Je wajua kwamba ishara ya kwanza ya Ukristo ilikuwa samaki sio Msalaba

Je wajua kwamba ishara ya kwanza ya Ukristo ilikuwa samaki sio Msalaba

Covax

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2021
Posts
13,555
Reaction score
40,749
Ni jambo linalojulikana wazi (kwa mujibu wa Groliers, “Bible Myths,” n.k.) kwamba ishara ya kwanza ya Ukristo ilikuwa samaki.

Katika vikombe vya sakramenti, mihuri, na taa, Roho Mtakatifu aliwakilishwa kwa ishara ya njiwa, Na Kristo aliwakilishwa na samaki (pengine kwa sababu wakati huo samaki walikuwa sehemu ya mlo mtakatifu) au mchungaji anayebeba kondoo mabegani mwake (Luka 15:3-7).

Msalaba haukuanza kutumika hadi muda mrefu baada ya kuondoka kwa Yesu. Moja ya sababu kuu ilikuwa kwamba anayekufa kwa msalaba alionekana kama amelaaniwa na Mungu (Wagalatia 3:13).

Maarifa ya kihistoria ya sasa yanatambua kwamba msalaba ulitambulika kama ishara ya kidini hata kabla ya ujio wa Yesu (rehma ziwe juu yake). Uliabudiwa India kama ishara ya mungu wa Kihindu aitwaye Agni, “nuru ya dunia.” Uliwekwa mikononi mwa Siva, Brahma, Vishnu, Krishna, Tvashtri, na Jama.

Msalaba pia ulifahamika miongoni mwa Wabudha tangu enzi za kale, na wafuasi wa Lama wa Tibet.

Wamisri wa kale pia walitumia msalaba kama ishara ya kidini ya miungu yao ya kipagani. Michoro mingi ya Wamisri inaonyesha watu wakishika misalaba mikononi mwao. Miongoni mwao, mkombozi wao Horus anaonyeshwa akishika msalaba. Pia huonyeshwa akiwa mtoto mdogo ameketi kwenye goti la mama yake na msalaba kwenye kiti chao.
Miongoni mwa misalaba maarufu iliyotumiwa na Wamisri hao wa kipagani ni Crux Ansata, ambayo baadaye ilichukuliwa na Wakristo.

Mkombozi wa Wamisri, Osiris — mungu wa wafu na wa ulimwengu wa chini wakati mwingine huonyeshwa akiwapa wanadamu msalaba huu kama ishara ya kuwa wameachana na maisha ya kufa na sasa wanaingia kwenye maisha yajayo.

Msalaba mwingine uligunduliwa Ireland. Ulitoka kwenye ibada ya mungu wa jua wa Kiajemi, Mithra, na unaonyesha mfano wa mtu aliyesulubiwa. Wagiriki na Warumi pia walitumia msalaba kama ishara ya kidini karne nyingi kabla Ukristo haujaanza kufanya hivyo.

Maandishi ya kale huko Tessaly yanaambatana na msalaba wa Calvary. Msalaba zaidi walipatikana pia ukipamba kaburi la mfalme Midas huko Frigia.

Hii inaonyesha kwamba matumizi ya msalaba kama ishara ya kidini yalitangulia sana Ukristo. Kwa hiyo, inazua hoja ya iwapo msalaba ni alama ya kipekee ya Ukristo au ni urithi kutoka kwa tamaduni za zamani za kipagani?
Uchambuzi wa kihistoria kama huu unafaa kuchochea fikra huru na utafiti wa kina juu ya asili ya alama tunazoamini.
Screenshot_20250713-090554_WhatsApp.jpg
 
Ni debate kwa namna unavyowasilisha mada zako
Kama wewe unaona maalifa kwa jicho la debate pia ni sawa kwahiyo leta upande wasko kwasbabu ina pande mbili.
 
Ni jambo linalojulikana wazi (kwa mujibu wa Groliers, “Bible Myths,” n.k.) kwamba ishara ya kwanza ya Ukristo ilikuwa samaki.

Katika vikombe vya sakramenti, mihuri, na taa, Roho Mtakatifu aliwakilishwa kwa ishara ya njiwa, Na Kristo aliwakilishwa na samaki (pengine kwa sababu wakati huo samaki walikuwa sehemu ya mlo mtakatifu) au mchungaji anayebeba kondoo mabegani mwake (Luka 15:3-7).

Msalaba haukuanza kutumika hadi muda mrefu baada ya kuondoka kwa Yesu. Moja ya sababu kuu ilikuwa kwamba anayekufa kwa msalaba alionekana kama amelaaniwa na Mungu (Wagalatia 3:13).

Maarifa ya kihistoria ya sasa yanatambua kwamba msalaba ulitambulika kama ishara ya kidini hata kabla ya ujio wa Yesu (rehma ziwe juu yake). Uliabudiwa India kama ishara ya mungu wa Kihindu aitwaye Agni, “nuru ya dunia.” Uliwekwa mikononi mwa Siva, Brahma, Vishnu, Krishna, Tvashtri, na Jama.

Msalaba pia ulifahamika miongoni mwa Wabudha tangu enzi za kale, na wafuasi wa Lama wa Tibet.

Wamisri wa kale pia walitumia msalaba kama ishara ya kidini ya miungu yao ya kipagani. Michoro mingi ya Wamisri inaonyesha watu wakishika misalaba mikononi mwao. Miongoni mwao, mkombozi wao Horus anaonyeshwa akishika msalaba. Pia huonyeshwa akiwa mtoto mdogo ameketi kwenye goti la mama yake na msalaba kwenye kiti chao.
Miongoni mwa misalaba maarufu iliyotumiwa na Wamisri hao wa kipagani ni Crux Ansata, ambayo baadaye ilichukuliwa na Wakristo.

Mkombozi wa Wamisri, Osiris — mungu wa wafu na wa ulimwengu wa chini wakati mwingine huonyeshwa akiwapa wanadamu msalaba huu kama ishara ya kuwa wameachana na maisha ya kufa na sasa wanaingia kwenye maisha yajayo.

Msalaba mwingine uligunduliwa Ireland. Ulitoka kwenye ibada ya mungu wa jua wa Kiajemi, Mithra, na unaonyesha mfano wa mtu aliyesulubiwa. Wagiriki na Warumi pia walitumia msalaba kama ishara ya kidini karne nyingi kabla Ukristo haujaanza kufanya hivyo.

Maandishi ya kale huko Tessaly yanaambatana na msalaba wa Calvary. Msalaba zaidi walipatikana pia ukipamba kaburi la mfalme Midas huko Frigia.

Hii inaonyesha kwamba matumizi ya msalaba kama ishara ya kidini yalitangulia sana Ukristo. Kwa hiyo, inazua hoja ya iwapo msalaba ni alama ya kipekee ya Ukristo au ni urithi kutoka kwa tamaduni za zamani za kipagani?
Uchambuzi wa kihistoria kama huu unafaa kuchochea fikra huru na utafiti wa kina juu ya asili ya alama tunazoamini.View attachment 3403977
Tumia akili alama ya msalaba ni kumbukizi tu ya kusulubiwa kwa yesu msalabani siyo kila msalaba ni mwema ndiyo maana walisulibiwa na wahalifu wawili misalabani .
 
Tumia akili alama ya msalaba ni kumbukizi tu ya kusulubiwa kwa yesu msalabani siyo kila msalaba ni mwema ndiyo maana walisulibiwa na wahalifu wawili misalabani .
Kwani mimi nimesemaje mkuu, mbona umekurupuka kasome upate kujua historia ya ishara ya msalaba mkuu, tulia.
 
Kwani mimi nimesemaje mkuu, mbona umekurupuka kasome upate kujua historia ya ishara ya msalaba mkuu, tulia.
Sasa unasema ilianza alama ya samaki wakati kumbukizi ya msalaba ilikuwepo toka kusulibiwa kwa yesu ulitakiwa kusema alama mojawapo ya wakristo wa madhehebu ya dini ni samaki ...kumbuka niliwaambia watu ujio wa madhehebu maana yake ni upotovu. Madhehebu ni mahekalu ya shetani mungu hato kuja kufanya madhehebu kwa maana hata Yesu kasema UFALME ULIO FARAKANA HAUTA SIMAMA ...Madhehebu maana yake ni mafarakano.
 
Nitakuelezea kidogo kwa misingi ya Biblia, ambayo ninaamini unaiamini ndio maana umekiri kuja duniani na kusulubiwa kwa Kristo kwenye aya ya kwanza ya maelezo yako.

Tukianza na huo mstari uliourejelea, Gal 3:13 unaanza na maelezo mengine kabla ya kurejea (quote) maelezo ya Kumb: 21:23 yanayoelezea hiyo laana. Kwa lugha rahisi kama ulitaka kuelezea laana ya msalaba, basi ungefanya rejea ya Kumbukumbu la Torati, ambapo huo mstari ndio unaeleza kuwa Mtu akitenda dhambi akauawa na kutundikwa juu ya mti, basi mzoga wake usikae usiku kucha kwasababu anakua amelaaniwa kwa kutundikwa juu ya mti kama mdhambi.

Lakini mstari uliourejelea (Gal 3:13), unaeleza kinyume chake. Paulo anatuambia kuwa Kristo alitukomboa kutoka katika laana ya Torati (maana yake alilazimika kufanyiwa vile ambavyo mtu alieadhaniwa kuwa mwenye laana zaidi anatendewa, ikiwa yeye anaaminika ni Mtakatifu ili kuonesha kwamba hakuna kitu kinachoweza kuwakilisha hali ya laana kwa mtu).

Katika maisha yetu ya kila siku tuna watu ambao tunawachukulia kama mifano yetu ama miongozo yetu katika imani, siasa, elimu na teknolojia. Mara nyingi wanapofanya vitu ambavyo sisi tulihofia kuvifanya basi tunaondoa ile hofu na kupata imani na mtazamo mpya juu ya hivyo vitu. Mfano ni namna tunavyoiga mitindonya maisha, namna wanasiasa wanavyoshiriki katika matukio mbalimbali yenye muonekano wa hali ya chini ili kutuaminisha wapo sawa na sisi, namna ambavyo tunatarajia viongozi wetu wa dini waishi kama mifano yetu ya Utakatifu.

Kwa mtazamo huo huo, ndipo Paulo anatuambia kwamba, kile tulichoamini ni laana katika Torati, kimefutwa na alietoka juu kuja kukaa nasi. Maana isingewezekana Mungu neno aliekingiwa dhambi ya asili tangu kizazi chake cha nyuma, aje kunajisiwa na wanadamu.

Kuhusu kuutumia mslaba kama ishara ya Ukristo, haijalishi ilichelewa kiasi gani na haijalishi hapo mwanzo msalaba uliwakilisha nini, lakini ukweli unabaki kwamba, Kristo mwenyewe aliainisha ili uwe mfuasi wake (Mkristo) ni lazima ubebe msalaba na kumfuata. Math 16:24, Luk 9:23, Mark 15:30

Ukibahatika kwenda shule, ukimaliza ukataka kupatiwa ajira inayoendana na shule yako basi watataka uwaoneshe uthibitisho wa wewe kwenda shule, hapo hawatahitaji uwaletee mkanda wa video unaoonesha kuwa wewe umekua ukihudhuria vipindi, bali alama pekee unayopewa kuwakilisha shule yako. Vivyo hivyo kwenye harakati zetu zote za maisha, kila mahali utatakiwa kuonesha alama fulani inayoonesha kuwa unastahili kuwepo eneo hilo.

Kutokana na Kristo kutuamuru tubebe msalaba (ambao ki maantiki alimaanisha kukubali kuteseka) basi na sisi tunaona ni sawa kabisa kuutumia huo msalaba aliotuamrisha kuubeba kama ishara yetu ya kuonesha kuwa ni wafuasi wake, itukumbushe kile ambacho yeye mwenyewe alipitia na angenda tukiishi.

Msalaba unatueleza uponyaji wetu, Yohan 3:14 inatueleza kwamba tutapona dhambi zetu pale ambapo mwana wa Adamu atainuliwa juu msalabani, kama ambavyo wana wa Israel walipona baada ya kumuangalia nyoka wa shaba alieinuliwa jangwana na Musa (Hesabu 21:4).
 
Kuhusu kutumika kwa alama ya samaki, kwa kifupi ni kutokana na mazingira aliyokulia, kuhubiri na kufundisha Kristo.

Anaanza kuwaita wafuasi wake kutoka kwenye uvuvi wa samaki, anahubiri habari njema pembezoni mwa bahari panapopatikana samaki, anawalisha maelfu kwa mkate na samaki.

Hivyo samaki inawakilisha wafuasi wa kristo, kama alivyowaeleza wavuvi wale (Simoni (Petro) na nduguye Andrea) katika Math: 3:19 kwamba hawatavua samaki tena, bali watawaleta wanadamu katika ufalme wa mbingu.

DUC IN ALTUM, msemo wa kilatini ambao msingi wake ni Luk 5:4, Yesu anamuamuru Simoni atweke zaidi mpaka kilimdini ili akavue samaki. Theolojia inasema mstari huu unatuasa kutokukata tamaa katika kuutafuta ufalme wa mbingu (hasa katika kuwaleta wengine katika imani ya Kristo).

Kwa misingi hiyo, alama ya samaki iliwakilisha kabisa wafuasi wa Kristo.
 
Hujui maana ya msalaba kaa kimwa uelimishwe
Mkuu sijui maana ya neno msalaba au ishara ya msalaba? Tulia usome nilio andika, naona Imani yako ulio aamini ina kutesa kukubaliana na ukweli.
 
Nitakuelezea kidogo kwa misingi ya Biblia, ambayo ninaamini unaiamini ndio maana umekiri kuja duniani na kusulubiwa kwa Kristo kwenye aya ya kwanza ya maelezo yako.

Tukianza na huo mstari uliourejelea, Gal 3:13 unaanza na maelezo mengine kabla ya kurejea (quote) maelezo ya Kumb: 21:23 yanayoelezea hiyo laana. Kwa lugha rahisi kama ulitaka kuelezea laana ya msalaba, basi ungefanya rejea ya Kumbukumbu la Torati, ambapo huo mstari ndio unaeleza kuwa Mtu akitenda dhambi akauawa na kutundikwa juu ya mti, basi mzoga wake usikae usiku kucha kwasababu anakua amelaaniwa kwa kutundikwa juu ya mti kama mdhambi.

Lakini mstari uliourejelea (Gal 3:13), unaeleza kinyume chake. Paulo anatuambia kuwa Kristo alitukomboa kutoka katika laana ya Torati (maana yake alilazimika kufanyiwa vile ambavyo mtu alieadhaniwa kuwa mwenye laana zaidi anatendewa, ikiwa yeye anaaminika ni Mtakatifu ili kuonesha kwamba hakuna kitu kinachoweza kuwakilisha hali ya laana kwa mtu).

Katika maisha yetu ya kila siku tuna watu ambao tunawachukulia kama mifano yetu ama miongozo yetu katika imani, siasa, elimu na teknolojia. Mara nyingi wanapofanya vitu ambavyo sisi tulihofia kuvifanya basi tunaondoa ile hofu na kupata imani na mtazamo mpya juu ya hivyo vitu. Mfano ni namna tunavyoiga mitindonya maisha, namna wanasiasa wanavyoshiriki katika matukio mbalimbali yenye muonekano wa hali ya chini ili kutuaminisha wapo sawa na sisi, namna ambavyo tunatarajia viongozi wetu wa dini waishi kama mifano yetu ya Utakatifu.

Kwa mtazamo huo huo, ndipo Paulo anatuambia kwamba, kile tulichoamini ni laana katika Torati, kimefutwa na alietoka juu kuja kukaa nasi. Maana isingewezekana Mungu neno aliekingiwa dhambi ya asili tangu kizazi chake cha nyuma, aje kunajisiwa na wanadamu.

Kuhusu kuutumia mslaba kama ishara ya Ukristo, haijalishi ilichelewa kiasi gani na haijalishi hapo mwanzo msalaba uliwakilisha nini, lakini ukweli unabaki kwamba, Kristo mwenyewe aliainisha ili uwe mfuasi wake (Mkristo) ni lazima ubebe msalaba na kumfuata. Math 16:24, Luk 9:23, Mark 15:30

Ukibahatika kwenda shule, ukimaliza ukataka kupatiwa ajira inayoendana na shule yako basi watataka uwaoneshe uthibitisho wa wewe kwenda shule, hapo hawatahitaji uwaletee mkanda wa video unaoonesha kuwa wewe umekua ukihudhuria vipindi, bali alama pekee unayopewa kuwakilisha shule yako. Vivyo hivyo kwenye harakati zetu zote za maisha, kila mahali utatakiwa kuonesha alama fulani inayoonesha kuwa unastahili kuwepo eneo hilo.

Kutokana na Kristo kutuamuru tubebe msalaba (ambao ki maantiki alimaanisha kukubali kuteseka) basi na sisi tunaona ni sawa kabisa kuutumia huo msalaba aliotuamrisha kuubeba kama ishara yetu ya kuonesha kuwa ni wafuasi wake, itukumbushe kile ambacho yeye mwenyewe alipitia na angenda tukiishi.

Msalaba unatueleza uponyaji wetu, Yohan 3:14 inatueleza kwamba tutapona dhambi zetu pale ambapo mwana wa Adamu atainuliwa juu msalabani, kama ambavyo wana wa Israel walipona baada ya kumuangalia nyoka wa shaba alieinuliwa jangwana na Musa (Hesabu 21:4).
Mkuu ahsante, kwa ufupi unacho pinga ni kipi? Na msimamo wako ni upi?
 
Mama wa mtoa mada angeolewa akiwa na umri sahihi tungeepushwa na mada kama hii, ila ndo hvy tena aliolewa akiwa mtoto wa miaka sita hvy hana ujuzi wa kulea mwana ipasavyo
 
Kuhusu kutumika kwa alama ya samaki, kwa kifupi ni kutokana na mazingira aliyokulia, kuhubiri na kufundisha Kristo.

Anaanza kuwaita wafuasi wake kutoka kwenye uvuvi wa samaki, anahubiri habari njema pembezoni mwa bahari panapopatikana samaki, anawalisha maelfu kwa mkate na samaki.

Hivyo samaki inawakilisha wafuasi wa kristo, kama alivyowaeleza wavuvi wale (Simoni (Petro) na nduguye Andrea) katika Math: 3:19 kwamba hawatavua samaki tena, bali watawaleta wanadamu katika ufalme wa mbingu.

DUC IN ALTUM, msemo wa kilatini ambao msingi wake ni Luk 5:4, Yesu anamuamuru Simoni atweke zaidi mpaka kilimdini ili akavue samaki. Theolojia inasema mstari huu unatuasa kutokukata tamaa katika kuutafuta ufalme wa mbingu (hasa katika kuwaleta wengine katika imani ya Kristo).

Kwa misingi hiyo, alama ya samaki iliwakilisha kabisa wafuasi wa Kristo.
Mkuu kwahilo la ishara ya samaki kuakilisha wafuasi wa ukristo tuko pamoja,
Sasa kwanini ilikuja kubadilishwa tena? Ikaletwa ishara ya msalaba ishara ilio kua inatumika na wa pegani?
 
Mkuu sijui maana ya neno msalaba au ishara ya msalaba? Tulia usome nilio andika, naona Imani yako ulio aamini ina kutesa kukubaliana na ukweli.
hiyo misalaba ipo ya aina nyingi kachunguze, kuna mpaka masonic crosses. We unazungumzia msalaba upi, ule mti aliyesulubiwa bwana wetu Yesu Kristo au misalaba yako unayoijua?
 
Back
Top Bottom