Je, unaamini kuwa uchawi upo?

sawabho

JF-Expert Member
Feb 25, 2011
5,286
3,107
Siku nyingi nimekuwa siamini kama kweli kuna uchawi katika Tanzania hii, achilia mbali huko kwa wengine. Nimekuwa siamini kwa sababu makosa yote hapa nchini yana adhabu zake isipokuwa la uchawi hii ikimaanisha kuwa Serikali inaamini kuwa hakuna uchawi.

Hatahivyo, siku za hivi karibuni imani yangu imeanza kupungua baada ya Kiongozi mmoja katika Serikali hiyo hiyo inayoamini kuwa hakuna uchawi kudai kuwa amegundaua mbinu kuwa anarogwa ili awe zoba auwawe kirahisi.

Sasa nikajiuliza, huyu mtu yumo ndani ya Serikalini inayoamini kuwa hakuna uchawi, akiwa pekee yake kuna uchawi, inakuwaje hapa?

Aidha, jana tarehe 28/03/2011 nilikuwa nasikiliza Redio Wapo FM kuanzia saa 1.30 jioni kipindi cha "yaliyotufikia" nikasika kuwa kuna fisi ameshambulia watu huko Mto wa Mbu, akauawa na askari wa wanyama pori, baada ya kuuawa, wakakuta ametobolewa masikio kama alikuwa anawekewa hereni.

Je, huyu fisi alikuwa anashiriki mashindano ya "Miss Mto wa Mbu" au ni fisi wa wachawi?

Sasa wana JF wenzangu ni kweli kuna uchawi? Au ni njama za wajanja kutishia wenzao.
 
uchawi upo ila inategemea wewe imani yako imeegemea upande gani,hata maandiko matakatifu yamezungumzia uchawi kwamba upo,serikali kwa ujumla wake haiamini uchawi ila viongozi ndani ya serikali wanaweza kuamini uchawi kwani wao pia ni wanajamii
 
Siku nyingi nimekuwa siamini kama kweli kuna uchawi katika Tanzania hii, achilia mbali huko kwa wengine. Nimekuwa siamini makosa yote hapa nchini yana adhabu zake ispokuwa la uchawi hii ikimaanisha kuwa Serikali inaamini kuwa hakuna uchawi. Hatahivyo, siku za hivi karibuni imani yangu imeanza kupungua baada ya Kingozi mmoja katika Serikali hiyo hiyo inayoamini kuwa hakuna uchawi kudai kuwa amegundaua mbinu kuwa anarogwa ili awe zoba auwawe kirahisi. Sasa nikajiuliza, huyu mtu yumo ndani ya Serikalini inayoamini kuwa hakuna uchawi, akiwa pekee yake kuna uchawi, inakuwaje hapa?

Aidha, jana tarehe 28/03/2011 nilikuwa nasikiliza Redio Wapo FM kuanzia saa 1.30 jioni kipindi cha "yaliyotufikia" nikasika kuwa kuna fisi ameshambulia watu huko Mto wa Mbu, akawauwa na askari wa wanyama pori, baada ya kuauwa, wakakuta ametobolewa masikio kama alikuwa anawekewa hereini.

Je, huyu fisi alikuwa anashiriki mashindano ya "Miss Mto wa Mbu" au ni fisi wa wachawi?

Sasa wana JF wenzangu ni kweli kuna uchawi? Au ni njama za wajanja kutishia wenzao.




Waswahili wanasema kuwa lisemwalo lipo,sasa kama uchawi unaongelewa basi maana yake ni kuwa upo.
 
Uchawi upo mkuu,ila fisi kutobolewa masikio kama vile alikuwa aikivaa hereni inawezakana sio uchawi,kwa sababu watafiti na wanasayansi mbalimbali wa viumbe huwa wanawawekea viumbe monitors au kamera klingana na utafiti wanaotaka kufanya.Inawezekana fisi huyo alishawahi kufanyiwa utafiti huo,ndo maana alikuwa ametobolewa masikio,sio masikio tu wanaweza kuweka vifaa hivyo maalum sehemu yoyote kulingana na aina ya kiumbe
 
serikali lazima iseme haitambui uchawi kwani kesi ya uchawi ushaidi wake hauwezi kuwa rahisi kutolewa waziwazi lazima matendo ya kichawi yatumike sasa unafikiri hakimu atkubali kushuhudia vimbwanga mahakamani?
 
Uchawi ni imani muflis kuwa watu fulani wana nguvu fulani yenye uwezo wa kudhuru wengine. Hili jambo ni imani tu na imani hizo zimejikita katika jamii kweli kweli. Hao waliokuwa wakiitwa au wanaoitwa wachawi katika jamii huwa ni watu dhaifu sana, maskini na waoga wanaodharauliwa sana na jamii. Mara nyingi watu hao wakiitwa wachawi, hawakatai wala kukubali, kwani wengine hufikiria kuwa watu wakimuona ana nguvu hiyo ya ajabu (yaani uchawi) itakuwa ni sababu ya kuheshimiwa na kuogopwa.

Wengi wao hujiingiza katika matendo ya kufanya viinimacho au mazingaombwe ya kuwasadikisha watu kuwa wao kweli wanazo hizo nguvu na wana uwezo wa kudhuru. Kutokana na hilo, wakazaliwa watu wanaoitwa wachawi au walozi. Hawa watu wameanzisha utamaduni wao, kama zilivyo dini. Tofauti yao ni kuwa wao mambo yao hufanyika kwa siri, kwani lengo ni kuwadanganya watu waamini kuwa kweli wanazo nguvu za ajabu.

Hizi jamii za kichawi, kama secrete societies zingine hutoa sadaka na kufanya vitimbi vya hapa na pale vyenye lengo la kuwaaminisha watu kuwa wao wana nguvu zisizoonekana.

Lakini ukweli ni kuwa kama zilivyo jamii zote za siri, mambo haya yanagundulika na walio wengi kuwa si kweli. Wale wanaodanganyika wanabaki kuishi kwa hofu na wakati mwingine enzi hizo watu walilazimika kutoa kitu kidogo kwa wachawi ili wasirogwe. Huo ndo uchawi.

Ukiogopa vitimbi vyao, utajisalimisha kwao na kuwapa kitu kidogo ili wakulinde na uchawi.

Jamii ya wachawi ina umri mrefu kuliko hata dini zetu nyingi, ambazo nazo zimetumia mbinu kama zile zile wanazotumia wachawi kupambana nao. Mbinu wanayotumia wachawi ni kutangaza uwezo wa kudhuru watu kwa kutumia "magic". Dini zinatumia "nguvu za kimungu" kupambana na wachawi. Nguvu zote hizo ni 'supernatural'.

Kwa mtu mwenye scientific knowledge ya mwili wa binadamu na mazingira yake, uchawi ni kama hadithi za riwaya kwake na hauna madhara yoyote!

Huo ndo uchawi!
 
Amini usiamini uchawi upo ila imani yako ndiyo itakuongoza katika hilo unaweza ukauamini au usiuamini, uchawi ni nguvu za ngiza
 
Uchawi upo mkuu,ila fisi kutobolewa masikio kama vile alikuwa aikivaa hereni inawezakana sio uchawi,kwa sababu watafiti na wanasayansi mbalimbali wa viumbe huwa wanawawekea viumbe monitors au kamera klingana na utafiti wanaotaka kufanya.Inawezekana fisi huyo alishawahi kufanyiwa utafiti huo,ndo maana alikuwa ametobolewa masikio,sio masikio tu wanaweza kuweka vifaa hivyo maalum sehemu yoyote kulingana na aina ya kiumbe

Mkuu hiyo naifahamu niliisoma kwenye "Wildlife Management" lakini sio kwa fisi bali kwa wanyama wawindwao.
 
kwani serikali ni nini? Inakuwaje serikali haiamini katika dini lakini viongozi wana dini? Haya yakipata majibu, hata la uchawi majibu yatapatikana

Lakini dini inafahamika na ndio maana nikikashfu dini ya mwenzangu nitachukiliwa hatua za kisheria, lakini kama nikutishia kukuroga sichukuliwi hatua yoyete.
 
serikali lazima iseme haitambui uchawi kwani kesi ya uchawi ushaidi wake hauwezi kuwa rahisi kutolewa waziwazi lazima matendo ya kichawi yatumike sasa unafikiri hakimu atkubali kushuhudia vimbwanga mahakamani?

Hapo Nakupata, Mkuu.
 
Uchawi upo, kuna simba alivamia mbagala akajeruhi mtu mmoja alivyouawa tu ndani ya sekunde chahce walikuta kanyofolewa zehemu zake za siri jamani zilipelekwa wapi? nilishangaa sana. You never know huyo fisi walimvisha hiyo hereni ili fsi wengine wasijitokeze mitaa hiyo kila watu wana imani yao.

Uchawi upo.
 
Amini usiamini uchawi upo ila imani yako ndiyo itakuongoza katika hilo unaweza ukauamini au usiuamini, uchawi ni nguvu za ngiza

Unadhani kwa nini zikaitwa nguvu za giza? na si nguvu ya mwangaza? Kuna vitu vingi vya uongo ndani yake. Mungu wa kweli hafanyi vitu vyake gizani,hufanya mchana na hata usiku. Hafichi kitu.Chunguza vizuri.
 
... Nimekuwa siamini kwa sababu makosa yote hapa nchini yana adhabu zake ispokuwa la uchawi hii ikimaanisha kuwa Serikali inaamini kuwa hakuna uchawi....

Sheria ipo tena nadhani it is one of the oldest legislations in Tz that has yet to be repealed:

CHAPTER 18
_______
THE WITCHCRAFT ACT


An Act to provide for the punishment of witchcraft and of certain acts connected
therewith.

[28th December, 1928]



1. This Act may be cited as the Witchcraft Act.

2. In this Act unless the context otherwise requires–


"court" includes a local court as defined in the Magistrates Courts Act;





"instrument of witchcraft" means anything which is used or intended to be used or is commonly used, or which is represented or generally believed to possess the power, to prevent or delay any person from doing any act which he may lawfully do, or to compel any person to do any act which he may lawfully refrain from doing, or to discover the person guilty of any alleged crime or other act of which complaint is made, or to cause death, injury or disease to any person or damage to any property, or to put any person in fear, or by supernatural means to produce any natural phenomena, and includes charms and medicines commonly used for any of the purposes aforesaid;
"police force" means the Tanzania Police Force;


"public officer" means any employee of Government or of a local government authority;
"witchcraft" includes sorcery, enchantment, bewitching, the use of instrument of witchcraft, the purported exercise of any occult power and the purported possession of any occult knowledge.




 
Agalia wakati mwingine spelling zaweza kuaribu maana ya kile ulichokusudia. Hebu hii " akawauwa na askari wa wanyama pori, baada ya kuauwa, wakakuta ametobolewa masikio kama alikuwa anawekewa hereini" Hii haijatulia.
 
Agalia wakati mwingine spelling zaweza kuaribu maana ya kile ulichokusudia. Hebu hii " akawauwa na askari wa wanyama pori, baada ya kuauwa, wakakuta ametobolewa masikio kama alikuwa anawekewa hereini" Hii haijatulia.

Asante Mkuu, maoni yamepokelewa na kufanyiwa kazi. Nilifundishwa kusikiliza ushauri na kuufanyia kazia.
 
Uchawi upo, kuna simba alivamia mbagala akajeruhi mtu mmoja alivyouawa tu ndani ya sekunde chahce walikuta kanyofolewa zehemu zake za siri jamani zilipelekwa wapi? nilishangaa sana. You never know huyo fisi walimvisha hiyo hereni ili fsi wengine wasijitokeze mitaa hiyo kila watu wana imani yao.

Uchawi upo.

Hiyo ni sehemu ya mazingaombwe na mauza uza ya kukufanya uamini kuwa kweli uchawi upo. Lakini mwenye akili ya ukweli ulivyo hawezi kutishika eti kwa sababu mtu kachukua viungo vya uzazi vya mnyama. Unaweza kweli kulitumia hili kama kithibitisho cha kuwepo kwa uchawi? Samahani, naona tuko kwenye viwango tofauti mno vya uelewa wa mambo na itakuwa vigumu kueleweshana ikiwa haya ndo madai ya kuthibitisha kuwepo kwa uchawi.

Uchawi ni dhana. Ni dhana inayoishi na watu. Ziko dhana nyingi sana zinazoishi na watu hadi leo. Hata mira nyingi na desturi ni dhana tu ambazo zimejijenga kwa muda mrefu. Nyingine zina sababu za msingi, nyingine hazina sababu yoyote.

Dhana ya uchawi ipo na itaendelea kuwepo kwa sababu mazingira yanayochochea kuwepo kwa dhana hiyo bado yapo. Si ajabu watu wakafanya mauaji, wakasingizia aliyeuawa karogwa! Ila kadri siku zinavyoenda ndivyo watu wanavyozidi kuacha kimoja, kimoja kati ya yale waliyokuwa wakifikiria uchawi unaweza kuyafanya. Mfano imani hizo katika miaka ya 1970 na kurudi nyuma zilikuwa nyingi na nguvu zaidi. Ila leo tunaona maeneo hasa ya mijini hayo mambo yakizidi kukosa mshiko kwani wengi wanaona kuwa ni uongo.

Kusema kuwa uchawi ni uongo, haina maana kuwa hauna madhara. Uongo una madhara mengi mno! Ila silaha ya kupambana na uongo ni kuujua ukweli. Kwenye uchawi, ukweli ni maalifa ya kupambana na matatizo ya kila siku ya binadamu na mazingira yanayomzunguka. Ukishajua mengi kwenye hii, hofu ya uchawi inapungua, ......, hatimaye inaisha. Ikiisha hofu ya uchawi, uchawi umeisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom