Je wajua?

kamili

JF-Expert Member
Feb 10, 2011
1,213
849
Je wajua kwamba sigara ina zaidi ya kemikali 400 zinazoweza sababisha saratani? Je wajua kuwa mvuta sigara ana uwezekano wa mara 15 zaidi ya kupata satani ya mapafu kuliko asiyevuta? Lakini Je wajua anayemaliza paketi moja ya sigara kwa siku ana uwezekano mara 25 zaidi wa kupata saratani ya mapafu kuliko asiyevuta. Je wajua mvuta sigara akiacha itamchukua miaka 15 zaidi kuondokana na hatari zilizokuwa zikimkabili kama alikuwa hajazipata? Je wajua kama unakaa karibu na mvuta sigara bila kujijua unavutishwa sigara (passive smokers)? na unahatari ya kupata saratani mara 2 zaidi ya mtuasiyevuta? Najua utachukua hatua.
 
Back
Top Bottom