Je, wageni wanaohujumu uchumi wetu waadhabiweje?

Poise

JF-Expert Member
May 31, 2016
7,633
7,912
Habari wana JF,

Naamini wote mu wazima poleni kwa kusoma namba , muda siyo mrefu mambo yatakuwa poa.

Napenda kwenda kwenye mada!

Wana JF, ningependa kupata maoni yenu kuhusu wageni (wasio watanzania) wanaojihusisha na uhujumu uchumi wetu hasa katika kuua na kusafirisha nyara za serikali.

Kama vile, meno ya ndovu, ngozi za kakakuona, ngozi na kucha za chui na simba na nyara zingine zifananazo na hizo.

Naulizia hivi kwa sababu, sasa hivi watuhumiwa wengi wanaokamatwa kujihusisha na vitendo hivyo ni wa kutoka nchi za nje.

Hata leo tu , wamekamatwa wageni wawili wakiwa na meno 2 ya tembo yenye uzito wa 40+kg (chanzo, TBC FM)

Ahsanteni
 
Back
Top Bottom