Jeans Chano ilivyoniachanisha na Mchumba wangu

Jeans Chano ilivyoniachanisha na Mchumba wangu

Mshamba wewe sijui wa wapi nshamba kunakuharibu khaaaa eti ukamsukuma ili iweje
 
Wasukuma inabidi muoane wenyewe kwa wenyewe tu kwa kweli. Just kidding.

2015-Mid-Waist-Jeans-Woman-Knee-Skinny-Pencil-Pants-Slim-Denim-Ripped-Boyfriend-Jeans-For-Women.jpg

Ilikuwa hivi, au?​
Zinanoga mnoo huyu nae sijui wa wapi hata usukumani hayupo
 
Kama wewe ni born again christian uko sawa Lakini kama hauko msamehe maridie maana hata wewe unakosea hakuna lisilo weza kuzumgumzika
 
Mtengeneze mtu the way unavyotaka awe. Jeans tu ndio drama zote hizo!!
 
Wana JF,

Nikiwa na tahashishi na mashamu shamu ya kukutana na chombo murua kabisa, nimesindikizwa na rafiki zangu wawili tukafika kwa mchumba wangu ambaye ndio kwanza alikuwa ana miezi miwili ameajiriwa kwenye hosptali moja ya mission Rubya Hospital ghafla anaingia mtu amejipamba sana , akiwa ameweka nywele nyingi kukifanya kichwa kuwa mzigo, huku chini akiwa amevaa kitop na jeansi lililochanika chanika, akataka kuniwau, nilishutuka nimebadilika na kumsukuma kwa muda, kutuachanisha alafu nikakaa kama dakika mbili hivi , nikamuuliza umefanya nini? yeye kimya)umefundishwa hivyo (kimya) nikawaambia rafiki zangu tuondoke.

Kwa kweli mchumba alibadilika akaangua kilio kuomba samahani nikamwambia tutaonana tu tukiwa peke yetu, akanikubalia tukaondoka. Tukiwa njiani tunatembea niliingiwa na ukimya sana rafiki zangu wakaniuliza mbona umeshindwa kumsamehe kwa kitu kidogo jeans tu. Nikawajibu, ndoa haijalibiwi, kama mtu anajiondoa ufahamu mapema anafanya vituko mbele ya marafiki zangu mapema hivi, akiizoea ndoa itakuwaje?

Wanandugu huu ulikuwa ujinga kwangu au niliona mbali, kama ungekuwa wewe mrembo unayemtegemea aongoze familia anakuja na nguo zinazovaliwa na machiz eti fashion ungefanyaje.
kwa hii ishu yako ndogo hivo umeshindwa kuislove! inafanya niamini ww bado mvulana. mambo hayaendi hivo jamaa, mngekaa peke yenu then ukamuelewesha.
 
Paka alijisahau akayaachia makucha.

Hongera sana kwa kubadili gia angani.
 
Nicheke kwa makelele [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji2]
 
Ndio kwenye zawadi za ndoa mnaletewa picha watu wanakula 0713 unawehuka.

Ni kuwa makini na vitu kama hivyo kama mtu hajapevuka vya kutosha mwache akalelewe akue kama yy akivaa hivyo mtoto atamvisha nini?
 
Ana umri gani huyo mchumba..Ila na wewe utakua mvulana. Wenzako huwa wanapotezea ishu kama hizo halafu baadae ndo anamuita na kumueleza hajapenda mavazi yake. Be a man bro. Hivyo ni vitu vidogo na vinarekebishika.
Bwana wewe alinishutua sana nikaona kwamba hii tabia uenda akaiendeleza
 
Wewe huna tatizo hata moja maishani? Kulikuwa na haja gani kumsukuma asikuwao?

Anyway nadhani na wewe una mapungufu sana ya kushindwa kuvumilia kitu, mume Bora ni Yule anaeweza kuona Jambo na akajipa muda kutafakari bila ku'overeact'

Kiufupi ulikosea na hilo halikuwa kosa la kuachana nae, ungemwambia tu unapenda mavazi ya namna gani na yapi hupendi......

Umekosa mke ambae pengine ndio angekuwa Bora kabisa. Mapenzi bila uvumilivu si sawa.

Hatujui lakini yawezekana ni yeye Mungu ndio kamuepusha na mume mwenye Gubu.........
hahaha kweli kabisa jamaa anajifanya ameshindwa kuvumilia kitu kidogo ila ni kweli mungu amemuepusha mschana na mikomoto mana huyu jamaa ni dikteta u....r
 
Mwanamke hakosolewi hadharani na mbaya zaidi mbele ya rafiki zako.

Lakini pia marafiki zako hawakushauri vizuri. Ingekuwa mimi ningekuambia live hiyo sio sehemu ya kurekebishana.
 
Mkuu, afadhali wewe uliudhika na hiyo jeans iliyochanwachanwa! Mimi msichana hata nimzimikie vipi nikigundua anavaa suruali aina yoyote, naishia hapohapo. Nitamfundisha mwanamke mengine lakini siyo kumfundisha mavazi. Kama hadi miaka ishirini na kitu hajui kujisitiri kwa mavazi, hata akianza kujiheshimu kwa ajili yangu....nisipokuwa karibu atajiachia tu! Kwangu mimi msichana mvaa suruali ni big no. Na msimamo huu umenisaidia sana na mambo haya, maana kizazi hiki wavaa suruali ni wengi mno.
 
Hao hao wavaa madela nakujisitili ndio wanaoongoza kwa michepuko, nani kakwambia kuvaa suluali nitabia mbaya hapo inategemea ni aina gani, mbona nyie mwavaa milegezo hatusemi mwasuka mpaka nywele, heleni mwavaa tatizo ushamba tuu kaoe kijijini mvaa kanga kuoga mpaka ucku wakati wakulala, wengi mnaogopa matumizi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom