_=1, to =31)

1753855053770.png
 

Attachments

  • 1753853401532.png
    1753853401532.png
    134.3 KB · Views: 19
  • 1753852642043.png
    1753852642043.png
    20.3 KB · Views: 19
Back
Top Bottom