Je, Werema, Muhongo na Maswi ni wahanga wa pesa za kampeni ya CCM?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Kurudishwa kwa Prof. Muhongo na pia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi kumezua maswali ambayo yanahitaji majibu mbadala!

Nisingepata maswali kama wangerudishwa na Serikali ya Rais Kikwete kutokana na historia yake kiutendaji lakini ninapatwa na maswali baada ya kurudishwa kwenye nafasi za juu za kisiasa katika serikali ya Rais Magufuli ambayo inajipambanua na nimeiona ni no-nonsense, results-driven government.

Kwa alichokifanya Rais Magufuli na historia aliyonayo ndani ya serikali, uteuzi wa Prof. Muhongo na Maswi unatoa picha nyingine kwenye kadhia ya Tegeta Escrow Account.

Wakati wa sakata la Tegeta Escrow account, Kumbukumbu zinaonyesha Prof. Muhongo aliwahi kusema hawezi kujiudhuru na kama ikitokea hivyo basi nchi itatikisika.Kwa maana nyingine, alikuwa amebeba bomu kubwa la kisiasa ambalo alikuwa tayari kuripua iwapo atashinikizwa kujiudhuru hata hivyo inaonekana alishauriwa na watu wa ‘’kitengo’’, akajiudhuru ili kulinda heshima ya serikali kwa matarajio ya baadaye.

Hata aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi aliwahi kusema hahusiki na sakata hili bali alifanya kazi kama alivyoshauriwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema.

Maswi baada ya kusafishwa na tume ya maadili, aliteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara huku Prof. Muhongo akijikita kutafuta nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea Urais na ubunge kwa tiketi ya CCM.

Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema alikiri hata ndani ya Bunge, kuwa ni kweli kuwa alitoa ushauri kwa mamlaka ya juu ili kuidhinisha fedha kutolewa na kwa maana hiyo yuko tayari kubeba msalaba wa Prof Muhongo na Maswi. Kwa sasa amerudi kwenye kazi yake ya Ujaji.

Mpaka sasa tunachofahamu ni kuwa, pesa zilichukuliwa lakini hatufahamu nani aliyechukua na kuweka kwenye ‘’mifuko ya lambo’’ na lumbesa katika Benki ya Stanbic, lakini kikubwa zaidi, hizo pesa zilienda wapi?

Uchunguzi wa sakata hili mpaka sasa ‘’haujamalizika’’ lakini waliowajibika kisiasa wamerudishwa katika nafasi za juu nchini.

Kwa yanayofanyika kwa sasa, kuna hatari na uwezekano tulikuwa tunacheza ngoma ya kisiasa ambayo hatufahamu mapigo yake achilia mbali wapigaji wake.

Hizi teuzi zinaacha maswali mengi bila majibu!

Ama kweli usilolijua...
 
Unasema werema kapewa ulaji mbona hutwambii ni nafasi gani kapewa? Hii hekaya ya kusadikika kwa kuunganisha dot ukimpelekea Kubenea atakulipa vizuri maana mkiiuza front page mtayakamata manyumbu ya kutosha.
 
Unasema werema kapewa ulaji mbona hutwambii ni nafasi gani kapewa? Hii hekaya ya kusadikika kwa kuunganisha dot ukimpelekea Kubenea atakulipa vizuri maana mkiiuza front page mtayakamata manyumbu ya kutosha.
Soma vizuri bandiko langu!

Ni kweli hii ni hekaya ya kusadikika! Kumbuka pia kuna mabilioni ya watu wana hekaya za kusadikika kama kuna Mungu lakini haina maana kuwa hakuna Mungu!

Kubenea ni nani? Nisaidie!
 
No research no right to speak keep quiet and shuuuutt upppp
What is research?
Kuna watu walifanya research na kugundua dunia ni flat!

Kuna wengine wakafanya tena research na kugundua dunia siyo flat!

Hawa wote walikuwa na right to speak.
 
labda. ngoja tusubili tuone kuna nini tena. Make kwa style hii unaweza kusikia wa chenji za rada na wa pesa ya mboga nao wanaula.
 
CCM kumejaa wezi lakino hao jamaa zako wamechagua kwa sababu wanahafathali. Wanakula( Wanaiba) na kupuliza(Wachapakazi) kama panya.
 
Tunachokosea sisi Waafrika ni kuweka akili, mioyo, masikio na matumaini yetu kwenye hizi serikali za viongozi wa Afrika.

Hakuna masiha hata mmoja. Kila mtu anakula kiasi chake.

Bora huo muda uwekeze kwenye shughuli yako ya kutafuta pesa.
 
Unasema werema kapewa ulaji mbona hutwambii ni nafasi gani kapewa? Hii hekaya ya kusadikika kwa kuunganisha dot ukimpelekea Kubenea atakulipa vizuri maana mkiiuza front page mtayakamata manyumbu ya kutosha.
Soma vizuri Ujaji Ulaji??
 
Tulisema tatizo ni mfumo,mnajionea wenyewe
Mkuu kama kiongozi umepata nafasi kwa waliokuwa nawe kutumia ushirikina basi hata wewe uwe mlokole kwenye hilo nawe ni mshirikina tuu. Hivyo hivyo Pesa za wizi au Rushwa na hadaa.
Matokeo ya fedha za ESCROW na kauli zile za Muhongo za kutishia kumwaga Michele na hatimae yeye na Katibu wake kutulizwa no wazi Pesa zile zilipigwa ili zitumike kwenye kampeni.
Hili linaondoa utakatifu anaotaka JPM kujinadi nao eti sijapokea hela ya mfanyabiashara yeyote kwenye kampeni.
Sawa lakini zile Rumbesa za Stanbic ndizo zilikuwa zinamlipia chakula, petrol, posho za watukanaji kina Bulembo, posho za wakata viuno na burudani kina Wema na mengine mengi tuu.
Usafi anaojinadi nao uko wapi?
 
Mkuu kama kiongozi umepata nafasi kwa waliokuwa nawe kutumia ushirikina basi hata wewe uwe mlokole kwenye hilo nawe ni mshirikina tuu. Hivyo hivyo Pesa za wizi au Rushwa na hadaa.
Matokeo ya fedha za ESCROW na kauli zile za Muhongo za kutishia kumwaga Michele na hatimae yeye na Katibu wake kutulizwa no wazi Pesa zile zilipigwa ili zitumike kwenye kampeni.
Hili linaondoa utakatifu anaotaka JPM kujinadi nao eti sijapokea hela ya mfanyabiashara yeyote kwenye kampeni.
Sawa lakini zile Rumbesa za Stanbic ndizo zilikuwa zinamlipia chakula, petrol, posho za watukanaji kina Bulembo, posho za wakata viuno na burudani kina Wema na mengine mengi tuu.
Usafi anaojinadi nao uko wapi?
Ni kweli mkuu watu kwa uzembe wa kushirikisha akili katika maswala walikuwa na matumaini makubwa sana kiasi cha kuwa tayari kugombana na mtu yeyote anayemkosoa Dr.Magufuli lakin kwasasa taratibu wameanza kuelewa,hizo ndio hela za press conference pale SERENA HOTEL..
 
Kurudishwa kwa Prof. Muhongo na pia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi kumezua maswali ambayo yanahitaji majibu mbadala!

Nisingepata maswali kama wangerudishwa na Serikali ya Rais Kikwete kutokana na historia yake kiutendaji lakini ninapatwa na maswali baada ya kurudishwa kwenye nafasi za juu za kisiasa katika serikali ya Rais Magufuli ambayo inajipambanua na nimeiona ni no-nonsense, results-driven government.

Kwa alichokifanya Rais Magufuli na historia aliyonayo ndani ya serikali, uteuzi wa Prof. Muhongo na Maswi unatoa picha nyingine kwenye kadhia ya Tegeta Escrow Account.

Wakati wa sakata la Tegeta Escrow account, Kumbukumbu zinaonyesha Prof. Muhongo aliwahi kusema hawezi kujiudhuru na kama ikitokea hivyo basi nchi itatikisika.Kwa maana nyingine, alikuwa amebeba bomu kubwa la kisiasa ambalo alikuwa tayari kuripua iwapo atashinikizwa kujiudhuru hata hivyo inaonekana alishauriwa na watu wa ‘’kitengo’’, akajiudhuru ili kulinda heshima ya serikali kwa matarajio ya baadaye.

Hata aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi aliwahi kusema hahusiki na sakata hili bali alifanya kazi kama alivyoshauriwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema.

Maswi baada ya kusafishwa na tume ya maadili, aliteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara huku Prof. Muhongo akijikita kutafuta nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea Urais na ubunge kwa tiketi ya CCM.

Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema alikiri hata ndani ya Bunge, kuwa ni kweli kuwa alitoa ushauri kwa mamlaka ya juu ili kuidhinisha fedha kutolewa na kwa maana hiyo yuko tayari kubeba msalaba wa Prof Muhongo na Maswi. Kwa sasa amerudi kwenye kazi yake ya Ujaji.

Mpaka sasa tunachofahamu ni kuwa, pesa zilichukuliwa lakini hatufahamu nani aliyechukua na kuweka kwenye ‘’mifuko ya lambo’’ na lumbesa katika Benki ya Stanbic, lakini kikubwa zaidi, hizo pesa zilienda wapi?

Uchunguzi wa sakata hili mpaka sasa ‘’haujamalizika’’ lakini waliowajibika kisiasa wamerudishwa katika nafasi za juu nchini.

Kwa yanayofanyika kwa sasa, kuna hatari na uwezekano tulikuwa tunacheza ngoma ya kisiasa ambayo hatufahamu mapigo yake achilia mbali wapigaji wake.

Hizi teuzi zinaacha maswali mengi bila majibu!

Ama kweli usilolijua...
 
Kurudishwa kwa Prof. Muhongo na pia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi kumezua maswali ambayo yanahitaji majibu mbadala!

Nisingepata maswali kama wangerudishwa na Serikali ya Rais Kikwete kutokana na historia yake kiutendaji lakini ninapatwa na maswali baada ya kurudishwa kwenye nafasi za juu za kisiasa katika serikali ya Rais Magufuli ambayo inajipambanua na nimeiona ni no-nonsense, results-driven government.

Kwa alichokifanya Rais Magufuli na historia aliyonayo ndani ya serikali, uteuzi wa Prof. Muhongo na Maswi unatoa picha nyingine kwenye kadhia ya Tegeta Escrow Account.

Wakati wa sakata la Tegeta Escrow account, Kumbukumbu zinaonyesha Prof. Muhongo aliwahi kusema hawezi kujiudhuru na kama ikitokea hivyo basi nchi itatikisika.Kwa maana nyingine, alikuwa amebeba bomu kubwa la kisiasa ambalo alikuwa tayari kuripua iwapo atashinikizwa kujiudhuru hata hivyo inaonekana alishauriwa na watu wa ‘’kitengo’’, akajiudhuru ili kulinda heshima ya serikali kwa matarajio ya baadaye.

Hata aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi aliwahi kusema hahusiki na sakata hili bali alifanya kazi kama alivyoshauriwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema.

Maswi baada ya kusafishwa na tume ya maadili, aliteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara huku Prof. Muhongo akijikita kutafuta nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea Urais na ubunge kwa tiketi ya CCM.

Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema alikiri hata ndani ya Bunge, kuwa ni kweli kuwa alitoa ushauri kwa mamlaka ya juu ili kuidhinisha fedha kutolewa na kwa maana hiyo yuko tayari kubeba msalaba wa Prof Muhongo na Maswi. Kwa sasa amerudi kwenye kazi yake ya Ujaji.

Mpaka sasa tunachofahamu ni kuwa, pesa zilichukuliwa lakini hatufahamu nani aliyechukua na kuweka kwenye ‘’mifuko ya lambo’’ na lumbesa katika Benki ya Stanbic, lakini kikubwa zaidi, hizo pesa zilienda wapi?

Uchunguzi wa sakata hili mpaka sasa ‘’haujamalizika’’ lakini waliowajibika kisiasa wamerudishwa katika nafasi za juu nchini.

Kwa yanayofanyika kwa sasa, kuna hatari na uwezekano tulikuwa tunacheza ngoma ya kisiasa ambayo hatufahamu mapigo yake achilia mbali wapigaji wake.

Hizi teuzi zinaacha maswali mengi bila majibu!

Ama kweli usilolijua]
 
Msiyoyajua ni mengi kuliko muyajuayo,HAPPY NEW YEAR.
Inawezekana unayoyasema ni kweli!

Sikuwahi kufikiria hata punje kama viongozi wakuu wa CHADEMA wanaweza kumkaribisha Lowassa na kuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA!

Uteuzi wa Prof. Muhongo na Maswi unagonga vichwa bila majibu!

Siasa za Tanzania siyo kama tuzijuavyo!
 
Back
Top Bottom