Je Unaridhika na Maazimio Ya kamati kuu Chadema?

Je Unaridhika na Maazimio Ya kamati kuu Chadema?

Alvin Slain

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
6,375
Reaction score
3,668
Hujambo na karibu.
""Katika hali ya kisiasa inayoendelea nchini Tanzania, Hususani katika chama cha Chadema, Chama kikuu cha Upinzani,
Maswali ni mengi kuliko majibu, Kamati kuu kama chombo cha juu kabisa ktk chama, Kiliazimia kuwavua vyeo makada maarufu wa chama hicho kikongwe, Katika siasa za Africa Mash. Tuhuma mbalimbali zuliorodheshwa ikiwa ni pamoja na kuunda, Kambi ndani ya chama wakati ambapo chama kikiwa na wakati mgumu,Ikizingatiwa chama kimekua kikizushiwa tuhuma mbalimbali.
Je kwa haya kamati imafanya vema??
 
Yah,maswali ninayojiuliza ni kuwa,hivi kama waliona viongozi wao wana mapungufu je wakikaa nao na kujaribu kuyatatua?au waliamua tu kuunda bila kujaribu kukaa pamoja?kama sivyo cdm wako sahihi kabisa kuwavua vyeo'maana wanaonekana walikuwa na mlengo tofauti.kwanini uendelee kupambana huku wasaliti wakiwa upande wako?
 
Waridhike wasiridhike cha msingi maamuzi ni muafaka..
 
Binafsi nimeridhika........japo hili suala ni gumu na pengine unaweza ukadhani ndio mwisho wa cdm ukiliangali juu juu lkn kiukweli hapo ndio uponyaji unapotokea.
 
Nianze kwa kuipa kamati BRAVO! Imeandika historia na ni somo kwa vyama vyote kuwa na maamuzi magumu. Hili la zito na wenzake ni kitu kidogo kwao na si sawa na wale madiwani wa Arusha waliopoteza ajira zao.
Kinachowashinda watu wengi ni kitu kidogo sana. Unapokuwa group member huwezi kuazisha group nyingine within na ukawa unataka kumeet objectives and goals za both group at the same time. Utachemsha lazima.
Zito and others of his kind kasome tena group formation uone kama mlichokuwa mnakifanya kinafanania.
Ushauri wangu kwa zito ni kuwa achana na vyombo vya habari kwani havina urafiki wala uadui wa kudumu na mtu yeyote. Vyaweza kukubomoa hadi ukasahaulika kabisa. Mifano unayo kama kina Walid Kabouru. Wapo wapi sasa? Najua waliokuponza ni wale wanaokutumia nawe ukakubali kutumika.
 
Wao na ukanda, ukabila, na udini wao. Sisi ni upendo, uzalendo na uzalendo wetu. Chadema imepata umaarufu kupitia zito na Dr. Silaha hawa kina lema na mnyika, mbowe na lisu wanasafiria nyota za kina zitto, kwa kuwa wamevunja daraja(zitto) kwa udini watarajie anguko kuu 2015,nina experience na hii kitu kwan tangu 1995 nimeshiriki kupiga kula, jiulize ipo wapi NCCR-MAGEUZI ya lyatonga mrema? Buriani chadema kwa kulewa sifa za kijinga
 
nimelidhika tena naona km uamzi ulichelewa sana, huu siyo muda wa siasa za majina ndani ya cdm, ikumbukwe watz wenzetu wamepoteza uhai kwaajili yakuitetea na kupigania cdm leo mtu aje ajifanye maarufu avuruge chama alafu achekewe? Hapana hongereni sana wajumbe wa kamati kuu
 
Wao na ukanda, ukabila, na udini wao. Sisi ni upendo, uzalendo na uzalendo wetu. Chadema imepata umaarufu kupitia zito na Dr. Silaha hawa kina lema na mnyika, mbowe na lisu wanasafiria nyota za kina zitto, kwa kuwa wamevunja daraja(zitto) kwa udini watarajie anguko kuu 2015,nina experience na hii kitu kwan tangu 1995 nimeshiriki kupiga kula, jiulize ipo wapi NCCR-MAGEUZI ya lyatonga mrema? Buriani chadema kwa kulewa sifa za kijinga
hahaha! Utoto huo ukabila, udini viliishashindwa we uko wapi? Ila ushaingiza buku 7 zako
 
Back
Top Bottom