Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,707
- 7,436
Kuna watu wanakiri kwamba wamepata utajiri baada ya kupewa "dawa" na waganga wa kienyeji au wachawi. Kulingana na Maandiko, inawezekana shetani akakupa mali lakini lazima ukubali kumsujudia. Katika Luka 4:5–7 imeandikwa:
"Akampandisha juu, akamwonesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja. Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa yeyote kama nipendavyo. Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake."
Hii inaonyesha kuwa Shetani ana uwezo fulani wa kutoa "fahari" na "enzi" ya kidunia — mali, mapesa, heshima — lakini kwa masharti kwamba lazima umsujudie na kumwabudu — kwa kushiriki mambo ya uchawi/ushirikina.
Shetani anajulikana kama baba wa uongo na muuaji.(Yohana 8:44). Akikupa mapesa au fahari ya dunia hii, ujue amekutega. Amekutega umwabudu mungu mwingine kinyume na agizo la Mungu. Mungu alisema: “Usiwe na miungu mingine ila mimi.” (Kutoka 20:3)
Ukiabudu miungu mingine maana yake unajitakia laana(Kum 28:15). Hivyo mali yoyote itakayokupeleka kwenye ibada nyingine ni laana hata kama inaonekana kama "baraka."
Hivyo ndugu yangu, kama unawaza kwenda kwa waganga ili upate utajiri, futilia mbali mawazo hayo. Shetani anakutega umsujudie halafu siku ya mwisho uangamie pamoja na yeye motoni.
cc: Nomadix
"Akampandisha juu, akamwonesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja. Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa yeyote kama nipendavyo. Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake."
Hii inaonyesha kuwa Shetani ana uwezo fulani wa kutoa "fahari" na "enzi" ya kidunia — mali, mapesa, heshima — lakini kwa masharti kwamba lazima umsujudie na kumwabudu — kwa kushiriki mambo ya uchawi/ushirikina.
Shetani anajulikana kama baba wa uongo na muuaji.(Yohana 8:44). Akikupa mapesa au fahari ya dunia hii, ujue amekutega. Amekutega umwabudu mungu mwingine kinyume na agizo la Mungu. Mungu alisema: “Usiwe na miungu mingine ila mimi.” (Kutoka 20:3)
Ukiabudu miungu mingine maana yake unajitakia laana(Kum 28:15). Hivyo mali yoyote itakayokupeleka kwenye ibada nyingine ni laana hata kama inaonekana kama "baraka."
Hivyo ndugu yangu, kama unawaza kwenda kwa waganga ili upate utajiri, futilia mbali mawazo hayo. Shetani anakutega umsujudie halafu siku ya mwisho uangamie pamoja na yeye motoni.
cc: Nomadix