ABC news na Fox news za Marekani wamereport habari hii katika namna ambayo inatujengea taswira mbaya!
Watalii tutawasikia kwenye bomba,mtalii gani atakayesikia habari hiyo halafu aje?Si ataona nchi ni ya kidikteta
[HASHTAG]#freemaxence[/HASHTAG]
Wala tusitie shaka na huzuni mioyoni mwetu, kadri giza linavyozidi ndio asubuhi iko karibu sana tofauti na tunavyofikiria..
tushikana pamoja tupige kelele japo wametuwekea maji midomoni mwetu, hata kwa kukoroma tutapiga kelele
[HASHTAG]#freemaxence[/HASHTAG]
Walingoe bunge meno liwe kibogoyo, waingilie mahakama, Watumie dola kufanikisha matakwa yao ila watuachie JF yetu!
Tunaomba hilo tu jamani, and i believe it is not too much to ask! please
Kama nilivyoahidi; waasisi na wadau wa JF tuna maamuzi ambayo tutayafanya ili kulinda uwepo na uthabiti wa JF. Wakaopoteza ni wale wanaofikiri wamepata.
Hivi ule uhuru watu walishereheka hivi majuzi ulikuwa wa kushangilia kuchukua kiti cha mkoloni mzungu kuwaziba midomo wananchi wasimkosoe Na kusema ukweli Na kudai haki zao ?