Je watu wasiojulikana wana "connection" na vyombo vya dola?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Kumekuwa na matukio mfululizo ya watu kutekwa, na watu tunaoaminishwa na serikali yetu iliyoko madarakani kuwa watu hao ni watu wasiojulikana, matukio ambayo yameongezeka sana katika utawala huu wa awamu ya tano, matukio ambayo hapo siku za nyuma hayakuwepo.

Swali kubwa tunalojiuliza wananchi, je watu hao wasiojulikana, je wana "connection" yoyote na vyombo vya dola, hususani na Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa?

Jibu ambalo naweza kulitoa ni kuwa watu hao tunaoaminishwa kuwa ni watu wasiojulikana ni watu WANAOJULIKANA vizuri sana na vyombo vya dola, hususani na Jeshi letu la Polisi na Usalama wa Taifa.

Nasema hivi nikiangalia namna ambavyo watu wanatekwa, watu wanashambuliwa, huku kitendawili hiki cha watu wasiojulikana kikiwa hakijatatuliwa.

Najua kuwa wajibu mkubwa namba moja wa Jeshi letu la Polisi ni kuwalinda Raia wake na Mali zao.

Sasa inapotokea raia wanaishi kwa hofu kubwa, wasijue ni lini na saa ngapi na wao watatekwa na watu wasiojulikana, ni dhahiri hapo kuwa Jeshi letu la Polisi linaposhindwa kuwabaini watu hao wasiojulikana, basi Jeshi hilo la Polisi, limeshindwa katika wajibu wao namba moja wa kuwalinda raia wake na mali zao na hivyo ni wajibu wa Rais wa nchi awatumbue viongozi wakuu wa Jeshi hilo la Polisi nchini.

Iwapo pia Rais wa nchi haonyeshi dalili yoyote ya kuguswa na yanayoendelea nchini, wananchi tunapata picha kuwa matukio yote yanayotokea nchini yana "baraka" zote za uongozi wa juu hapa nchini

Ni jambo lililothibitishwa kuwa kutokana na "staili" ya utekaji waliofanyiwa mwandishi wa habari Eric Kabendera na hili la hivi majuzi la Tito Magoti kuwa Jeshi letu la Polisi nchini "linahusika" aidha directly au indirectly na matukio ya kutekwa kwa hao niliowataja.

Zipo sababu za kueleza kuwa nimejiridhisha kuwa vyombo hivyo vya dola vinahusika moja kwa moja na utekaji huo.

Tukiangalia matukio yote hayo mawili namna yalivyotekelezwa ni lazima wananchi washuku kuwa vyombo hivyo vya dola, yaani Jeshi letu la Polisi na Usalama wa Taifa, ni vigumu vyombo hivyo vya dola, kujiweka kando na matukio hayo ya utekaji.

Jeshi letu la Polisi linajua taratibu za kumkamata mtu ambaye wanamshuku kuwa ni mhalifu, zikiwemo kujitambulisha kuwa wewe ni askari na uonyeshe kitambuisho chako cha kazi na yule unayemkamata unamweleza sababu za kumshuku kuwa ametenda uhalifu gani wa jinai na pia ni lazima wakati unamkamata uwajulishe jamaa zake wa karibu ni katika kituo kipi cha Polisi ambako unampeleka mtuhumiwa huyo na unawaeleza pia ndugu wa mtyhumiwa huyo kuwa wanaruhusiwa kumteua mwanasheria wao atakayewawakilisha katika kutoa maelezo Polisi.

Ni jambo la ajabu kuwa taratibu zote hizo za kisheria ingawa zinaeleweka wazi na Jeshi letu la Polisi, lakini taratibu zote hizo za ukamataji wa mtuhumiwa zilikiukwa katika kuwakamata watuhumiwa Eric Kabendera na hili la majuzi la Tito Magoti.

Vile vile kujichanganya wanakojichanganya Jeshi letu la Polisi katika kutoa Maelezo ya watu hao wanaowakamata ndiko kunaashiria kuwa Jeshi hilo la Polisi ni "part and parcel" ya watu hao wasiojulikana.

Maoni yangu hayo nayatoa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) ambayo inasema "mtu yoyote yuko huru kutoa maoni yake katika chombo chochote cha habari na mawasiliano yake hayapaswi yaingiliwe kati na chombo chochote kile" mwisho wa kunukuu.
 
Ni jambo linaloshangaza sana kuwa hao wanaokamatwa wanaelezwa makosa mengine ya utata wao wa uraia, lakini wanapofikishwa mahakamani baada ya "mbinde" za wananchi, wanageizuwa kibao kuwa wao ni watakitashaji pesa na wahujumu uchumi!

Taifa linapofanya uonevu wa waziwazi kabisa wa aina hii, linaongeza chuki na visasi ndani ya jamii
 
hakuna mtu asiye na kosa, ikiwa tu wenye mamlaka wakiamua kukuchekecha vema. shida labda ni uvivu wa wanao shughulika na haya mambo na nini kianze.

kwamba uchunguze kwanza na kuainisha makosa ya mtu ndipo umkamate kwa utaratibu mzuri tu. au ukamate halafu uanze mchakato wa kuchunguza ndipo uainishe makosa yake.

panya atakunywa maji ya kumtosha tumbo lake, na tembo hivyo hivyo. jambo la msingi ni kuelewa nafasi yako na mipaka yako.
ufugaji wa nguruwe unaeleweka, usilazimishe kubadilisha utaratibu wake jaribu kuishi kulingana na hayo mazingira.

ni vema ukafikiri vya kutosha kabla haujatenda, kujua athari yake kwako na familia yako. nchi yetu bado changa sana kuhisi kuna watu wataandamana kukutetea. unaweza kushinda vita vya muda mfupi, muda ukipita watu hukusahau.

daima nyumbani kwa shujaa ulindima vilio, na nyumbani kwa muoga ni kicheko.

Hasara Umfika Mwenye Mabezo
 

Mbona wanajulikana kabisa na wanaye msemaji wao ambaye huwa anasema ni lini wataachiwa.
Rejea alipotekwa Mo na hata alipotekwa roma Mkatoliki
That is true

Bashite alitueleza kuwa Mo ametekwa na wa-South Africa, wakati uchunguzi hata bado haujaanza!

Pia alitabiri kuwa Roma Mkatiliki atarejea Jumapili, na kweli ilipofika siku hiyo tukaona watekaji wake wamemuachia!
 
Wasiojulikana ni vyombo vya dola vyenyewe, vyombo vya dola vinapotimiza majukumu yao kwa kufuata maadili ya kazi yao, vinajiita ni vyombo vya dola, vinapobadilisha mfumo wao wa kiutendaji na kuvaa ngozi ya chui asiye na huruma vinajiita ni watu wasiojulikana.
 
Wasiojulikana ni vyombo vya dola vyenyewe, vyombo vya dola vinapotimiza majukumu yao kwa kufuata maadili ya kazi yao, vinajiita ni vyombo vya dola, vinapobadilisha mfumo wao wa kiutendaji na kuvaa ngozi ya chui asiye na huruma vinajiita ni watu wasiojulikana.
Absolutely true
 
hakuna mtu asiye na kosa, ikiwa tu wenye mamlaka wakiamua kukuchekecha vema. shida labda ni uvivu wa wanao shughulika na haya mambo na nini kianze.

kwamba uchunguze kwanza na kuainisha makosa ya mtu ndipo umkamate kwa utaratibu mzuri tu. au ukamate halafu uanze mchakato wa kuchunguza ndipo uainishe makosa yake.

panya atakunywa maji ya kumtosha tumbo lake, na tembo hivyo hivyo. jambo la msingi ni kuelewa nafasi yako na mipaka yako.
ufugaji wa nguruwe unaeleweka, usilazimishe kubadilisha utaratibu wake jaribu kuishi kulingana na hayo mazingira.

ni vema ukafikiri vya kutosha kabla haujatenda, kujua athari yake kwako na familia yako. nchi yetu bado changa sana kuhisi kuna watu wataandamana kukutetea. unaweza kushinda vita vya muda mfupi, muda ukipita watu hukusahau.

daima nyumbani kwa shujaa ulindima vilio, na nyumbani kwa muoga ni kicheko.

Hasara Umfika Mwenye Mabezo
Hivi sijui ni kwa nini watu wengi kama wewe mnathamini familia zenu kuliko jamii nzima utasikia ukafanya hivi utakamatwa utaicha familia yaki.

Hivi hujui kuwa katika dunia hii kuna watu wamezaliwa kwa ajili ya kutetea watu,sasa nakushangaa wewe una wasihi watu waishi kulingana na mazingira yaani maana yake katika utawala huu wote tuwe wa kusifua na kusema ndio mzee.

Lazima utambue duniani watu tupo tofauti sio wote wanaweza kujidhalilisha utu wao kwa kuogopa kwamba atakufa,kuna mwingine yupo tayari kufa akitetea anachokiamini yeye.
 
Watumishi wa Umma wanakuhujumu mchana kweupe sababu wamechoka kudhalilishwa, juhudi zako hazienda kokote. Zaidi ya haya madaraja, hakuna kitakchofanikiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumekuwa na matukio mfululizo ya watu kutekwa, na watu tunaoaminishwa na serikali yetu iliyoko madarakani kuwa watu hao ni watu wasiojulikana, matukio ambayo yameongezeka sana katika utawala huu wa awamu ya tano, matukio ambayo hapo siku za nyuma hayakuwepo

Swali kubwa tunalojiuliza wananchi, je watu hao wasiojulikana, je wana "connection" yoyote na vyombo vya dola, hususani na Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa?

Jibu ambalo naweza kulitoa ni kuwa watu hao tunaoaminishwa kuwa ni watu wasiojulikana ni watu WANAOJULIKANA vizuri sana na vyombo vya dola, hususani na Jeshi letu la Polisi na Usalama wa Taifa

Nasema hivi nikiangalia namna ambavyo watu wanatekwa, watu wanashambuliwa, huku kitendawili hiki cha watu wasiojulikana kikiwa hakijatatuliwa.

Najua kuwa wajibu mkubwa namba moja wa Jeshi letu la Polisi ni kuwalinda Raia wake na Mali zao.

Sasa inapotokea raia wanaishi kwa hofu kubwa, wasijue ni lini na saa ngapi na wao watatekwa na watu wasiojulikana, ni dhahiri hapo kuwa Jeshi letu la Polisi linaposhindwa kuwabaini watu hao wasiojulikana, basi Jeshi hilo la Polisi, limeshindwa katika wajibu wao namba moja wa kuwalinda raia wake na mali zao na hivyo ni wajibu wa Rais wa nchi awatumbue viongozi wakuu wa Jeshi hilo la Polisi nchini

Iwapo pia Rais wa nchi haonyeshi dalili yoyote ya kuguswa na yanayoendelea nchini, wananchi tunapata picha kuwa matukio yote yanayotokea nchini yana "baraka" zote za uongozi wa juu hapa nchini

Ni jambo lililothibitishwa kuwa kutokana na "staili" ya utekaji waliofanyiwa mwandishi wa habari Eric Kabendera na hili la hivi majuzi la Tito Magoti kuwa Jeshi letu la Polisi nchini "linahusika" aidha directly au indirectly na matukio ya kutekwa kwa hao niliowataja

Zipo sababu za kueleza kuwa nimejiridhisha kuwa vyombo hivyo vya dola vinahusika moja kwa moja na utekaji huo

Tukiangalia matukio yote hayo mawili namna yalivyotekelezwa ni lazima wananchi washuku kuwa vyombo hivyo vya dola, yaani Jeshi letu la Polisi na Usalama wa Taifa, ni vigumu vyombo hivyo vya dola, kujiweka kando na matukio hayo ya utekaji

Jeshi letu la Polisi linajua taratibu za kumkamata mtu ambaye wanamshuku kuwa ni mhalifu, zikiwemo kujitambulisha kuwa wewe ni askari na uonyeshe kitambuisho chako cha kazi na yule unayemkamata unamweleza sababu za kumshuku kuwa ametenda uhalifu gani wa jinai na pia ni lazima wakati unamkamata uwajulishe jamaa zake wa karibu ni katika kituo kipi cha Polisi ambako unampeleka mtuhumiwa huyo na unawaeleza pia ndugu wa mtyhumiwa huyo kuwa wanaruhusiwa kumteua mwanasheria wao atakayewawakilisha katika kutoa maelezo Polisi

Ni jambo la ajabu kuwa taratibu zote hizo za kisheria ingawa zinaeleweka wazi na Jeshi letu la Polisi, lakini taratibu zote hizo za ukamataji wa mtuhumiwa zilikiukwa katika kuwakamata watuhumiwa Eric Kabendera na hili la majuzi la Tito Magoti

Vile vile kujichanganya wanakojichanganya Jeshi letu la Polisi katika kutoa Maelezo ya watu hao wanaowakamata ndiko kunaashiria kuwa Jeshi hilo la Polisi ni "part and parcel" ya watu hao wasiojulikana

Maoni yangu hayo nayatoa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) ambayo inasema "mtu yoyote yuko huru kutoa maoni yake katika chombo chochote cha habari na mawasiliano yake hayapaswi yaingiliwe kati na chombo chochote kile" mwisho wa kunukuu
Waulize Red brigade Wameambiwa wafanye ili kupata ya kuzungumza kwenye Siasa.
 
vita ambavyo matokeo yake ni kwenda kushindwa ni vema vikaepukwa, au kuahirishwa ukijipanga upya. kupigana vita ambavyo vitaacha mafuvu uwanjani pako ni kutowajali watu wako wa karibu.

kama hauwezi kuilinda familia yako, unatoa wapi ujasiri wa kuilinda dunia?

ndio maana namuheshimu sana Mbowe, alikuwa sahihi kuomba maridhiano na watawala.

tofauti na hivyo, kilio cha samaki
Hivi sijui ni kwa nini watu wengi kama wewe mnathamini familia zenu kuliko jamii nzima utasikia ukafanya hivi utakamatwa utaicha familia yaki.

Hivi hujui kuwa katika dunia hii kuna watu wamezaliwa kwa ajili ya kutetea watu,sasa nakushangaa wewe una wasihi watu waishi kulingana na mazingira yaani maana yake katika utawala huu wote tuwe wa kusifua na kusema ndio mzee.

Lazima utambue duniani watu tupo tofauti sio wote wanaweza kujidhalilisha utu wao kwa kuogopa kwamba atakufa,kuna mwingine yupo tayari kufa akitetea anachokiamini yeye.

Hasara Umfika Mwenye Mabezo
 
vita ambavyo matokeo yake ni kwenda kushindwa ni vema vikaepukwa, au kuahirishwa ukijipanga upya. kupigana vita ambavyo vitaacha mafuvu uwanjani pako ni kutowajali watu wako wa karibu.

kama hauwezi kuilinda familia yako, unatoa wapi ujasiri wa kuilinda dunia?

ndio maana namuheshimu sana Mbowe, alikuwa sahihi kuomba maridhiano na watawala.

tofauti na hivyo, kilio cha samaki


Hasara Umfika Mwenye Mabezo
Wewe una maana kuwa watu waone kutekwa kwa watu ambako kunafahamika kuwa kunafanywa na vyombo vya dola, halafu wakae kimya!
 
Wewe una maana kuwa watu waone kutekwa kwa watu ambako kunafahamika kuwa kunafanywa na vyombo vya dola, halafu wakae kimya!

Muhimu kujiangalia upya na kutafuta njia tofauti ya kupata ufumbuzi, maana njia ya kutokaa kimya haijasaidia
 
Mkuu General Akudo, watu tunapaza sauti ili vitendo hivi vya kiounevu vikomeshwe nchini kwetu
Sina nia ovu wala sifurahii vitendo vya kidhalimu, lakini najaribu kuona hizi harakati manufaa yake ni nini?

kwa sababu Tito Magoti siku kadhaa nyuma alikuwa akishiriki hashtag freeIdrissaSultan leo ni yeye.

hakuna unafuu watu wanasombwa tu
 
Back
Top Bottom