Je, unamwelewaje mwanaume huyu?

Je, unamwelewaje mwanaume huyu?

Nyam

Senior Member
Joined
Jul 9, 2012
Posts
134
Reaction score
72
Habari wana JF..

Mimi ni mdada, nilianzisha mahusiano na kijana mmoja aliyenizidi zaidi ya miaka 10, wakati naanza nae mahusiano sikuwa serious ,nilitaka tu aniondolee stress nilizokuwa nazo kwa kipindi icho baada ya kuachana na mpenzi wangu zaidi ya mwaka mmoja, kipindi chote icho sijawahi kuwa na mahusiano.

Sasa baada ya kukutana na huyu kijana,nimeshangaa mwenzangu kaning'ang'ania na kila nikitaka kutoka mikononi mwake inashindikana.Kwa upande wake yeye ana mtoto mmoja mwenye miaka 8 anaishi na mama yake (mama mtoto) ambaye hawana mahusiano tena na kila mtu anaishi kivyake.

Baada ya kupita kama miezi 3 toka nimeanza kuwa nae kimahusiano ameanza kuniomba nimzalie mtoto ila mimi najiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu...Je ni kweli ananipenda au mtoto ndo msukumo wa kuwa na mimi ingawaje ananambia yupo tayari kwenda nyumbani kujitambulisha...Ila topic yake kubwa nimzalie mtoto.

Kitu kingine kinachoniogopesha alinambia kuwa miaka mi4 iliyopita aliwahi kupata ajali akaumia mguu, docta akamwambia uwezekana wa yeye kupata mtoto kwa kipindi icho ni mgumu sana labda mpakaumdae upite, eti ndo mana ananiomba ajaribu kama ataweza kuzaa tena ndo afanye process nyingine za kwenda nyumbani....

Nisaidieni kutafakari juu ya hili...
 
Last edited by a moderator:
@Nyam nikisema hujitambui nakosea?

Mbali nakuufata moyo wako, lazima uwe na msimamo wa mwanaume unayemtaka, sifa zake, na ujue nini unahitaji katika maisha yako. Je ukiwa na huyo jamaa mdoto zako zitatimia?

Acha ujinga, mtu anakudanganya kwenda kwenu unakubali kuzaa nae.

Kama anataka umzalie mwambie afate process zote za ndoa iliuishi pamoja.

Ukipuuza utanikumbuka..
 
Funga ndoa kwanza. .
. ujinga mwingine sahau..
 
@Nyam nikisema hujitambui nakosea?

Mbali nakuufata moyo wako, lazima uwe na msimamo wa mwanaume unayemtaka, sifa zake, na ujue nini unahitaji katika maisha yako. Je ukiwa na huyo jamaa mdoto zako zitatimia?

Acha ujinga, mtu anakudanganya kwenda kwenu unakubali kuzaa nae.

Kama anataka umzalie mwambie afate process zote za ndoa iliuishi pamoja.

Ukipuuza utanikumbuka..
Mkuu umemaliza kila kitu
 
yaani kidogo tu ndoa, yaani miezi mi3 unataka ndoa afu unakuja huku na gia "eti unang'ang'aniwa" kama mtoto si tayari anae, sema wewe na kiherehere chako, ndio unataka ndoa!
 
Mwambie ukweli kuwa hukuwa na malengo nae it was just for pleasure
 
Kama anakupenda si mfunge ndoa. Kama haumpend sidhan kama kuna haja ya kuendelea na hayo mahusiano maana mnapoyezeana muda.
Hiv inakuaje mtu unashindwa kuachana na mtu if u real mean it? Nina waswas bado uko mguu nje mguu ndani
 
Kweli mahusiano ya siku hizi ni shida sana. Yani kila kitu ni kuombana hadi kuzaa.Mimi najua mkisha anza kugegedana mtoto huwa ni matokeo siyo kuanza oooh tuzae mara oooh tusubiri kwanza. Kwanini mgegedane halafu muogope kuzaa? Yani mtu ule muwa halafu uogope kukutana na fundo!
 
Sasa kama humpendi si umwambie tu ukweli na uondoke bila kelele
 
Habari wana JF..

Mimi ni mdada, nilianzisha mahusiano na kijana mmoja aliyenizidi zaidi ya miaka 10, wakati naanza nae mahusiano sikuwa serious ,nilitaka tu aniondolee stress nilizokuwa nazo kwa kipindi icho baada ya kuachana na mpenzi wangu zaidi ya mwaka mmoja, kipindi chote icho sijawahi kuwa na mahusiano.

Sasa baada ya kukutana na huyu kijana,nimeshangaa mwenzangu kaning'ang'ania na kila nikitaka kutoka mikononi mwake inashindikana.Kwa upande wake yeye ana mtoto mmoja mwenye miaka 8 anaishi na mama yake (mama mtoto) ambaye hawana mahusiano tena na kila mtu anaishi kivyake.

Baada ya kupita kama miezi 3 toka nimeanza kuwa nae kimahusiano ameanza kuniomba nimzalie mtoto ila mimi najiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu...Je ni kweli ananipenda au mtoto ndo msukumo wa kuwa na mimi ingawaje ananambia yupo tayari kwenda nyumbani kujitambulisha...Ila topic yake kubwa nimzalie mtoto.

Kitu kingine kinachoniogopesha alinambia kuwa miaka mi4 iliyopita aliwahi kupata ajali akaumia mguu, docta akamwambia uwezekana wa yeye kupata mtoto kwa kipindi icho ni mgumu sana labda mpakaumdae upite, eti ndo mana ananiomba ajaribu kama ataweza kuzaa tena ndo afanye process nyingine za kwenda nyumbani....

Nisaidieni kutafakari juu ya hili...
Nyam,
Unapojenga hoja jaribu kujihadhari na ulimi ambao unaponza.
Statement yako ya awali ni kwamba ulimkubali kukuondolea stress, sasa hii habari unaleta mbele ya jukwaa ni nini kama sio ushambenga? Sikiliza mwenyewe unavyonogewa na uamue. Usitafute ushauri wa watu kwa hoja ya unafki.
 
Uzi huu unamkanganyiko na watoa majibu wengine wanajikanganya.
Mtoa mada umesema hapo mwanzo wala humpendi bwana huyu sasa huko kwingine kwa nini?
Yaani humpendi mtu na wataka kumzalia ili iweje? Eti anataka kujaribu na wewe unakuja kuuliza kama unataka kuwa mwili wa majaribio? Yaani kabisa mwili wa majaribio kama anaweza kuzaa ama laa khaaa...watu bwana.
Haya huyu atakikuoa utaishia kugongwa nje mpk maana huna mapenzi nae hiyo ndo itadumu vipi? Eti kang'ang'ania mtu anawezaje kufanya hivyo hili hali nawe hutaki?
Acha longo longo ninachokiona hapa wewe ndio umeng'ang'ania sijui kwa nini lakini ndo ilivyo na lambda yeye ndio hakupendi na pengine wewe ndio wamwomba mtoto.
 
Habari wana JF..

Mimi ni mdada, nilianzisha mahusiano na kijana mmoja aliyenizidi zaidi ya miaka 10, wakati naanza nae mahusiano sikuwa serious ,nilitaka tu aniondolee stress nilizokuwa nazo kwa kipindi icho baada ya kuachana na mpenzi wangu zaidi ya mwaka mmoja, kipindi chote icho sijawahi kuwa na mahusiano.

Sasa baada ya kukutana na huyu kijana,nimeshangaa mwenzangu kaning'ang'ania na kila nikitaka kutoka mikononi mwake inashindikana.Kwa upande wake yeye ana mtoto mmoja mwenye miaka 8 anaishi na mama yake (mama mtoto) ambaye hawana mahusiano tena na kila mtu anaishi kivyake.

Baada ya kupita kama miezi 3 toka nimeanza kuwa nae kimahusiano ameanza kuniomba nimzalie mtoto ila mimi najiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu...Je ni kweli ananipenda au mtoto ndo msukumo wa kuwa na mimi ingawaje ananambia yupo tayari kwenda nyumbani kujitambulisha...Ila topic yake kubwa nimzalie mtoto.

Kitu kingine kinachoniogopesha alinambia kuwa miaka mi4 iliyopita aliwahi kupata ajali akaumia mguu, docta akamwambia uwezekana wa yeye kupata mtoto kwa kipindi icho ni mgumu sana labda mpakaumdae upite, eti ndo mana ananiomba ajaribu kama ataweza kuzaa tena ndo afanye process nyingine za kwenda nyumbani....

Nisaidieni kutafakari juu ya hili...
Kimbia kwa usalama wako
 
Ulitaka kupunguza stress, sasa stress zimeongezeka. Kulikuwa na haja gani kuanzisha mahusiano wakati hukujiandaa

Tafakari chukua hatua
 
Moja ya changamoto kubwa sana kwa vijana ni kutokujitambua, hujui hama yako hadi ufikie umri ambao kimsingi utaona kabisa zile ndoto zako zooote zinabakia kuwa ndoto tuuuu, then unaamliwa na force imprecion sasa ndo shida inapoanzia hapo
 
Back
Top Bottom