Je, tumeamua kuifanya Tanzania kuwa ‘a pariah state’?

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Katika miaka ya hivi karibuni, kuna mambo mengi sana yamefanyika nchini Tanzania ambayo yamerudisha nyuma sana juhudi za kujenga jamii iliyostaarabika, inayojiheshimu na inayoheshimika.

Leo sitamnyooshea kidole yoyote kwa lawama hizi ila naomba nigusie tu madhara ya kuwa ‘a pariah state’.

Kwa mujibu wa mtandao wa Wikipedia:

“A pariah state (also called an international pariah or a global pariah) is a nation considered to be an outcast in the international community. A pariah state may face international isolation, sanctions or even an invasion by nations who find its policies, actions, or its very existence unacceptable.”

Kwa tafsiri isiyo rasmi ni kuwa “a pariah state ni taifa ambalo Jumuia ya Kimataifa imeliona kuwa halina hadhi au sifa za kuwa katika Jumuia hiyo. Na taifa hilo kama lisipojirekebisha huwa linaenda kutengwa, kuwekewa vikwazo, na hata kuvamiwa. Katika macho ya dunia, sera, matendo na hata uwepo wa taifa la namna hiyo ni vitu ambavyo havikubaliki”.

Kiufupi kuwa a pariah state, au an outcast siyo jambo zuri. Linakunyima vingi. Ndiyo, utabaki na uhuru wako wa kujifungia ndani na kujiamulia mambo yako wakati wenzako wanajumuika na kufurahi pamoja. Kuwa an outcast siyo jambo zuri kwa mtu mmoja mmoja na hata kwa taifa.

Kwenye issue ya corona, Tanzania tuliona tuangalie kwanza maslahi ya taifa na tukaweka pembeni jukumu letu kama sehemu ya Jumuia ya Kimataifa.

Kutoa takwimu na taarifa rasmi na za uhakika za mambo kama maambukizi ya milipuko, ni moja ya majukumu yetu. Taarifa hizi zinasaidia dunia na wataalamu kujua mwenendo wa maambukizi na ndiyo msingi wa jinsi Jumuiya ya Kimataifa inatumia kujua wapi pa kusaidia. Fikiria kila taifa lingesema, sisi hatupimi na hatutoi taarifa zozote, leo dunia ingekuwa kwenye hali gani?

Tunatumia takwimu za wengine kuwazodoa kuwa wao corona imewapiga kweli kweli ila sisi takwimu zetu hatutaki kuzitoa.

Tunapowaza kuwa a pariah state, embu tuangalie taifa kama Eritrea limefaidika vipi kwa hali hiyo na ni hasara gani wamepata. Na hapo hata sijazungumzia mambo ya haki za binadamu na utawala wa sheria.

Naomba tujitafakari, nadhani kuna njia bora zaidi kuliko hizi tunazochukua.

NYONGEZA:

Sijui tafsiri rasmi ya kiswahili ya ‘a pariah state’ ila ukiniuliza mimi nitasema ni ‘taifa la kihuni’.
 
Unfortunately this is where our nation is headed. Too bad!

We have a chance to redeem ourselves in October, but should we miss it, another five years of the same shit will for sure send us into a Banana Republic.
 
Unfortunately this is where our nation is headed. Too bad!

We have a chance to redeem ourselves in October, but should we miss it, another five years of the same shit will for sure send us into a Banana Republic.
Pure balderdash.
 
Upuuzi huu umefunzwa wapi eti unatafsiri kwanini usiandike lugha moja tu
 
Unfortunately this is where our nation is headed. Too bad!

We have a chance to redeem ourselves in October, but should we miss it, another five years of the same shit will for sure send us into a Banana Republic.
October hakuna miujiza,watafanya michezo yao ile ile ya tangu 1995 mpk leo.
 
Unfortunately this is where our nation is headed. Too bad!

We have a chance to redeem ourselves in October, but should we miss it, another five years of the same shit will for sure send us into a Banana Republic.

Bahati mbaya nchi ikiwa a pariah state, wananchi wengi wanakuwa hawajui hilo, wanakuwa wameshazoezwa umaskini, mahangaiko na shida.

Watu wachache wanaopinga kwa nguvu zote haya yanayoendelea sasa ndiyo ngao ya mwisho iliyobaki. Itafika muda watapotea wote either kwa kukimbia nchi, kufa, kuwa jela au kukata tamaa na baada ya hapo, mahangaiko haya yatakuwa normalized.

Bahati mbaya Jumuia ya Kimataifa huwa wanakuwa slow sana kuchukua hatua. Sioni kama taifa tukiwekewa vikwazo au kuvamiwa ila hatutapata wawekezaji wa maana na maisha ya mtanzania mmoja mmoja hayataboreka.

Tunaweza kuishi kwenye hali hii hata kwa miaka 30 ijayo. Inasikitisha ila nadhani ndiyo ukweli.
 
Sijui hizi fikra huwa mnazitoa wapi! Belarus hawajui kuhusu barakoa, lockdown wala nini. Kazi zimeendelea kipindi chote. Mechi za ligi zimepigwa kipindi chote na kubet tumebet na kula na kuliwa tukiwa lockdown huku. Rais anawaambia wananchi wake, "...kabla hujaenda kazini, kunywa glass moja ya Vodka. Kabla hujaenda kuangalia mechi, kunywa glass moja ya Vodka. Corona utaisikia kwa jirani". Belarus haijawa Pariah State!

Lakini kwa Tanzania na kwa hatua zote ilizochukuliwa kwasababu haikuwa na lochdown, tayari unaleta mambo ya Pariah State!! Huu ni ujinga na upumbavu! Na nakuhakikishia, omba uombavyo! Toa kafara uwezavyo, nchi hii haitakuwa Pariah State na itazidi kusonga mbele! Na atakayejaribu kuikwamisha, atakwama yeye!
 
Sijui hizi fikra huwa mnazitoa wapi! Belarus hawajui kuhusu barakoa, lockdown wala nini. Kazi zimeendelea kipindi chote. Mechi za ligi zimepigwa kipindi chote na kubet tumebet na kula na kuliwa tukiwa lockdown huku. Rais anawaambia wananchi wake, "...kabla hujaenda kazini, kunywa glass moja ya Vodka. Kabla hujaenda kuangalia mechi, kunywa glass moja ya Vodka. Corona utaisikia kwa jirani". Belarus haijawa Pariah State!

Lakini kwa Tanzania na kwa hatua zote ilizochukuliwa kwasababu haikuwa na lochdown, tayari unaleta mambo ya Pariah State!! Huu ni ujinga na upumbavu! Na nakuhakikishia, omba uombavyo! Toa kafara uwezavyo, nchi hii haitakuwa Pariah State na itazidi kusonga mbele! Na atakayejaribu kuikwamisha, atakwama yeye!
Hiyo Belarus unayoitolea mfano pamoja na kuwa na idadi ya watu 9,449,510 ni nchi ya ishirini na mbili duniani kuwa na maambukizi mengi ya virusi vya COVID-19.
Maambukizi nchini humo ni 38,059 na wameshakufa watu 208 kwa ugonjwa wa Corona.
Wakati rais wao analichukulia janga hili poa kwa dharau na kejeri eti watu wake wajipigie vodka,taifa la Belarus linaangamia.
Tusubiri time will tell.
 
Hiyo Belarus unayoitolea mfano pamoja na kuwa na idadi ya watu 9,449,510 ni nchi ya ishirini na mbili duniani kuwa na maambukizi mengi ya virusi vya COVID-19.
Maambukizi nchini humo ni 38,059 na wameshakufa watu 208 kwa ugonjwa wa Corona.
Wakati rais wao analichukulia janga hili poa kwa dharau na kejeri eti watu wake wajipigie vodka,taifa la Belarus linaangamia.
Tusubiri time will tell.
Na Marekani inayochukua tahadhari zote dhidi ya maambukizi ni ya ngapi kwa maambukizi duniani mkuu?
 
Hiyo Belarus unayoitolea mfano pamoja na kuwa na idadi ya watu 9,449,510 ni nchi ya ishirini na mbili duniani kuwa na maambukizi mengi ya virusi vya COVID-19.
Maambukizi nchini humo ni 38,059 na wameshakufa watu 208 kwa ugonjwa wa Corona.
Wakati rais wao analichukulia janga hili poa kwa dharau na kejeri eti watu wake wajipigie vodka,taifa la Belarus linaangamia.
Tusubiri time will tell.
Sasa umeshaambiwa hofu inaua hata kuliko Corona. Jipe moyo ndo usurvive.
 
Au Brazil ambao nao Rais alikuwa jeuri kuwa hakuna shida sasa watu wote hawataki kumwona hata wa chama chake ila kwa kuwa huku ukisema tu njia sahihi ya kitaalamu unatumbuliwa
Hiyo Belarus unayoitolea mfano pamoja na kuwa na idadi ya watu 9,449,510 ni nchi ya ishirini na mbili duniani kuwa na maambukizi mengi ya virusi vya COVID-19.
Maambukizi nchini humo ni 38,059 na wameshakufa watu 208 kwa ugonjwa wa Corona.
Wakati rais wao analichukulia janga hili poa kwa dharau na kejeri eti watu wake wajipigie vodka,taifa la Belarus linaangamia.
Tusubiri time will tell.
 
Katika miaka ya hivi karibuni, kuna mambo mengi sana yamefanyika nchini Tanzania ambayo yamerudisha nyuma sana juhudi za kujenga jamii iliyostaarabika, inayojiheshimu na inayoheshimika.

Leo sitamnyooshea kidole yoyote kwa lawama hizi ila naomba nigusie tu madhara ya kuwa ‘a pariah state’.

Kwa mujibu wa mtandao wa Wikipedia:

“A pariah state (also called an international pariah or a global pariah) is a nation considered to be an outcast in the international community. A pariah state may face international isolation, sanctions or even an invasion by nations who find its policies, actions, or its very existence unacceptable.”

Kwa tafsiri isiyo rasmi ni kuwa “a pariah state ni taifa ambalo Jumuia ya Kimataifa imeliona kuwa halina hadhi au sifa za kuwa katika Jumuia hiyo. Na taifa hilo kama lisipojirekebisha huwa linaenda kutengwa, kuwekewa vikwazo, na hata kuvamiwa. Katika macho ya dunia, sera, matendo na hata uwepo wa taifa la namna hiyo ni vitu ambavyo havikubaliki”.

Kiufupi kuwa a pariah state, au an outcast siyo jambo zuri. Linakunyima vingi. Ndiyo, utabaki na uhuru wako wa kujifungia ndani na kujiamulia mambo yako wakati wenzako wanajumuika na kufurahi pamoja. Kuwa an outcast siyo jambo zuri kwa mtu mmoja mmoja na hata kwa taifa.

Kwenye issue ya corona, Tanzania tuliona tuangalie kwanza maslahi ya taifa na tukaweka pembeni jukumu letu kama sehemu ya Jumuia ya Kimataifa.

Kutoa takwimu na taarifa rasmi na za uhakika za mambo kama maambukizi ya milipuko, ni moja ya majukumu yetu. Taarifa hizi zinasaidia dunia na wataalamu kujua mwenendo wa maambukizi na ndiyo msingi wa jinsi Jumuiya ya Kimataifa inatumia kujua wapi pa kusaidia. Fikiria kila taifa lingesema, sisi hatupimi na hatutoi taarifa zozote, leo dunia ingekuwa kwenye hali gani?

Tunatumia takwimu za wengine kuwazodoa kuwa wao corona imewapiga kweli kweli ila sisi takwimu zetu hatutaki kuzitoa.

Tunapowaza kuwa a pariah state, embu tuangalie taifa kama Eritrea limefaidika vipi kwa hali hiyo na ni hasara gani wamepata. Na hapo hata sijazungumzia mambo ya haki za binadamu na utawala wa sheria.

Naomba tujitafakari, nadhani kuna njia bora zaidi kuliko hizi tunazochukua.

NYONGEZA:

Sijui tafsiri rasmi ya kiswahili ya ‘a pariah state’ ila ukiniuliza mimi nitasema ni ‘taifa la kihuni’.
Duh!
Si nasikia lakini mamisaada yanaanza kuflow!
 
Unfortunately this is where our nation is headed. Too bad!

We have a chance to redeem ourselves in October, but should we miss it, another five years of the same shit will for sure send us into a Banana Republic.

Very unfortunate indeed. God forbid!
Without a new recommended Tanzania Constitution and an Independent Election Comission, CCM YA MAGUFULI is there to stay.
It needs the Powerful Hand of The Almighty God to get out of this shit!
 
Back
Top Bottom