Jeans Chano ilivyoniachanisha na Mchumba wangu

Jeans Chano ilivyoniachanisha na Mchumba wangu

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,793
Reaction score
7,171
Wana JF,

Nikiwa na tahashishi na mashamu shamu ya kukutana na chombo murua kabisa, nimesindikizwa na rafiki zangu wawili tukafika kwa mchumba wangu ambaye ndio kwanza alikuwa ana miezi miwili ameajiriwa kwenye hosptali moja ya mission Rubya Hospital ghafla anaingia mtu amejipamba sana , akiwa ameweka nywele nyingi kukifanya kichwa kuwa mzigo, huku chini akiwa amevaa kitop na jeansi lililochanika chanika, akataka kuniwau, nilishutuka nimebadilika na kumsukuma kwa muda, kutuachanisha alafu nikakaa kama dakika mbili hivi , nikamuuliza umefanya nini? yeye kimya)umefundishwa hivyo (kimya) nikawaambia rafiki zangu tuondoke.

Kwa kweli mchumba alibadilika akaangua kilio kuomba samahani nikamwambia tutaonana tu tukiwa peke yetu, akanikubalia tukaondoka. Tukiwa njiani tunatembea niliingiwa na ukimya sana rafiki zangu wakaniuliza mbona umeshindwa kumsamehe kwa kitu kidogo jeans tu. Nikawajibu, ndoa haijalibiwi, kama mtu anajiondoa ufahamu mapema anafanya vituko mbele ya marafiki zangu mapema hivi, akiizoea ndoa itakuwaje?

Wanandugu huu ulikuwa ujinga kwangu au niliona mbali, kama ungekuwa wewe mrembo unayemtegemea aongoze familia anakuja na nguo zinazovaliwa na machiz eti fashion ungefanyaje.
 
no body is perfect, there is no an angel. endelea kutafuta utampata asiyevaa jeans ila kikojozi au mlevi n.k
lakini ishara ya kua-act uchizi mapema kwenye maisha ya uchumba ilikuwa sahihi?
 
Wewe huna tatizo hata moja maishani? Kulikuwa na haja gani kumsukuma asikuwao?

Anyway nadhani na wewe una mapungufu sana ya kushindwa kuvumilia kitu, mume Bora ni Yule anaeweza kuona Jambo na akajipa muda kutafakari bila ku'overeact'

Kiufupi ulikosea na hilo halikuwa kosa la kuachana nae, ungemwambia tu unapenda mavazi ya namna gani na yapi hupendi......

Umekosa mke ambae pengine ndio angekuwa Bora kabisa. Mapenzi bila uvumilivu si sawa.

Hatujui lakini yawezekana ni yeye Mungu ndio kamuepusha na mume mwenye Gubu.........
 
Wasukuma inabidi muoane wenyewe kwa wenyewe tu kwa kweli. Just kidding.

2015-Mid-Waist-Jeans-Woman-Knee-Skinny-Pencil-Pants-Slim-Denim-Ripped-Boyfriend-Jeans-For-Women.jpg

Ilikuwa hivi, au?​
 
Hahahaha yaan nilidhan sijui kafanyaje
 
lakini ishara ya kua-act uchizi mapema kwenye maisha ya uchumba ilikuwa sahihi?
Nadhani kama unamfahamu kwa muda mrefu labda miezi sita ni lazima utakua unafahamu style yake ya mavazi. kama ndiyo mara ya kwanza kuvaa ina maana anaiga na ni rahisi kuacha maana hujapendezwa nayo. ila kama anavaaga na ukampenda hivyo hivyo, unamwonea sababu ulimpenda jinsi alivyo. kitu cha msingi ongea na mchumba wako umweleze kuwa hupendi na kama anakupenda kweli ataacha.
 
hukumpenda!!( whole point)
mavazi: kama mwanamke unampenda kweli na yeye anakupenda unayabadilisha
mimi binafsi sijawahi kuwa na mwanaume ambaye hajawahi kunichagulia mavazi
mfano: nilipata ostadh nikawa navaa mabaibui na madera
nikapata kijana nikawa navaa kasoro vimini na nguo anazokataza...

tatizo hukumpenda tuu huna lolote..
angekataa kubadili mavazi siku ingine ungemwacha kaka...

kosa moja haliachi mke..
 
Wana JF,

Nikiwa na tahashishi na mashamu shamu ya kukutana na chombo murua kabisa, nimesindikizwa na rafiki zangu wawili tukafika kwa mchumba wangu ambaye ndio kwanza alikuwa ana miezi miwili ameajiriwa kwenye hosptali moja ya mission Rubya Hospital ghafla anaingia mtu amejipamba sana , akiwa ameweka nywele nyingi kukifanya kichwa kuwa mzigo, huku chini akiwa amevaa kitop na jeansi lililochanika chanika, akataka kuniwau, nilishutuka nimebadilika na kumsukuma kwa muda, kutuachanisha alafu nikakaa kama dakika mbili hivi , nikamuuliza umefanya nini? yeye kimya)umefundishwa hivyo (kimya) nikawaambia rafiki zangu tuondoke.

Kwa kweli mchumba alibadilika akaangua kilio kuomba samahani nikamwambia tutaonana tu tukiwa peke yetu, akanikubalia tukaondoka. Tukiwa njiani tunatembea niliingiwa na ukimya sana rafiki zangu wakaniuliza mbona umeshindwa kumsamehe kwa kitu kidogo jeans tu. Nikawajibu, ndoa haijalibiwi, kama mtu anajiondoa ufahamu mapema anafanya vituko mbele ya marafiki zangu mapema hivi, akiizoea ndoa itakuwaje?

Wanandugu huu ulikuwa ujinga kwangu au niliona mbali, kama ungekuwa wewe mrembo unayemtegemea aongoze familia anakuja na nguo zinazovaliwa na machiz eti fashion ungefanyaje.
Umepanic vbaya mkuu.Nina mke ni mwaka mmoja sasa nilimbadilisha dini.Taratbu anajitahid kuvaa kiislam(kama ntakavyo).So,mfahamishe tu jinsi gan unapenda avae na vp asivae
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom