Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 36,357
- 23,760
Ndugu zangu Watanzania,
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Limetoa taarifa ya kuwa halijapokea taarifa yoyote ile juu ya uwepo wa tishio la kuuwawa kwa Dkt Kitima katibu Mkuu wa TEC. Ambaye hivi karibuni alitoa taarifa zenye kueleza uwepo wa Taarifa za Tishio la kuuwawa kwake.
Akisema ya kuwa siku chache zilizopita alitaka kuhudhuria msiba wa Marehemu Jenista Mhagama lakini akashindwa baada ya kupewa Taarifa za kumtaka asihudhurie kutokana na kuwindwa na watu aliodai wasiojulikana.
Ikumbukwe ya Kuwa Padri huyu Amekuwa akizungumza mambo mbalimbali bila kuweka ushahidi hadharani ama kutoa taarifa ama kuripoti katika vyombo vya ulinzi na Usalama hususani Jeshi la polisi ambalo ndio lenye Jukumu hilo la kuchunguza ,kupeleleza na kufanyia kazi madai ya aina hiyo juu ya usalama wa mtu yeyote yule anayehisi yupo hatarini ama anawindwa na watu wasiojulikana.
Embu soma hapa taarifa ya Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam kupitia Kamanda wake wa Kanda hiyo Jumanne Mulilo.👉Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Jumanne Muliro amesema hawajapokea taarifa yoyote kutoka kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Dkt. Charles Kitima juu ya madai ya kutaka kuuliwa.
Akijibu swali la Mwandishi wa AyoTV leo Kamanda Muliro alisema “Ndio nimesikia kutoka kwako, kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda kila Mtu wakiwemo Ma-Father”.
Itakumbukwa hivi karibuni, Padri Kitima alisikika akizungumzia hofu ya maisha yake wakati akimtambulisha Naibu Katibu Mkuu mpya wa Baraza hilo Padri Dkt. Faustine Furaha wa Jimbo Katoliki Moshi ambaye amechukua nafasi ya Padri Chesco Msaga aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Kristo Duniani.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Limetoa taarifa ya kuwa halijapokea taarifa yoyote ile juu ya uwepo wa tishio la kuuwawa kwa Dkt Kitima katibu Mkuu wa TEC. Ambaye hivi karibuni alitoa taarifa zenye kueleza uwepo wa Taarifa za Tishio la kuuwawa kwake.
Akisema ya kuwa siku chache zilizopita alitaka kuhudhuria msiba wa Marehemu Jenista Mhagama lakini akashindwa baada ya kupewa Taarifa za kumtaka asihudhurie kutokana na kuwindwa na watu aliodai wasiojulikana.
Ikumbukwe ya Kuwa Padri huyu Amekuwa akizungumza mambo mbalimbali bila kuweka ushahidi hadharani ama kutoa taarifa ama kuripoti katika vyombo vya ulinzi na Usalama hususani Jeshi la polisi ambalo ndio lenye Jukumu hilo la kuchunguza ,kupeleleza na kufanyia kazi madai ya aina hiyo juu ya usalama wa mtu yeyote yule anayehisi yupo hatarini ama anawindwa na watu wasiojulikana.
Embu soma hapa taarifa ya Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam kupitia Kamanda wake wa Kanda hiyo Jumanne Mulilo.👉Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Jumanne Muliro amesema hawajapokea taarifa yoyote kutoka kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Dkt. Charles Kitima juu ya madai ya kutaka kuuliwa.
Akijibu swali la Mwandishi wa AyoTV leo Kamanda Muliro alisema “Ndio nimesikia kutoka kwako, kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda kila Mtu wakiwemo Ma-Father”.
Itakumbukwa hivi karibuni, Padri Kitima alisikika akizungumzia hofu ya maisha yake wakati akimtambulisha Naibu Katibu Mkuu mpya wa Baraza hilo Padri Dkt. Faustine Furaha wa Jimbo Katoliki Moshi ambaye amechukua nafasi ya Padri Chesco Msaga aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Kristo Duniani.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.