Je wewe ulishaonja hii?

Je wewe ulishaonja hii?

ameline

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
2,292
Reaction score
1,152
[h=3]HILI SUFURIA UKILITAZAMA SUPU ILIYOPIKWA HUMO HUWEZI KUITAMANI,LAKINI....[/h]
Hapa imepikwa supu ya hatarii yenye mchanganyiko wa makongoro,utumbo,mkia,ulimi n.k
Sufuria huwekwa mezani kama hivi na watu hulizunguka kuchagua unachotaka
Hapo unasimama unachagua kipande unachokitaka unakatiwa katiwa na kuwekewa supu kwenye kibakuli huku ikiwa ni ya motoooo.
Baada ya nusu saaa tu sufuria linawezakuwa jeupeeee mzigo umekata.









[h=3]KUTANA NA KITU CHA MTURA[/h]
Mtura ni chakula maarufu sana mkoani Arusha.Ni utumbo ule unaoitwa utumbo wa maziwa unaoshwa vizuri na kufungwa halafu ndani kuwekwa vipande vidogo vidogo vya nyama.Nyama hizo zinakuwa zimetiwa pilipipili,ndimu,mboga mboga na viungo mbali mbali inategemea.Halafu unafungwa na kuchomwa.
Ukiiva ndio unaliwa na salad kama hivyo na ndizi hata chipsi.





Karibuni sana Arusha jaman, msisite kunitafuta ili niwapeleke zinakopatikana huduma hizi.....
 
yaan supu bila pilipili? na malimao ya kutosha usiwaze
 
mi hapo nataka mtura tu maana nimemis sana hiyo kitu...loh yani ameline leo na post zako unanijaza mate mdomoni maan tulianza na bamia na sas ni hii dhuu
 
Last edited by a moderator:
ooh my dear Rich woman usijali mate hayo yatakauka tu siku moja, nataka muenjoy jamani
 
Arusha sehemu gn zinapatikana hivi vitu maana tunajua ukitaka nyama ya mbuzi ya uwakika ni kwa MUROMBO sasa tujuze na hii supu zinapatikana wapi au UNGA LIMITED?
 
Arusha sehemu gn zinapatikana hivi vitu maana tunajua ukitaka nyama ya mbuzi ya uwakika ni kwa MUROMBO sasa tujuze na hii supu zinapatikana wapi au UNGA LIMITED?

maeneo ni mengi jamani sasa nikitaja hapa sitaambiwa kuwa natangaza biashara za watu?
 
Daa Krismass iliyopita nilikaa pale Keni Garden nikapata supu safii na mtura..Halafu ukizingatia Mwezi ule mvua na baridi ilikuwa at climax...Baaasi raha ya supu ya kongoro unaipata kuanzia utosini mpaka kwenye unyayo..
 
Arusha sehemu gn zinapatikana hivi vitu maana tunajua ukitaka nyama ya mbuzi ya uwakika ni kwa MUROMBO sasa tujuze na hii supu zinapatikana wapi au UNGA LIMITED?

Keni Gardeni na maeneo yotee yaliyo karibu, Jogoo house pia...Ahhh sehemu nyingi tuu mkuu..
 
Hiyo mitura zamani nilikuwa nikifikiri ni zile 'private parts' za mbusi au ngombe. siku niliyokuja kuifahamu nilistaabishwa sana.

kweli hiyo thupu ni fresh wala siyo ya kukaa kwenye majokofu kwa muda mrefu. walio mbali na nyumbani (Tanzania) nafikiri wao ndiyo mate zaidi.

kweli raha ya thupu uchague mwenyewe.
 
Hiyo mitura zamani nilikuwa nikifikiri ni zile 'private parts' za mbusi au ngombe. siku niliyokuja kuifahamu nilistaabishwa sana.

kweli hiyo thupu ni fresh wala siyo ya kukaa kwenye majokofu kwa muda mrefu. walio mbali na nyumbani (Tanzania) nafikiri wao ndiyo mate zaidi.

kweli raha ya thupu uchague mwenyewe.

Acha kabisa ndugu yangu junk food hazifai , nakumbuka enzi zangu nikienda picnic bar hapo ARUSHA hizo vitu nilikuwa nakula sana.
 
Back
Top Bottom