Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,801
- 71,223
Tatizo viongozi wetu wana kichwa ngumu na sio rahisi kujifunza kutokana na maovu yaliyo pita.
Au ni kutudharau kuwa Watanzania hawa ni zumbukuku watatufanya nini sisi na chama chetu CCM?
KADCO imetafuna KIA na sasa kwa namna ileile DUBAI na kampuni yao DPW wanapewa watafune Bandari zetu lakini Watanzania wakitaka kupinga wanatumia watoto wetu Polisi (nao bila aibu wanakubali) kutuvunja miguu.
Nakumbuka utawala wa Dikteta wa Sudan Omar El Bashir ulipoanza kutaka kuwazuia raia kuandamana kwa kutumia polisi wake Jeshi la wananchi (kama JWTZ yetu) liliamua kusimama na wananchi hadi akaondolewa madarakani kwa kukaidi mawazo yao na ameishia kifungoni.
Kwa nini wetu hawajifunzi?
Au ni kutudharau kuwa Watanzania hawa ni zumbukuku watatufanya nini sisi na chama chetu CCM?
KADCO imetafuna KIA na sasa kwa namna ileile DUBAI na kampuni yao DPW wanapewa watafune Bandari zetu lakini Watanzania wakitaka kupinga wanatumia watoto wetu Polisi (nao bila aibu wanakubali) kutuvunja miguu.
Nakumbuka utawala wa Dikteta wa Sudan Omar El Bashir ulipoanza kutaka kuwazuia raia kuandamana kwa kutumia polisi wake Jeshi la wananchi (kama JWTZ yetu) liliamua kusimama na wananchi hadi akaondolewa madarakani kwa kukaidi mawazo yao na ameishia kifungoni.
Kwa nini wetu hawajifunzi?
Uwanja wa KIA warudishwa serikalini baada ya miaka 25
Serikali imetangaza leo kuwa hatimaye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) utakabidhiwa kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) inayomilikiwa na Serikali kuanzia kesho, Novemba 10 2023. Hata hivyo, taarifa kuhusu wamiliki wa awali wa Kampuni ya Uendelezaji na Uendeshaji wa...
swahilitimes.co.tz