MTZ 255Dar
JF-Expert Member
- Sep 25, 2018
- 1,152
- 3,967
LENGO LA PUTIN LIMEANGUKIA PUA?
Putin alijua akitishia kuivamia kijeshi Ukraine Basi NATO wataogopa na kukubali matakwa ya Urusi ili asiivamie Ukraine. Malengo ya Urusi yalikuwa Kama ifuatavyo;
1. Marekani na Washirika wake wa NATO wasaini mkataba na URUS ambao utaipiga Marufuku nchi ya Ukraine kujiunga na NATO mazima.
NATO wamekataa takwa Hilo la URUS wakisema Uanachama wa Ukraine kujiunga NATO ni jukumu la uamuzi wa Mataifa 30 wanachama wa NATO. NATO imeongeza kwa kusema,URUS Haina mamlaka ya kuzuia Sera ya NATO ya OPEN DOOR POLICY hata Kidogo. Ukraine ikikidhi vigezo itajiunga na NATO.
2. Marekani na Washirika wake wa NATO waondoe Siraha zao ambazo wameipa nchi ya Ukraine tangu mwaka 2014. URUS imedai kuwa Ukraine ametumia Siraha hizo kuwapiga Washirika wa Urusi kwenye majimbo ya CRIMEA, DONBASS, LUHANSK na DONETSK.
Marekani na Washirika wake wa NATO inaonekana kabisa wamepuuza matakwa hayo badala yake Marekani na Uingereza wameongeza msaada wa Siraha kwa Ukraine hivi Karibuni.
3. Marekani na Washirika wake wa NATO wasijitanue kwa kuweka Majeshi yake na Siraha kwenye nchi za Ulaya Mashariki ambazo zilijiunga na NATO Kabla ya mwaka 1997. Hapa Urusi ilimaanisha nchi za ROMANIA, HUNGARY, LITHUANIA na LATVIA.
Marekani na Washirika wake wa NATO wamepuuza matakwa hayo. Hivi Karibuni rais wa Marekani JOE BIDEN ameiamuru wizara ya Ulinzi ya Pentagon kuwaweka Wanajeshi 8,500 tayari kupelekwa Ulaya Mashariki mda wowote ule. Tunavyoongea hivi Sasa,Wizara ya Ulinzi PENTAGON imeanza kuwapelekwa Wanajeshi 2,000 nchini Poland kutoka Marekani na Wengine 1,000 walioko Ujeruman imeanza kuwapeleka nchini ROMANIA.
Nchi za POLAND na ROMANIA zote Zina mpaka wa moja kwa moja na nchi ya Ukraine. Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema wazi kwamba NATO haitapeleka Wanajeshi wake nchini Ukraine ambayo sio wanachama lakini itatoa usaidizi wa vifaa vya kijeshi vya kujilinda kwa Ukraine.
Putin alijua akitishia kuivamia kijeshi Ukraine Basi NATO wataogopa na kukubali matakwa ya Urusi ili asiivamie Ukraine. Malengo ya Urusi yalikuwa Kama ifuatavyo;
1. Marekani na Washirika wake wa NATO wasaini mkataba na URUS ambao utaipiga Marufuku nchi ya Ukraine kujiunga na NATO mazima.
NATO wamekataa takwa Hilo la URUS wakisema Uanachama wa Ukraine kujiunga NATO ni jukumu la uamuzi wa Mataifa 30 wanachama wa NATO. NATO imeongeza kwa kusema,URUS Haina mamlaka ya kuzuia Sera ya NATO ya OPEN DOOR POLICY hata Kidogo. Ukraine ikikidhi vigezo itajiunga na NATO.
2. Marekani na Washirika wake wa NATO waondoe Siraha zao ambazo wameipa nchi ya Ukraine tangu mwaka 2014. URUS imedai kuwa Ukraine ametumia Siraha hizo kuwapiga Washirika wa Urusi kwenye majimbo ya CRIMEA, DONBASS, LUHANSK na DONETSK.
Marekani na Washirika wake wa NATO inaonekana kabisa wamepuuza matakwa hayo badala yake Marekani na Uingereza wameongeza msaada wa Siraha kwa Ukraine hivi Karibuni.
3. Marekani na Washirika wake wa NATO wasijitanue kwa kuweka Majeshi yake na Siraha kwenye nchi za Ulaya Mashariki ambazo zilijiunga na NATO Kabla ya mwaka 1997. Hapa Urusi ilimaanisha nchi za ROMANIA, HUNGARY, LITHUANIA na LATVIA.
Marekani na Washirika wake wa NATO wamepuuza matakwa hayo. Hivi Karibuni rais wa Marekani JOE BIDEN ameiamuru wizara ya Ulinzi ya Pentagon kuwaweka Wanajeshi 8,500 tayari kupelekwa Ulaya Mashariki mda wowote ule. Tunavyoongea hivi Sasa,Wizara ya Ulinzi PENTAGON imeanza kuwapelekwa Wanajeshi 2,000 nchini Poland kutoka Marekani na Wengine 1,000 walioko Ujeruman imeanza kuwapeleka nchini ROMANIA.
Nchi za POLAND na ROMANIA zote Zina mpaka wa moja kwa moja na nchi ya Ukraine. Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema wazi kwamba NATO haitapeleka Wanajeshi wake nchini Ukraine ambayo sio wanachama lakini itatoa usaidizi wa vifaa vya kijeshi vya kujilinda kwa Ukraine.

