Je, TAESA bado inafanya kazi?

Je, TAESA bado inafanya kazi?

EEM M

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2022
Posts
475
Reaction score
980
Habari wana JF,

Leo nimeona nianzishe huu uzi ili kupata hoja zenu maana naamini hapa ndo home of intelligent.

To make it short, kuna huu mfumo wa Serikali wa TAESA ambao ulikuwa unajihusisha na kuwasaidia vijana hasa graduates kupata internship na kazi.

Mfumo huu ulikuwa ni useful sana hasa kwa vijana ambao wanamaljza chuo na hawana waya mrefu (connection) kupata nafasi za kujitolea au hata kupata kazi.

Lakini siku za hivi karibuni mfumo huu umekuwa ni kama haufanyi kazi. Yani hauruhusu watu wapya kufungua account (creating of new accounts).

Nimejaribu mara nyingi sana kutumia kwa kutumia simu bila mafanikio lakini pia nikajaribu kutumia PC mambo bado yakawa vile vile maana wananiletea notification kuwa "This site can't be reached"

Mwenye uelewa na huu mfumo anakaribishwa kuchangia.

Je, bado unafanya kazi? Au serikali imeamua kuufungia? Je, kuna mbadala wa huu mfumo mbali na ajira portal (japo natambua ajiraportal haitoi internship)? Kama upo mwingine, ni upi?

Karibuni wana JF
 
Kwa sasa tumerudi tena enzi zileee!! Za kuulizana wewe ni mtoto wa nani? Baba yako ana nafasi gani kwenye chama na serikali, nk.
Na hii ndo inajenga chuki kwa serikali na utawala
 
Unashangaa zaidi ukisikia Ni kitengo Rasmi cha Huduma za Ajira ndani na nje ya nchi chini ya ofisi ya Waziri Mkuu.

Nashauri, kwa vile mambo ya Bure mengi yamekuwa nuksi na Yameleta maafa kwa Wanyonge ni bora kila ofisi ya umma na Taasisi ikiwemo TaESA ikawa na Private wing kama Hospitali na vituo vya afya.

Mana kama mtu alisoma kwa vipesa vyake na msaada kidogo wa Gov. Hatashindwa kumalizia mkia hata akiuza vimbuzi kule loliondo kuliko kukaa mwaka mzima unasubiri kuitwa kisa huduma za Umma za Bure. Hii ni Mbaya na inachafua mpaka PM office.
 
Kwa sasa tumerudi tena enzi zileee!! Za kuulizana wewe ni mtoto wa nani? Baba yako ana nafasi gani kwenye chama na serikali, nk.
Kuna kazi zilitoka kwenye chama pendwa, wakawa wanataka lazima uwe na Kaf ya chama Chao, Kama hauna pisha mbali.
 
To make it short, kuna huu mfumo wa Serikali wa TAESA ambao ulikuwa unajihusisha na kuwasaidia vijana hasa graduates kupata internship na kazi.
Ukiomba Internship ofisini kwetu bila Endorsement ya TAESA tunakurudisha, so from my office point of view Yes Taesa inafanya kazi
 
Kuna kazi zilitoka kwenye chama pendwa, wakawa wanataka lazima uwe na Kaf ya chama Chao, Kama hauna pisha mbali.
Daaah!, Ndo mana watu wanajitosa tu ata bondeni [emoji28]
 
Back
Top Bottom