Ndugu yangu Omary kutangaza urais sio dhambi. Ni vema na haki. Lakini ukumbuke kama una peculiarities na some doubts surrounding you, usitegemee watu wakae kimya na wakupokee kwa mikono miwili na kukupigia vigelegele eti kwa kuwa wewe ni shujaa kwani umewahi miaka mitano kabla kutangaza nia. Ni vizuri sana mh. Zitto alivyotangaza nia ya urais mapema kwani anatimiza demokrsia na haki yake ya msingi ya kugombea urais kama ametimiza vigezo vyote.
Lakini ndugu yangu Omary nini lengo la kutangaza nia mapema?
Simply, ni kukuwezesha watu wakufahamu vizuri, mazuri yako (na mabaya yako) ili watu wapime na wenyewe waweze kuchuja na pumba na mchele then wa decide kukupa dhamana kubwa ya kuwalinda, kutetea, kuwatumikia na mwisho kuwaletea maisha bora zaidi ya yale uliyowakuta nayo!
Ndugu yangu unapochambuliwa ukae ukijua unapitishwa kwenye microscope kali kabisa na watu wanaku screen na kuku probe mpaka wajiridhishe kuwa unafaa. Hapo ndipo mtu unapochambuliwa na kuwa exposed kwa mazuri na mabaya yako! Yaani hapo ndipo unapovuliwa nguo kisiasa ili kuonekana usafi au uchafu wako.
Kama una mabaya ni lazima yasemwe, na kama kuna doubts ni lazima ziwe cleared. Na kama unasifa pia usifiwe. Ndugu yangu hiyo ni very painful process, kwani utapata kila aina ya dhoruba na hata kusingiziwa kunakuwepo. Lakini kama uko clean, then atleast unaweza ukatembea kifua mbele kama Dr Slaa bila wasiwasi, ingawa pia unaweza ukazushiwa mambo mabaya! Lakini mwisho wa siku wananchi ndio wanaamua uwepo au usiwepo. Lakini pia kura zako zinawezaibiwa au ukachezewa kila aina ya rafu za kisiasa.
Ndugu yangu hiyo ndiyo hali halisi, na ndio mchezo unaoitwa siasa! Cha maana kuwa strong, vumilia na pambana! TURIDHISHE, tu CONVINCE.
Sisi wananchi ni tunayo haki ya kujiridhisha na kutoa maoni na madukuduku yetu, lengo likiwa ni kuboresha na ni demokrasia.
Hivyo ndugu yangu naomba utofautishe kutangaza nia mapema na kuwa screened. Ni kweli kabisa hiyo process ya kuwa screened ni ngumu na ni kazi kwelikweli kama ulivyosema! Cheche lazima ziwepo!! kUONGEA NA KUTOA MAONI NA MADUKUDUKU NITAFANYA BILA KUSITA ILI NISIJEJILAUMU BADAE BALI NIPATE MTU ATAKEYENIONGOZA KATIKA MAISHA BORA!