Jery Muro wa TBC amenusurika kupewa kichapo majira ya mchana leo tar.15.05.2013 kutokana na issue ya gas. Kama mujuavyo huyu jamaa anaendesha kipindi chake cha rasilimali gas TBC, leo alikuwepo mjini Mtwara kuchukua maoni kwa wanamtwara juu ya msimamo wao ktk ujenzi wa bomba la gas kutoka Mtwara kuelekea dar. Chanzo cha mtafaruko baina ya wananchi na Jery Muro ni pale Jery alipojaribu kuonesha kuiunga mkono serikali kuendeleza nia yake ya kutaka kujenga bomba la gas huku akijaribu kusema wanamtwara wakubali tu kwan watanufaika km wanavyonufaika wananchi wa Kilwa kupitia mradi wa SONGAS kwa kusanya kodi ya mrahaba wa 0.3%. Bila police kufika mapema kumwokoa story zingekuwa tofauti kbs.