Hili swala la ununuzi sijui usombaji wa korosho siyo jukumu la jeshi letu.
Dunia inashangaa kuona jeshi letu badala ya kulinda mipaka ya nchi linatumika kuwatisha raia na mali zao.
Hatukununua magari ya jeshi Kwa ajili ya kusomba korosho ambazo hata hatuja ambiwa zinasombwa kupelekwa wapi.
Kuliingiza jeshi kufanya kazi ndogondogo kama hizo ni kulidhalilisha jeshi letu.
Huenda Amri jeshi hajui muda wa kukagua magari na kutembelea jeshi, ni ule muda ambao Nchi ipo kwenye hatari ya kuvamiwa.
Unapotembelea jeshi Kwa minajili ya kununua korosho tunakua na mashaka na nia yako.
Tulipe jeshi letu heshima.lina kazi kubwa ya kufanya Kwa ajili ya kulinda mipaka ya nchi yetu siyo kusomba sijui kubangua korosho.
Tusitumie jeshi letu kisiasa.