Je, U.S.A inapanga kuizingira Iran?

Je, U.S.A inapanga kuizingira Iran?

“Kuanzia sasa hivi mara moja, Jeshi la Wanamaji la Marekani — lililo bora zaidi duniani — litaanza mchakato wa kuzuia (blockade) meli zote zinazojaribu kuingia au kutoka katika Mlango wa Bahari wa Hormuz,” aliandika Rais wa Marekani Donald Trump kwenye Truth Social.

Nikimnukuu:

“Kwa hiyo, kama mnavyoona, mkutano ulienda vizuri, mambo mengi yalikubaliwa, lakini jambo muhimu zaidi — suala la nyuklia — halikukubaliwa.

Kuanzia sasa mara moja, Jeshi la Wanamaji la Marekani, lililo bora zaidi duniani, litaanza mchakato wa kuzuia (blockade) meli zote zinazojaribu kuingia au kutoka katika Mlango wa Bahari wa Hormuz.

Wakati fulani, tutafikia hali ya ‘kila mtu anaweza kuingia, kila mtu anaweza kutoka,’ lakini Iran haijaruhusu hilo kwa kudai tu kwamba ‘huenda kuna bomu la baharini mahali fulani,’ jambo ambalo hakuna anayelijua isipokuwa wao.
Hii ni unyang’anyi wa kimataifa, na viongozi wa nchi, hasa wa Marekani, hawatakubali kunyanyaswa.

Nimeagiza pia jeshi letu la wanamaji kufuatilia na kuzuia kila meli katika maji ya kimataifa ambayo imelipa tozo kwa Iran. Hakuna atakayelipa tozo haramu atakayekuwa salama baharini.

Pia tutaanza kuharibu mabomu ya baharini ambayo Iran imeweka katika njia hiyo.

Muirani yeyote atakayefyatua risasi dhidi yetu au dhidi ya meli za kiraia atakabiliwa na nguvu kali sana.

Iran inajua, kuliko mtu yeyote, namna ya kumaliza hali hii ambayo tayari imeiharibu nchi yao. Jeshi lao la majini halipo, jeshi la anga halipo, ulinzi wa anga na rada zao hazina maana, na viongozi wao wengi wamekufa kutokana na azma yao ya nyuklia.

Zuio hili (blockade) litaanza muda si mrefu. Nchi nyingine pia zitahusika.

Iran haitaruhusiwa kufaidika na kitendo hiki kisicho halali cha unyang’anyi. Wanataka pesa, na zaidi wanataka nyuklia.

Zaidi ya hayo, wakati ufaao utakapofika, sisi tuko tayari kabisa kijeshi, na jeshi letu litakamilisha kilichobaki dhidi ya Iran.”
 
Vitisho tuu.. Keshachemsha hamuwezi muajemi tena
Rais Donald Trump ameshiriki makala kwenye Truth Social inayoelezea mkakati unaowezekana wa Marekani wa kuizingira Iran kwa jeshi la majini (naval blockade), baada ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran mjini Islamabad kumalizika bila kufikiwa makubaliano.

Blockade ni Nini Kijeshi?

Tofauti na vikwazo vya kawaida vya kiuchumi, Naval Blockade ni kitendo cha kivita ambapo Marekani itatumia meli zake za kivita kuzuia kitu chochote kuingia au kutoka nchini Iran kupitia baharini. Vitu vinavyozuiliwa:

1. Hakuna Mafuta

Iran haitaweza kuuza hata pipa moja la mafuta nje.

2. Hakuna Chakula wala Dawa

Kila meli inayoelekea bandari za Iran (kama Bandar Abbas) itasimamishwa, kukaguliwa, au kugeuzwa na jeshi la Marekani.

3. Kukata Mapato

Hii itaiyeyusha ile akiba ndogo ya fedha ambayo Iran imebaki nayo ndani ya wiki chache.

Mkakati wa "Mtego wa Chuma"

Makala aliyoishiriki Trump inadokeza kuwa Marekani inaweza kutumia:

Meli za Kubeba Ndege (Aircraft Carriers): Zitalinda Mlango-bahari wa Hormuz na Bahari ya Oman.
Nyambizi (Submarines): Zitafuatilia meli yoyote ya siri inayojaribu kupita chini ya rada.

Droni za Majini: Zitafanya doria saa 24 kuhakikisha hakuna mashua ya Iran inayothubutu kutega mabomu mapya baada ya zile 28 za mwanzo kuzamishwa.

Kwanini Sasa?

Trump anatumia mbinu yake ya zamani ya "Maximum Pressure": Baada ya Iran kukataa masharti ya Marekani usiku kucha, Trump anataka kuwaonyesha kuwa "Gharama ya kusema HAPANA ni kubwa."

Ujumbe kwa China

Blockade hii pia ni onyo kwa China, ambayo ndiyo mnunuzi mkuu wa mafuta ya Iran. Marekani inasema, "Kama mnataka mafuta ya Iran, itabidi mpambane na jeshi letu la majini."
Makafir wanasubiriwa ardhin ile waonje nguvu halisi ya mujahdeen
 
Makafir wanasubiriwa ardhin ile waonje nguvu halisi ya mujahdeen
Unaongea hayo ukiwa masjid kubra ukihudimia masheikh ubwabwa alkasusu
FB_IMG_1775667776328.jpg
 
Jamaa hawafikirii hilo ,

Anachofanya USA ni kutumia busara tu
Achaa uhuni! Marekani hàjawahi kuwa na busarà Wala hurumà mbéle ya maslahi yake. Na huwa haogopi kusemwa au kujadiliwa vibaya pale anapotimiza matakwa yake. Hàna busarà Wala hurumà dhidi ya watu wa Iran.
Anatumiaje busarà mtu ambaye ameshindwa kutimiza matarajio yake?
 
Back
Top Bottom