Wana JF, leo ninakwenda kusimama mbele ya Wabunge wote wa CCM kuomba kupitishwa kwenye kura zao za maoni ya kugombea Ubunge wa EAC, ninaamini niaenda pale nikiiwakilisha JF sasa ni muhimu sana leo tukaweka tofauti ya itikiadi zetu pembeni na kwua kitu kimoja katika kuombeana na kutakiana heri, kupita kwangu ni kupita kwa JF.
- Nimesema huko nyuma na ninasema tena mimi Mwanachama wa CCM, tena hai na wa muda mrefu sana toka mwaka 1982 nikiwa JKT Oljoro kwa mujibu wa sheria ya mwaka mmoja baada ya kusomeshwa bure na Serikali ya Awamu ya kwanza. Nia na madhumuni yangu siku zote ni mabadiliko ya mwenendo wa kisiasa kwa taifa letu, ili tuweze kusonga mbele kulingana na wakati, ninaamini kwamba wengine wakija na ideas kutoka upinzani na wengine tukija na the same ideas kutokea ndani ya CCM, siku moja tutalisaidia taifa letu kufikia pahali linapotakiwa kwa nyakati hizi za kisayansi.
- Kwa kifupi ninataka kwenda EAC, ili kulisimamia taifa langu kwenye masuala ya interest za kiuchumi na hasa Ardhi yetu nikiwa ninajua kwamba nchi zingine Nne za Jumuiya hazina sheria za serikali za kusimamia Ardhi zao kwa sababu hata hiyo Ardhi hawana tena yote ilishanunuliwa na wananchi wao, sisi tu ndio bado tuna Ardhi inayosimamiwa kisheria na serikali yetu. Pia ninataka kuhakikisha Tanzania haturudii tena makosa ya nyuma ya kushirki kwenye Jumuiya iliyokufa mwaka 1977, ambapo ilipokufa sisi tuliumia sana kwa sababu tulikuwa tumejikita sana huko, infact mpaka leo kuna areas kama za Airline na Railways, bado tumeshindwa ku-recover, sitaki Tanzania tukimbizwe na Kenya walivunja Jumuiya ya kwanza kwenye One Currency na Political Federation, ninasema kwamba tujifunze kuwa EU sasa hivi iko matatizoni ni kwa sababu ya mbio mbio za kuanzisha jumuiya hiyo bila utafiti wa kutosha.
Kwa hayo machache ninaomba kuwaomba JF wote leo tujaribu kuombeana heri ili tupite kwa sababu kupita kwangu ni kupita kwa JF pia!
MUNGU AIBARIKI TANZANIA NA PIA AIBARIKI JF KUMKOMA NYANI1
William.