Jeshi la polisi Ruvuma: Tunaendelea na upelelezi wa tukio la kupotea kwa Padre Camillus Nikata Mhadhili wa Chuo Kikuu SAUT

Jeshi la polisi Ruvuma: Tunaendelea na upelelezi wa tukio la kupotea kwa Padre Camillus Nikata Mhadhili wa Chuo Kikuu SAUT

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
33,612
Reaction score
40,158
Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma linaendelea na Upelelezi wa tukio la kupotea kwa Padre Camillus Nikata wa Jimbo kuu Songea ambaye pia ni Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) Mwanza.

Akiongea Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Kamisha Msaidizi Mwandanizi wa Polisi (SACP) Marco G. Chilya amesema kuwa Padri Nikata alifika Songea tarehe 03.10.2025 akitokea Dodoma huku akiwa na mhadhili mwenzake ambaye ni Padre wa Jimbo la Songea na kufikia katika nyumba ya Mapadre, St. Shanney, Ilipofika tarehe 07.10.2025 majira ya jioni Father Nikata alionwa na padre mwenzake huko Mtaa wa Kanisani akiwa na kibegi kidogo Mkononi akielekea Stendi ya zamani ya Mabasi Mfaranyaki ambapo tokea tarehe hiyo hakuweza kurudi mahali alipofikia jimboni.

Hata hivyo uongozi wa Kanisa hilo na Mapadre wenzake waliendelea na Juhudi za Kumtafuta sehemu tofautitofauti ambazo walisadiki kuwa atakuwepo lakini hawakufanikisha kumpata ndipo ilipofika tarehe 09.10.2025 waliweza kutoa taarifa ya kutoonekana kwa Father Nikata tangu tarehe 07.10.2025.

Pia Soma: Kanisa Katoliki latoa taarifa ya "kutoonekana" kwa Padre Camillus Nikata wa Jimbo Kuu la Songea
 
Yeye huyu hana tatizo la afya ya akili kama yule mwenzie tulioambiwa alijiteka!?
 
Imagine kila mahali ni hadithi za kupotezwa, taifa la kihuni sana limekuwa.
 
Screenshot_20251012-142151.jpg
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma linaendelea na Upelelezi wa tukio la kupotea kwa Padre Camillus Nikata wa Jimbo kuu Songea ambaye pia ni Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) Mwanza.

Akiongea Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Kamisha Msaidizi Mwandanizi wa Polisi (SACP) Marco G. Chilya amesema kuwa Padri Nikata alifika Songea tarehe 03.10.2025 akitokea Dodoma huku akiwa na mhadhili mwenzake ambaye ni Padre wa Jimbo la Songea na kufikia katika nyumba ya Mapadre, St. Shanney, Ilipofika tarehe 07.10.2025 majira ya jioni Father Nikata alionwa na padre mwenzake huko Mtaa wa Kanisani akiwa na kibegi kidogo Mkononi akielekea Stendi ya zamani ya Mabasi Mfaranyaki ambapo tokea tarehe hiyo hakuweza kurudi mahali alipofikia jimboni.

Hata hivyo uongozi wa Kanisa hilo na Mapadre wenzake waliendelea na Juhudi za Kumtafuta sehemu tofautitofauti ambazo walisadiki kuwa atakuwepo lakini hawakufanikisha kumpata ndipo ilipofika tarehe 09.10.2025 waliweza kutoa taarifa ya kutoonekana kwa Father Nikata tangu tarehe 07.10.2025.

Pia Soma: Kanisa Katoliki latoa taarifa ya "kutoonekana" kwa Padre Camillus Nikata wa Jimbo Kuu la Songea
Wamemteka wao ujinga tu anaeleza hapa. Anadhani watu ni wajinga
 
Back
Top Bottom