Kwani wewe ulimuandika vibaya??huyu mchungaji mlevi hadi kufika march mwakani atakufa kwa njaa Kwa kukosa sadaka au nusu ya waumini wake watamkimbia
huu ni utabiri wangu kwake,hiyo mikwala yake akawatishe watoto wake na misukule(waumini)wake yeye nani mpaka awatabirie kifo waandishi?
Lishatolewa na Dr. Mwigulumimi nilijua wanatoa tamko la maiti zilizofukiwa.
swissme
Aah kabisa. Maana mi sijaelewa kwamba jeshi la polisi siku hizi linakazi ya kutoa matamko?Tujiandae kwa danadana na doublestandard!
Je, Lema kwao ni mungu mpaka wamshtaki?Huu unabii wa mzee wa upako si unafanana na ndoto ya mbunge wa Arusha Godbless Lema. Ngoja tuone hatua zitakazochukuliwa na vyombo vya usalama.
Lema anafananishwaje hapa?unafikiri kutumia ubongo kweli au sehemu tofauti?Huu unabii wa mzee wa upako si unafanana na ndoto ya mbunge wa Arusha Godbless Lema. Ngoja tuone hatua zitakazochukuliwa na vyombo vya usalama.
mkuu umewaza nini? Nimebaki nacheka tu ndo mana waumini huitwa KONDOOKama Mungu ni wa udongo basi utabiri wake utatimia.
Sirro mwenyewe anaogopa kufa unadhani atatoa kauliSiku moja baada ya Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo maarufu Mzee wa Upako kusema waandishi waliomuandika vibaya watakufa kabla ya Machi 2017, Jeshi la Polisi linatarajia kutoa msimamo wake dhidi ya kauli hiyo leo.
Kauli hiyo ya Mzee wa Upako aliyoitoa juzi kanisani kwake, ilikuwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo akijibu yale yaliyoandikwa katika vyombo vya habari kuhusu madai ya kulewa na kumfanyia fujo jirani.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Kipolisi ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro jana alisema ni mapema kuzungumzia sakata hilo kwa sababu jana ilikuwa sikukuu na atatolea ufafanuzi leo.
“Anasema hao waandishi watakufa kabla ya Machi 2017 kwani yeye Mungu? Hilo ni suala zito, tumeandaa mkutano na waandishi wa habari tutalizungumzia suala hilo kesho (leo),” alisema Kamanda Sirro.
Katika kauli hiyo, Mzee wa Upako alisema kila mwandishi aliyemuandika vibaya ikifika Machi mwakani hatakuwa hai na kama wataendelea kuishi, ataacha kazi ya kuhubiri injili na kwenda kuuza gongo.
Hayo mamlaka ya kuhukumu ameyatoa wapi? Math 7: 1-5mkuu umewaza nini? Nimebaki nacheka tu ndo mana waumini huitwa KONDOO
Nasubiria Polisi wamuweke ndani Bila dhamana kama walivyo fanya kwa Lema.Siku moja baada ya Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo maarufu Mzee wa Upako kusema waandishi waliomuandika vibaya watakufa kabla ya Machi 2017, Jeshi la Polisi linatarajia kutoa msimamo wake dhidi ya kauli hiyo leo.
Kauli hiyo ya Mzee wa Upako aliyoitoa juzi kanisani kwake, ilikuwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo akijibu yale yaliyoandikwa katika vyombo vya habari kuhusu madai ya kulewa na kumfanyia fujo jirani.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Kipolisi ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro jana alisema ni mapema kuzungumzia sakata hilo kwa sababu jana ilikuwa sikukuu na atatolea ufafanuzi leo.
“Anasema hao waandishi watakufa kabla ya Machi 2017 kwani yeye Mungu? Hilo ni suala zito, tumeandaa mkutano na waandishi wa habari tutalizungumzia suala hilo kesho (leo),” alisema Kamanda Sirro.
Katika kauli hiyo, Mzee wa Upako alisema kila mwandishi aliyemuandika vibaya ikifika Machi mwakani hatakuwa hai na kama wataendelea kuishi, ataacha kazi ya kuhubiri injili na kwenda kuuza gongo.
Mambo ya kishetani au giza yana mwisho mbaya. Makucha yameanza kujitokeza. Matusi, vitisho, sijui ulevi.... vyote tunaviona na kusikia kwa masikio yetu hata uki google kwenye google videos utapata na kuchambua mbichi na mbivu. Anayezungumza kwenye video kwa kutukana na vitisho ni yeye. Kwanini alaumu wengine?Nna mashaka sana na akili za waumini wa huyu mzee...!