Je, wajua Rais aweza kuteua yeyote hata darasa la saba?. Teuzi hizi hazihojiwi popote na yeyote!

Wanabodi,

Bandiko hili ni kufuatia watu fulani humu wenye vimbelembele kutaka kuhoji kila kitu sasa wameingilia kuhoji uwezo wa serikali ya JPM vetting kabla ya teuzi fulani fulani, hawajui kuwa vetting is nothing!, rais ana mamlaka ya kumteua yoyote regardless vetting imesema nini, na hauhusiwi kuhojiwa na yeyote!.

Hii ni kufuatia tabia ya baadhi ya wana jf kuhoji kila kitu, ama kwa kujua, ama kwa kutokujua, sasa sii wengi wanaojua kuhusu mamlaka ya rais ya uteuzi, anaweza kumteua mtu yoyote, mwenye elimu yoyote, hata ya darasa la saba, katika nafasi yoyote, bila kuwa sifa zozote, au kwa vigezo vyovyote, bila kuhojiwa na mamlaka yoyote, au mtu yoyote, popote!, who are you jf members kuhoji mamlaka ya rais ya uteuzi!.

Moja ya sifa kuu za jf ni kuelimishana, katika kuelimishana huku, tunajikuta tunasaidiana kwa kuongezeana maarifa kwa mambo watu wasioyajua.


Mamlaka ya rais ya uteuzi inaitwa presidential appointment powers ambapo katiba yetu yetu imempa mamlaka rais wetu kumteua mtu yoyote kwenye nafasi yoyote, bila kufuata ushauri wa yeyote, na bila kuhitajika kutoa sababu zozote kwa yeyote.

Ukiondoa teuzi ambazo rais anapaswa kuwateua watu wenye sifa fulani maalum, zilizoainishwa, mfano Jaji Mkuu lazima awe mwanasheria, Mwenyekiti wa NEC lazima awe Jaji Mstaafu, CDF lazima awe ni mwanajeshi, IGP lazima awe polisi, Director wa TISS lazima awe ni "wale jamaa", Msajili wa vyama ni Jaji, CAG mtu wa mahesabu, au wakurugenzi wakuu wa taasisi za umma katika positions za utendaji, lazima wawe na sifa fulani za kielimu na kitaaluma, lakini katika positions za kisiasa, rais anaweza kumteua yoyote, kwa kumuokota popotena bado akawa yuko right. Hivyo hizi kelele za mkuu wa mkoa fulani kufoji cheti, kufoji jina au kutokusoma sekondari, hata ikikutikana ni yote yanayosemwa kuhusu elimu ya mkuu huyo ni ya kuunga unga, bado uteuzi wake unabaki kuwa ni halali, kwa sababu ana deliver, na sio majina wala sio macheti!.

Sifa za Kuteuliwa na Rais.
Sifa kuu pekee za mtu kuteuliwa na rais kuwa mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa au mbunge wa kuteuliwa au nafasi nyingine yoyote ya uongozi na sio ya utendaji, wakiwemo wenyeviti wa bodi mbalimbali ni
1. Kuwa Mtanzania
2. Kutimiza umri wa miaka 18
3. Kujua kusoma na kuandika.

Hivyo rais ana mamlaka ya kumteua mtu yoyote mwenye sifa hizo, kwa kushauriana na mamlaka elekezi, kuwa mkuu wa mkoa, au mkuu wa wilaya, au uteuzi mwingine wowote, hivyo rais yuko very right hata kuteua mtu wa darasa la saba, hivyo hata ikitokea, ikathibitishwa mteuliwa fulani aliishia darasa la saba, bado uteuzi wake ni halali.

Rais Halazimishwi Kupokea Ushauri Wowote kwa Yeyote. na ana Haki ya Kuupuuza Ushauri Wowote
Rais wetu, ana wasaidizi mbalimbali kuanzia Makamo wa rais, waziri mkuu, mawaziri, wataalamu mbalimbali wanaomshauri kwenye kila nyaja.

Katika powers za rais za uteuzi, katiba inampa mamlaka rais kabla ya kuteua baadhi ya watu, atashauriana na fulani, mfano uteuzi wa Waziri Mkuu, rais atashauriana na Makamo wa Rais. Wakurugenzi wa bodi, na wakuu wa taasisi za umma, rais atashauriana na mawaziri husika

Kazi ya washauri wote hawa ni kushauri tuu, na sio kumlazimisha rais kufuata ushauri. Hivyo katiba imempa rais mamlaka ya kupokea ushauri wowote, au kutopokea ushauri wowote ikiwepo mamlaka ya kupuuza ushauri wowote na rais akaamua vyovyote yeye mwenyewe na bado yuko right.

Zoezi la Uhakiki wa Vyeti Kwa Watumishi wa Umma.
Zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma, linawahusu waajiriwa wote wa utumishi wa umma, ambao ajira zao, ziliwahitaji kuwa sifa na vigezo vya elimu ya kiwango fulani,ili waweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu, lakini zoezi hili haliwahusu wateule wa rais kwa sababu mamlaka ya rais kufanya uteuzi wowote, haukuweka sifa wala vigezo vya rais kuteua, hivyo rais anaweza kuteua hata mtu asiyejua kusoma wala kuandika, na akamuwekea mtu wa kumsomea na kumuandikia, yeye kazi yake ikabaki kusaini kwa dole gumba na bado rais akawa yuko right.

Waliohitimu Vyuo Vikuu Kwa Majina ya Wengine.
Elimu ya Chuo Kikuu anayeipata ni mtu yule aliyehudhuria masomo, na jina la yule alihudhuria, na anayehesabika aliyehiti ni yule mtu na sio lile jina, jina niutambulisho tuu, mfano mimi Paskali, nilipokuwa mdogo niliitwa Kashinde, jina la utotoni, nikaandikishwa shule kwa jina la ubatizo Paskali. Nikajiunga chuo kikuu kwa jina la Kiti Moto, na nikahitimu kama Kiti Moto, mwenye hiyo elimu ni mimi in person, regardless natumia jina gani, au nilitumia jina gani, kilichohitimu ni mimi na sio jina, hivyo naweza kwenda kwa wakili yoyote nikatengeneza affidavit ya kubadili jina na kutumia jina lolote, hivyo jina doesn't matter, haijalishi kama nilisoma sekondari au sikusoma, lakini nikaingia chuo kikuu na kuhitimu, mimi ni mhitimu wa chuo kikuu kwa the end justifies the means.

Hivyo nawaomba watu humu jf, msihamanike sana na majina ya watu waliotumia, ama kama walisoma sekondari au laa, as long as waliohitimu chuo kikuu ni wahitimu halali wa chuo kikuu na kuteuliwa kushika wadhifa wowote ni halali.

Paskali.

Swala si ikiteuliwa Bali konda ashtakiwe kwa kigushi vyeti,hilo ndo kosa pekee LA huyu kinda wa UDART
 
Daaa!!!! Mkuu hapa umeniacha nikishangaa,

Mfano; mimi ni jina langu ni Jiwe kidato cha nne nikawa nimezungurusha hapo nitakua nimepoteza sifa ya kuendelea na masomo ya juu, halafu rafiki yangu anaitwa Sukari amepata div. one tuseme ya point 7 , lakini kwa sababu mbalimbali za kimaisha akashindwa kuendelea na masomo, mimi nikamshawishi anipatie cheti chake nae akakubali hicho cheti nikapeleka labda tuseme TIA kusoma cheti cha uhasibu, nikafanikiwa kupata nafasi na nikafaulu, hapo kwa maelezo uliyotoa ni sahihi kwako, mimi naona kwa upande wangu si sahihi, na sababu inayonifanya niseme si sahihi ni kwamba nimedanganya kwa kutumia matokeo ya mtu mwingine kupata nafasi ya masomo, na moja kati ya sifa ya kusoma uhasibu ni uadilifu nikigundulika nitapokonywa vyeti vyote.

Suala lilopo mbele yetu halihusiani na uteuzi wa Makonda, suala hapa ni uadilifu wa kiongozi kufoji vyeti na kama kweli amefoji (mimi sina hakika) hiyo pekee inamuondelea sifa ya kuteuliwa.
 
shida ni kufoji .it is criminal act! kuongozwa na muhalifu atakemea vipi uhalifu? he must be in jail and not in public office using our resources!
Ha ha ha! Halafu nikiona ile misfara yake ya ma-V8 ya nguvu na ulinzi wa makomandoo wa kutosha huwa nachoka kabisa.
 
Kuanzia Leo na SAA hii; kwa mamlaka niliyonayo "namtangaza rasmi, PASCAL MAYALA @ Pasco kuwa janga la Jf." Hatuwezi kuendelea kukuheshimu wakati heshima unavunja mwenyewe kwa post zisizo na kiwango kama hii. Potelea mbali kama utachukia, lakini najua siko peke yangu , naamini wenye kujitambua tuko wengi humu na tutakususia posts zako kama tulivyofanya kwa wengine wanaotetea upuuzi hasa ukiwa umetendwa na wa upande wao.

Wazee wenzie walishampuuza toka muda humu, amebakia tuokote sisi tu.
Anajifanya yuko Neutral.

Kujifanya hauna upande uko neutral kwenye maovu ni kuwa wewe umechagua kuwa upande wa maovu.
 
Hivi Pascal unatuona sisi majuha, tunachohoji ni Makonda kufoji cheti au kutumia cheti ambacho sio chake hatuhoji uwezo wa rais kumteua Makonda.

Eti rais anaweza kuokota yeyote unataka kusema kamuokota Makonda.
 
Wanabodi,

Bandiko hili ni kufuatia watu fulani humu wenye vimbelembele kutaka kuhoji kila kitu sasa wameingilia kuhoji uwezo wa serikali ya JPM vetting kabla ya teuzi fulani fulani, hawajui kuwa vetting is nothing!, rais ana mamlaka ya kumteua yoyote regardless vetting imesema nini, na hauhusiwi kuhojiwa na yeyote!.

Hii ni kufuatia tabia ya baadhi ya wana jf kuhoji kila kitu, ama kwa kujua, ama kwa kutokujua, sasa sii wengi wanaojua kuhusu mamlaka ya rais ya uteuzi, anaweza kumteua mtu yoyote, mwenye elimu yoyote, hata ya darasa la saba, katika nafasi yoyote, bila kuwa sifa zozote, au kwa vigezo vyovyote, bila kuhojiwa na mamlaka yoyote, au mtu yoyote, popote!, who are you jf members kuhoji mamlaka ya rais ya uteuzi!.

Moja ya sifa kuu za jf ni kuelimishana, katika kuelimishana huku, tunajikuta tunasaidiana kwa kuongezeana maarifa kwa mambo watu wasioyajua.


Mamlaka ya rais ya uteuzi inaitwa presidential appointment powers ambapo katiba yetu yetu imempa mamlaka rais wetu kumteua mtu yoyote kwenye nafasi yoyote, bila kufuata ushauri wa yeyote, na bila kuhitajika kutoa sababu zozote kwa yeyote.

Ukiondoa teuzi ambazo rais anapaswa kuwateua watu wenye sifa fulani maalum, zilizoainishwa, mfano Jaji Mkuu lazima awe mwanasheria, Mwenyekiti wa NEC lazima awe Jaji Mstaafu, CDF lazima awe ni mwanajeshi, IGP lazima awe polisi, Director wa TISS lazima awe ni "wale jamaa", Msajili wa vyama ni Jaji, CAG mtu wa mahesabu, au wakurugenzi wakuu wa taasisi za umma katika positions za utendaji, lazima wawe na sifa fulani za kielimu na kitaaluma, lakini katika positions za kisiasa, rais anaweza kumteua yoyote, kwa kumuokota popotena bado akawa yuko right. Hivyo hizi kelele za mkuu wa mkoa fulani kufoji cheti, kufoji jina au kutokusoma sekondari, hata ikikutikana ni yote yanayosemwa kuhusu elimu ya mkuu huyo ni ya kuunga unga, bado uteuzi wake unabaki kuwa ni halali, kwa sababu ana deliver, na sio majina wala sio macheti!.

Sifa za Kuteuliwa na Rais.
Sifa kuu pekee za mtu kuteuliwa na rais kuwa mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa au mbunge wa kuteuliwa au nafasi nyingine yoyote ya uongozi na sio ya utendaji, wakiwemo wenyeviti wa bodi mbalimbali ni
1. Kuwa Mtanzania
2. Kutimiza umri wa miaka 18
3. Kujua kusoma na kuandika.

Hivyo rais ana mamlaka ya kumteua mtu yoyote mwenye sifa hizo, kwa kushauriana na mamlaka elekezi, kuwa mkuu wa mkoa, au mkuu wa wilaya, au uteuzi mwingine wowote, hivyo rais yuko very right hata kuteua mtu wa darasa la saba, hivyo hata ikitokea, ikathibitishwa mteuliwa fulani aliishia darasa la saba, bado uteuzi wake ni halali.

Rais Halazimishwi Kupokea Ushauri Wowote kwa Yeyote. na ana Haki ya Kuupuuza Ushauri Wowote
Rais wetu, ana wasaidizi mbalimbali kuanzia Makamo wa rais, waziri mkuu, mawaziri, wataalamu mbalimbali wanaomshauri kwenye kila nyaja.

Katika powers za rais za uteuzi, katiba inampa mamlaka rais kabla ya kuteua baadhi ya watu, atashauriana na fulani, mfano uteuzi wa Waziri Mkuu, rais atashauriana na Makamo wa Rais. Wakurugenzi wa bodi, na wakuu wa taasisi za umma, rais atashauriana na mawaziri husika

Kazi ya washauri wote hawa ni kushauri tuu, na sio kumlazimisha rais kufuata ushauri. Hivyo katiba imempa rais mamlaka ya kupokea ushauri wowote, au kutopokea ushauri wowote ikiwepo mamlaka ya kupuuza ushauri wowote na rais akaamua vyovyote yeye mwenyewe na bado yuko right.

Zoezi la Uhakiki wa Vyeti Kwa Watumishi wa Umma.
Zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma, linawahusu waajiriwa wote wa utumishi wa umma, ambao ajira zao, ziliwahitaji kuwa sifa na vigezo vya elimu ya kiwango fulani,ili waweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu, lakini zoezi hili haliwahusu wateule wa rais kwa sababu mamlaka ya rais kufanya uteuzi wowote, haukuweka sifa wala vigezo vya rais kuteua, hivyo rais anaweza kuteua hata mtu asiyejua kusoma wala kuandika, na akamuwekea mtu wa kumsomea na kumuandikia, yeye kazi yake ikabaki kusaini kwa dole gumba na bado rais akawa yuko right.

Waliohitimu Vyuo Vikuu Kwa Majina ya Wengine.
Elimu ya Chuo Kikuu anayeipata ni mtu yule aliyehudhuria masomo, na jina la yule alihudhuria, na anayehesabika aliyehiti ni yule mtu na sio lile jina, jina niutambulisho tuu, mfano mimi Paskali, nilipokuwa mdogo niliitwa Kashinde, jina la utotoni, nikaandikishwa shule kwa jina la ubatizo Paskali. Nikajiunga chuo kikuu kwa jina la Kiti Moto, na nikahitimu kama Kiti Moto, mwenye hiyo elimu ni mimi in person, regardless natumia jina gani, au nilitumia jina gani, kilichohitimu ni mimi na sio jina, hivyo naweza kwenda kwa wakili yoyote nikatengeneza affidavit ya kubadili jina na kutumia jina lolote, hivyo jina doesn't matter, haijalishi kama nilisoma sekondari au sikusoma, lakini nikaingia chuo kikuu na kuhitimu, mimi ni mhitimu wa chuo kikuu kwa the end justifies the means.

Hivyo nawaomba watu humu jf, msihamanike sana na majina ya watu waliotumia, ama kama walisoma sekondari au laa, as long as waliohitimu chuo kikuu ni wahitimu halali wa chuo kikuu na kuteuliwa kushika wadhifa wowote ni halali.

Paskali.

Kwenye swala LA chuo kikuu Bro umechemka vibaya. Dishonesty na cheating ndio dhambi kubwa kuliko zote vyuoni.
 
Katika dunia ya leo ya karne ya 21 ya sayansi na teknolojia, kama rais anaweza kumteua STD VII, simply kwasababu eti uteuzi wake hauwezi kuhojiwa na mtu/chombo chochote. Hao STD VII ndiyo awategemee kuifanya nchi ya viwanda, basi huyo Rais atakuwa na matatizo makubwa kuliko hao akina Kayumba aka STD VII!
 
Ukiona una maadui wengi basi mshukuru Mungu kwa sababu unaogopwa.

Makonda anaogopwa, na sio kuogopwa tu, bali wapo ambao wanajaribu kuwatetea wale ambao walionekana ni wasafi kumbe sio lolote.

Makonda fanya kazi kwa nguvu zako zote, hizi mbwembwe za elimu na vyeti wakati Tanzania inashindwa hata kutengeneza kijiko, hazina maana yoyote.
 
Hapa jukwaani huenda mimi pekee ndo mwenye elimu ya darasa la saba.Huwa nashangaa inakuwaje wasomi mnashindwa kumuelewa Pasco na mimi wa darasa la saba namuelewa vizuri tu?
Watu wanaoandika ujumbe kwa njia ya Pasco ni adimu sana so usishangae kama wangekua wamewahi kuwasoma akina Ndimara na Mabala wangemuelewa haraka
 
Ukiona una maadui wengi basi mshukuru Mungu kwa sababu unaogopwa.

Makonda anaogopwa, na sio kuogopwa tu, bali wapo ambao wanajaribu kuwatetea wale ambao walionekana ni wasafi kumbe sio lolote.

Makonda fanya kazi kwa nguvu zako zote, hizi mbwembwe za elimu na vyeti wakati Tanzania inashindwa hata kutengeneza kijiko, hazina maana yoyote.
Na kwako wewe kuogopwa ni sifa nzuri!!
 
Back
Top Bottom